Joshua Nassari apata ajali ya chopa

mmaranguoriginal.

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2014
Posts
4,060
Reaction score
460
Wanabodi nawasalimu sana.

Nimepewa taarifa muda huu kuwa mbunge Wa Arumeru Mashariki, ndugu Joshua Nassari, amepata ajali muda huu akiwa maeneo ya Leguruki.

Mosi, inasemekana amenusurika na amepata majeraha madogo lakini mmoja Wa abiria wake kavunjika mguu.

Nitazidi kuwajuza kadri nitakavyopokea taarifa.

Nawasilisha.

******** Updates *********

Mbunge amekimbizwa katika Hospitali ya Selian na kwa mujibu wa Katibu wa mbunge hajaumia sana, ila abiria wawili mmoja anajulikana kwa jina la Eve ambaye ni mmoja wa viongozi wa BAWACHA jimboni kaumia mbavu na mwingine kavunjika mguu.

Tupo jimboni na tunawatoa hofu wananchi wote waliopata taharuki jimboni kuwa Mbunge ni mzima amepatwa na majeraha kidogo!!

Tunamshukuru Mungu kwa rehema zake.



Mbunge Nassari azungumzia ajali, Ndesamburo kununua chopa mpya!
 
Hizi habari ni za ukweli kamanda Nassari amepata ajali ya helkopita leo wakati akitoka kwenye kampeni za kuhamasisha watu kujiandikisha taarifa ambazo hajithibitishwa Nassari ameumia ambulance ipo njiani ndo inampeleka katika hospital selian Arusha
 
Mbunge amekimbizwa ktk Hosptal ya Selian na kwa mujibu wa Katibu wa mbunge hajaumia sana ila abiria wawili mmoja anajulikana kwa jina la Eve ambaye ni mmoja wa viongozi wa BAWACHA jimboni kaumia mbavu na mwingine kavunjika mguu.

Tupo jimboni na tunawatoa hofu wananchi wote waliopata taaruki jimboni kuwa Mbunge ni mzima amepatwa na majeraha kidogo!!

Tunamshukuru Mungu kwa rehema zake.
 
twashukuru sanaaa ndg.kwa taarifaa hizoo unapopata zingine just expose
 
Taarifa kutoka kwa Ndote Katibu wa Mbunge Mbowe juu ya ajali Hii hapa
í-½í±‡í-½í±‡í-½í±‡

Chopper imepigwa na storm kwa takriban dk 2. Pilot amefanikiwa kufanya landing manouvre lakini kimbungaa kilikuwa kikali sana. Ndege imecrash abiria wameumia kiasi tu. Wamepelekwa Selian Hospital.

Ndege imebaki vipande. Nimeongea na pilot akiwa na tune nzuri tu. Wenzake walikuwa wametangulia hospitalini. Tuwaombee wapate nafuu haraka.
 
Eti,kapata vijeraha vidogo?na pia kavunjika mguu mmoja wapo?
sidhani!!!
 
Nasari kwa nn anatumia chopa kipindi hiki?
 
Pole kwake dogo janja na wenzake!!!Mungu awape ahueni haraka
 
Hizi habari ni za ukweli kamanda Nassari amepata ajali ya helkopita leo wakati akitoka kwenye kampeni za kuhamasisha watu kujiandikisha taarifa ambazo hajithibitishwa Nassari ameumia ambulance ipo njiani ndo inampeleka katika hospital selian Arusha

Mkuu thanks,
 
get well our Mp and all who got injured

God will stand with you
 
Ni kwamba anashindwa kuzungukia jimbo kwa gari? Juzi tu hapa nimepost kuhitaji kujua umuhimu na ulazima wa Nassari kutumia chopa ndani ya jimbo kama sio ufujaji wa pesa... but pole kwake
 
Mungu awaponye makamanda wote walihusishwa na ajali hiyo.Mapambano yanaendelea
 
Haya ndiyo madhara ya kupuuza utabiri wa hali ya hewa, mbona jana TMA walitoa tahadhari ya weather today.Poleni wajeruhiwa mnatakiwa mheshimu utaalamu
 
Ni kwamba anashindwa kuzungukia jimbo kwa gari? Juzi tu hapa, nimepost kuhitaji kujua umuhimu na ulazima wa Nassari kutumia chopa ndani ya jimbo kama sio ufujaji wa pesa... but pole kwake

Hiyo pesa anatoa wapi kukodi chopa?
 
Haya ndiyo madhara ya kupuuza utabiri wa hali ya hewa, mbona jana TMA walitoa tahadhari ya weather today.Poleni wajeruhiwa mnatakiwa mheshimu utaalamu

Mkuu hao ni wapinzani, kila amri itokayo kwa watendaji wa serikali wameagizwa kuipinga tu, na hii ya hali ya hewa nayo watadai aliyeitoa kaajiriwa na ccm hivyo sio rahisi kutii amri hiyo. Poleni majeruhi.
 
Mkuu hao ni wapinzani, kila amri itokayo kwa watendaji wa serikali wameagizwa kuipinga tu, na hii ya hali ya hewa nayo watadai aliyeitoa kaajiriwa na ccm hivyo sio rahisi kutii amri hiyo. Poleni majeruhi.

kumbee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…