Joram Kihango vs Willy Gamba

daaaah, WILLY GAMBA, bonge la sterling! na visa vya mapenzi ndani! aisee natamani nitafute na kuzisoma tena!
Tokea jamaa E.A.Musiba amefariki sijui kama tutapata tena. ilifaa familia yake isimamie tena uchapaji wa vitabu ili visipotee. ni kweli alikuwaamejikita mwenye ukombozi wa afrika na hasa dhidi ya makaburu lakini maudhui yake hayapotei.
 

hapa unapoongea narudia 24hrs kwa mara ya sita!!!!
 
Umenikumbusha mbali sana,uncle wangu nowdays ni shushushu baada yakuvutiwa na kazi
za hao jamaa,nitapata wapi hivyo vitabu?
Waandishi wa siku hizi Hussein Tuwa anajitahidi,pia yupo Beka Mfaume na Innocent Ndayanse.
 
Willy Gamba alikuwa kiboko. Umenikumbusha Veronica maskini lakini hakufa kijinga aliondoka na watu.
Bado kitabu nilikisoma nikiwa kijijini lakini Musiba alivyo portray mitaa ya Dar Nilikuwa najiona Nipo Dar lol!
 
Kwa sasa majeshi nimehamishia kwa Hussein Tuwa, Mdunguaji na Mkimbizi ni noma sana
 
you guys..long time. Kuna kitabu nlikisoma nliazima library ya arusha mkoa, kinaitwa MBIO ZA JASUSI..dah kilikua nooma. those days..
 
you guys..long time. Kuna kitabu nlikisoma nliazima library ya arusha mkoa, kinaitwa MBIO ZA JASUSI..dah kilikua nooma. those days..

Dah! nimekikumbuka lakini mwandishi wake nimemsahau. Kulikuwa na Hammie Rajabu AMA ZAO AMA ZANGU, Nadhani aliandika pia dimbwi la damu na simu ya kifo. kilichonifanya nikumbuke ni uwezo wa kuongeza kujua kusoma na kuandika ulioongezwa na matokeo ya kusoma kitabu kwa haraka kabla hujanyang'anywa. Unajua Tanzania ya sasa watoto hawasomi kabisa na hawana namna ya kujiongezea maarifa kupitia vitabu. Kwa wenzetu watoto wanasoma sana tangu wakiwa wadogo.
 

walikuwepo ma staring wazuri wengi... Edie Kakhi... Kwenye unyama wa mafia! Na majambazi kama Dr. MOTOWN.. AKA mzungu katili, KABWE MAKANIKA... Aka Jitu kumbuka... Akina jarufu Ram na mzee Helgal ajenti wa MAFIA tanzania... PIA KILIKUWEPO KITABU mbio za jasusi... Nakikumbuka saaaana na staring alikuwa mkali saana! Baadae tukasoma MASHIMO YA MFALME SULEIMAN... tukamuona UMBOPA.. aliefundishwa vita na UMSOLOPOGAAS! NA PIA tukasoma HADITHI YA ALLAN QUATERMAIN.. NIKAMUONA umsolopogaas na shoka lake INKSOKAZ! HAKIKA hivi vitabu vya alan quatermain niliamini ni vya kweli. Na mtunzi aliitwa H. RIDER. HAGARD. ni mwingereza maarufu sana wa karne ya 20!
 
Kwa kweli mpingauonevu umenikumbusho mambo ya muda kwa kweli majira tulionao sidhani kama kuna mstaa kama hao.

Wale waliotangulia mbele ya haki na Bwana awape pumziko la milele shambani mwake!
 
Last edited by a moderator:
Nadhani bado nakumbuka kidogo............
Kufa na Kupona-Wizi wa Karatasi za Siri
Njama-Harakati za Ukombozi Kusini mwa Afrika
Kikosi Cha Kisasi-Mtanange ulikuwa pale DRC Kongo
Kikomo-Wizi wa Almas Mwadui
Hujuma-

I stand to be corrected......Hivi Mkuu wapi ntapati vitabu hivi?
 
Ili kuwaenzi hawa magwiji wa riwaya ni vizuri mwenye softcopy ya vitabu vyao waviweke hapa ili tuvisome
 
Reactions: SG8
Dah umenikumbusha mbali. Kitabu cha njama nilikipenda zaidi.
 
Kuna mtu anaweza kutoa msaada wa jinsi ya kupata hivyo vitabu,hususani hicho cha NJAMA
 
yeah,mtunzi wa kabwe makanika,JITU KUMBUKA alikua zahily ally zorro babake banana zorro.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…