jua kali sana radi inatoka wapi!

white wizard

JF-Expert Member
May 18, 2011
8,307
13,269
kweli tembea uone maajabu usisubili kuambiwa mambo ya sumbawanga,leo hii hapa mpanda(katavi)imepiga radi hiyo huku jua ni kali sana hadi imeunguza laptop yangu jamani,cha ajabu nyumba niliyofikia ina circuit braker ikajizima!ila haikusaidia!ila wenyeji wa huku wanasema hiyo ilikuwa inatafuta mtu,nilijua ni bomu kwani sijawahi shuhudia radi huku jua linawaka!cjui wanasayansi mnatwambia nini?
 
Huko ukimuudhi mtu anavua shati na kulitundika hewani ili mzitwange!!
 
Ndo ujue s'wanga sio mchezo, pole kwa kuunguliwa na laptop

Mkuu,nashukuru ila nimeogopa sana!nilidhani niko ndotoni!,kumbe adaptor ndio imeungua nimejaribishia kwa jamaa imewaka,ukisikia hatari ndio hii,mpaka sasa wageni tunaizungumzia,ila kwa wenyeji sio stori!
 
Mdau, hiyo ni trailer tu...picha kamili subiri vua zianze!!, hapa tunakosa raha ya kuangalia epl kwani hata wenye cable wameziima mitambo Yao!!! Kwakweli ni noumer!!!!
 
kweli tembea uone maajabu usisubili kuambiwa mambo ya sumbawanga,leo hii hapa mpanda(katavi)imepiga radi hiyo hu ku jua ni kali sana hadi imeunguza laptop yangu jamani,cha ajabu nyumba niliyofikia ina circuit braker ikajizima!ila haikusaidia!ila wenyeji wa huku wanasema hiyo ilikuwa inatafuta mtu,nilijua ni bomu kwani sijawahi shuhudia radi huku jua linawaka!cjui wanasayansi mnatwambia nini?[/QUOTE

Mpanda ni mkoa wa katavi na sumabawanga ipo mkoa wa rukwa
 
Poleni sana kwa hali iliyotokea kila watu na yao mkuu.Hiyo ni miji ya wenyewe so kaa nao kwa tahadhari but they are good people if you are good to them.Be wise!
 
Ukanda huo ndio makombora yao, ni hadi Kigoma. Hiyo ni sayansi yetu wazungu hawaiwezi.
 
Wataalamu wa masuala ya mvua mmepata kwa kuanzia ili kuweza kufanya tafiti zakuyaamuru maji ya Ziwa Rukwa kuwa mvua isiyo na madhara. Kazi ni kwenu ....
 
Kuna makala moja kwenye gazeti la Mwananchi walielezea hizo radi na zinauzwa kati ya shilingi elfu 30,000-40,000.
 
Yaani huko mvua zinanyesha kwenye shamba la flani tu.
Pale kwenye mpaka wa shamba ulipoishia na mvua inaishia hapohapo.
 
sumbawanga manake TUPA WANGA
ukienda huko kama huna kitu hawakutafuti
labda wamehisi unataka kuwaibia wake zao.
au umeingia anga za watu huku ukiwa nguvu za roho mt,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom