Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Kwenye pitapita zangu nimekutana na tangazo hili kutoka kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance ikitangazia umma kuhusu Bi Neema Vegula kuwa sio sehemu ya familia ya Jubilee Insurance.
Ukilisoma tangazo hili limekaa kimtego sana na kwa upande mwingine sidhani kama linafuata miongozo na sera za Rasilimali Watu katika Kampuni ya Jubilee. Je Neema ameacha kazi, amestaafu, amefukuzwa, ameiba, amehamia kampuni nyingine?
Maana Kwa taarifa hii sisi tutaona mmemfanyia figisu huko ofisini na wasiompenda Hadi akaachishwa kazi, tunajua changamoto ya fitina maofisini.
Sidhani kama hii imekaa sawa kwa pande zote mbili, hapo mnazidi kumchafua Bi Neema na kumnyima fursa ya kupata kazi sehemu zingine. Kama ameiba au amefanya jambo baya ni vyema kuweka umma wazi.
Ukilisoma tangazo hili limekaa kimtego sana na kwa upande mwingine sidhani kama linafuata miongozo na sera za Rasilimali Watu katika Kampuni ya Jubilee. Je Neema ameacha kazi, amestaafu, amefukuzwa, ameiba, amehamia kampuni nyingine?
Maana Kwa taarifa hii sisi tutaona mmemfanyia figisu huko ofisini na wasiompenda Hadi akaachishwa kazi, tunajua changamoto ya fitina maofisini.
Sidhani kama hii imekaa sawa kwa pande zote mbili, hapo mnazidi kumchafua Bi Neema na kumnyima fursa ya kupata kazi sehemu zingine. Kama ameiba au amefanya jambo baya ni vyema kuweka umma wazi.