JOSHUA NASSARI: The Lord of the Rings: The Return of the King

3D.

JF-Expert Member
Sep 7, 2010
1,018
282
Kwa wale waliotazama mfululizo wa sinema tatu (Trilogy) za The Lord of the Rings (The Fellowship of the Ring, The Two Towers na The Return of the King) wataona kuwa CCM imekuwa ikitishia watu kama mzimu wa Sauron. Watu watapambana lakini akifika Sauron majeshi yote yanaangukia mikononi mwake. Mwisho wake ilibidi ateuliwe mtoto mdogo dhaifu Frodo (Joshua Nassari) ili akaitupe pete ya uchawi ya Sauron. Alipitia wakati mgumu sana hadi kufanikisha Aragon (Watanzania) kuwa mfalme (The Return of the King).

Hivyo nikifananisha matukio ya mfululizo huu:
  1. The Fellowship of the Ring: Nassari, Vicent Nyerere, Mbowe, Slaa, Lwakatare, wafuasi wote wa CDM na Watanzania kwa ujumla waliunda Fellowship (Umoja) ili kuuangusha mzimu wa Sauron (CCM)
  2. The Two Towers: Ni mapambano makali katika kata mbalimbali (Towers) za Arumeru Mashariki. Wakati mwingine Frodo (Joshua Nassari) alipata mashambulizi makubwa ambayo baadhi yetu yalitupa hofu juu ya kufanikiwa mission yetu. Gandalf the Grey (Mbowe, Slaa etc) alikuwepo na farasi (Helkopta) kusaidia mapambano katika hatua ambazo zilionekana ni ngumu sana.
  3. The Return of the King: Battle is seriously fiercer now. Frodo gets so close to the victory but Gollum (Tume ya Uchaguzi, TISS, Tendwa, Rushwa, Polisi etc) anajaribu walau kwa dakika ya mwisho kuchelewesha ushindi. Hatimaye pete ya uchawi (hofu juu ya CCM) yatupwa, na Aragon (Watanzania) awa Mfalme.

I highly recommend these films. The Lord of the Rings: The Return of the King is 5th highest grossing film in history behind Avatar, Titanic, Harry Potter and the Deathly Hallows Part 2 na Transformers: Dark of the Moon.

Tusiidharau CCM. Tusiipe credit sana CCM. Tulinde kura hata hivyo.

Movement for Change,
Movement for Chadema.

THE LORD OF THE RINGS: THE RETUN OF THE KING!!!
 
Thanx 3D,
Umenifanya niiangalie tena sinema ya The Lord of The Rings
kwa kuanza na mfululizo kama ulivyo: The Fellowship of The Ring,
The Two Towers na kumalizia na ile ya The Return of The King.
This is what we call VISUALIZATION...
 
Thanx 3D,
Umenifanya niiangalie tena sinema ya The Lord of The Rings
kwa kuanza na mfululizo kama ulivyo: The Fellowship of The Ring,
The Two Towers na kumalizia na ile ya The Return of The King.
This is what we call VISUALIZATION...

Director Peter Jackson alifanya kazi kubwa kweli. Nikuulize swali la kizushi, unadhani itachukua muda gani kwa sisi Watanzania kuweza kuandaa filamu yenye kiwango kama hicho?
 
Director Peter Jackson alifanya kazi kubwa kweli. Nikuulize swali la kizushi, unadhani itachukua muda gani kwa sisi Watanzania kuweza kuandaa filamu yenye kiwango kama hicho?

Hadi pale tutakapoacha kuendekeza siasa hata kwa mambo ya msingi...
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Hadi pale tutakapoacha kuendekeza siasa hata kwa mambo ya msingi...

Ila itachukua muda kwa politics kuacha interference katika mambo ya msingi. Maybe something has to be done. Honestly, katika sinema nazofikiria kuandaa nitakuwa nachomeka vijembe kwa watu wa politics. Kuna filamu naifikiria, nitakutaarifu.
 
Back
Top Bottom