13 Oct 2019
Hakuna makutano ya kifikra baina ya Ofisi mbili kuu, yaani Ofisi ya Rais Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inayosimamia uchaguzi wa serikali za mitaa na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inasimamia masuala ya siasa, hayo yamesemwa na Mzee John Shibuda na hivyo anasema kuna pahala pana mushkeli mkubwa katika matayarisho na mipango kuelekwa uchaguzi wa serikali za mitaa.
John Shibuda anasema hoja nzuri za wadau wa siasa kama vyama vya siasa zilipuuzwa na serikali na ndiyo tunaona hali hii ya kusuasua katika kujiandikisha.
Wakati taifa likielekea wiki ya kilele cha maadhimisho ya kifo cha baba wa taifa, Mwalimu Julius Nyerere pia tunaelekea katika hitimisho la wiki ya uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mtaa. Zoezi hilo limeonekana kulega lega kwa baadhi ya maeneo. Je, kuna tatizo mahali? Tunajadili hayo kiundani katika MIZANI YA WIKI inayoongozwa na Nurdin Selemani akiwa na mkuu wa wilaya ya kinondoni, Daniel Mchongolwa, mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa John Shibuda, mhadhiri wa idara ya sayansi ya siasa ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda.
Source: Azam TV
Hakuna makutano ya kifikra baina ya Ofisi mbili kuu, yaani Ofisi ya Rais Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inayosimamia uchaguzi wa serikali za mitaa na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inasimamia masuala ya siasa, hayo yamesemwa na Mzee John Shibuda na hivyo anasema kuna pahala pana mushkeli mkubwa katika matayarisho na mipango kuelekwa uchaguzi wa serikali za mitaa.
John Shibuda anasema hoja nzuri za wadau wa siasa kama vyama vya siasa zilipuuzwa na serikali na ndiyo tunaona hali hii ya kusuasua katika kujiandikisha.
Wakati taifa likielekea wiki ya kilele cha maadhimisho ya kifo cha baba wa taifa, Mwalimu Julius Nyerere pia tunaelekea katika hitimisho la wiki ya uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mtaa. Zoezi hilo limeonekana kulega lega kwa baadhi ya maeneo. Je, kuna tatizo mahali? Tunajadili hayo kiundani katika MIZANI YA WIKI inayoongozwa na Nurdin Selemani akiwa na mkuu wa wilaya ya kinondoni, Daniel Mchongolwa, mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa John Shibuda, mhadhiri wa idara ya sayansi ya siasa ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda.
Source: Azam TV