John Cheyo: Mazungumzo ya maridhiano kuendeshwa kwa gredi yaani ya 'ukubwa' wa vyama viwili tu siyo sahihi

19 February 2023
Dar es Salaam, Tanzania

ACT-Wazalendo wafungua mikutano ya hadhara kwa maandamano

 
16 February 2023
Dodoma, Tanzania

Waziri wa kilimo Mh. Hussein Bashe atembelewa na ujumbe mzito wa makatibu wa kanda CHADEMA, na wajumbe hao kuelezewa hali ya sekta ya kilimo Tanzania ilivyo ....

1677089140571.png
 
17 February 2023

Mzee John Cheyo - Hili la vyama vinavyojiita Chama Tawala na Chama Kikubwa kuteka agenda za nchi halikubaliki



Mwenyekiti wa chama cha UDP Mh. John Cheyo alalamika siasa kuwekwa "gredi" vyama gani vinaweza kujadili katiba ya nchi, maana kwa sasa suala hili linajadiliwa na vyama viwili tu kimoja kinajiita ni tawala na kingine ni chama 'kikubwa' huku vyama vingine vinavyoitwa vya mfukoni vikiachwa nje ya mjadala huu mkubwa.

Mzee Cheyo anasema umri wake umamueleza kuwa leo chama kinaweza kuwa kikubwa na tawala lakini kesho kikawa kidogo hivyo ikitokea mazungumzo muhimu je chama hicho huko miaka ijayo kitabaguliwa ?

Anaongeza kuwa ustaarabu wa kisiasa uwe katika nyanja zote na siyo lugha tu. Hili la ukubwa na huyu mtawala haikubaliki hivyo baraza la vyama la siasa lipewe hatamu na jukumu la kuongoza mazungumzo yatayojumuisha vyama vyote badala ya vyama viwili kujifungia chumbani bila wananchi kushirikishwa na ushirikishwaji ndiyo people's power ya wale rafiki zetu.

Mkongwe huyo wa siasa anasema maisha ni magumu ni katika mifuko yao wananchi inayosababishwa na bei ya mafuta kupanda. Hivyo hii ya serikali kuamua kuagiza mchele kutoka nje haitasaidia kupunguza bei ya mchele dukani.

Jibu la kukabiliana na mfumuko wa bei ni kutumia neno moja tu ruksa la rais mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi na hivyo bulk procurement ya wachache kuagiza (kununua) mafuta ndiyo mzizi wa mfumuko wa bei /root cause ya mfumuko wa bei unaonufaisha wanunuzi wachache wa mafuta kupitia bulk procurement.

Ruksa ya Mzee rais Ali Hassan Mwinyi kuacha milango wazi kwa kila kitu ndiyo jibu endelevu / sustainable la kukabiliana na mfumuko wa bei hivyo EWURA na TBS wabaki kuwa wasimamizi wa ubora wa bidhaa na baada ya hapo bei ya mafuta itakuwa chini ya Tshs 2,000 kwa lita na hili litapelekea mfumuko wa bei wa kila kitu nchini kwenda chini na maisha kuwa nafuu.

Wafanyabiashara wa vitu na bidhaa zote hata mafuta lazima wawe wengi na ndiyo unafuu kwa maisha ya wananchi utapatikana, hii zimamoto ya kusimamia bei ya mafuta au kuagiza mchele toka nje kukabiliana na ughali wa maisha siyo suluhisho la kudumu.

John Cheyo mfanyabiashara wa siku nyingi anasema watanzania zaidi ya nusu hawaishi mashambani, bali wanaishi mijini na shamba lao ni mifukoni hivyo mchele toka Katavi, Shinyanga na Mbeya kuwa juu kwa walaji wa mijini unasababishwa na bei ya juu ya nishati ya mafuta ya dizeli na siyo vinginevyo pia wala ruzuku haitasaidia jibu ni neno ruksa kuruhusu biashara huria ya wafanyabiashara wengi wa biashara za ndani na nje.

Mzee John Cheyo anafurahishwa na waziri wa kilimo Hussein Bashe kutoyumbishwa na mbinyo wa kelele za kutoa bei elekezi kwa mazao ya wakulima au kufunga mipaka wakulima kuuza soko la nje. Mazao ni Mali ya wakulima anasisitiza Mzee John Cheyo na hiyo ndiyo sera ya UDP ya kuwajaza mapesa watanzania ikiwemo wakulima.

Huyu Mwenyekiti wa kudumu wa UDP aamke sasa ule mshiko toka kwa Mwendazake hautokuwepo tena
 
Mbeya, Tanzania

Mwenyekiti CHADEMA taifa Mh. Freeman Mbowe kunguruma mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Iringa katika mikutano ya hadhara



Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya kamanda China wa China afafanua kazi ya chama itakayofanywa na mwenyekiti wa CHADEMA taifa katika ujio wake kanda ya CHADEMA Nyasa
Source : Busokelo TV
 
Iringa, Tanzania

MWENYEKITI wa CHADEMA MKOA WA IRINGA - NI WAKATI WA KILIMO CHA TANZANIA KUWA CHA KISASA , ACHAMBUA HALI YA UCHUMI WA NCHI"



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoa wa Iringa William Mungai amezungumzia masuala mbali mbali ya siasa za Tanzania, Uchumi wa nchi, Tuachane na kilimo cha jembe la mkono ili tuzalishe kwa wingi nafaka Tanzania izalishe nafaka kama ngano kwa wingi kama inavyofanya Ukraine na Urusi tuuze nje.

Chadema ni chama kikubwa tupo kila kijiji na wilaya, mazingira ya kisiasa yamebadilika wanachama wetu waliokuwa wafungwa wa kisiasa wameachiwa kuna mwanga mzuri ktk uwanja wa kisiasa nchi inapumua sanjari na kutoa ushauri kwa serikali huku akipongeza baadhi ya mambo ikiwemo kuruhusiwa kwa mikutano ya hadhara, mahusiano baina ya Tanzania na mataifa mengine.

‘Hali ya kisiasa nchini inaimarika na hili nimpongeze sana Rais Samia kwa kuona kuwa zinahitajika sauti za wengi kwa kuwa nchi hii ni yetu sote.suala la mikutano ya hadhara ndiyo tiba ya maumivu ya wananchi kwa kuwa wananchi wanapata nafasi ya kuwauliza maswali viongozi wao na wao wanajibiwa hivyo nampongeza kwa kuliona hilo na sisi chadema tumejipanga na hapa Iringa siku si nyingi tutaanza mikutano ya hadhara kwenye maeneo yote ya mkoa.

CHADEMA tumewapigania sana media yaani vyombo vya habari na mitandao ya kijamii iwe huru ...

Tume Huru ya Uchaguzi na mabadiliko kupitia katiba mpya ni muhimu sana. Haki upande wa mahakamani ni muhimu sana lakini bado watu waliopo katika mfumo wa haki jinai bado wanaishi kama wapo katika mazingira ya awamu ya tano wakati sasa kuna awamu ya sita inayojitahidi kufungua nchini kwa kila namna

Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa CHADEMA anaelezea changamoto ya Ugumu wa kuanzisha na kufanya biashara nchini Tanzania kwa unatakiwa utazamwe upya uwe rafiki na utawezesha watu kujiajiri.


Mfumuko wa bei nchini pia freight charges kuleta mizigo Tanzania kutoka Dubai, China n.k ni changamoto hivyo serikali kutuelezea A-B-C ya matatizo bila A-B-C ya hatua gani ya kuchukua kupambana na hali hii ya kibiashara ndiyo kazi muhimi ya serikali kutatua kero anasisitiza mwenyekiti wa mkoa CHADEMA kamanda William Mungai.

Asilimia 40% ya mapato ya mtanzania inakwenda kwenye kugharamia chakula na mlo wa mwananchi.
 
Sasa mbona JPM mpaka aliapa kukiua CDM? Kama CDM ni cha mfukon kwann alipambana nao? Teka, tesa, uaaaa, filisi, wape kesi uhujumu,na kibaya zaid baada ya kuwanunua CDM akawapa na nafas za uongoz!!! Je ukijichunguza maneno yako huoni kama unaupungufu wa ubongo?
Roho ya Shetani isivyo na aibu, akawageuka wenzie..
 
Hv mnajadiliana nn na chama chenye wanachama wawili?? Yaani mume ndo mkiti Taifa, na mke ndo Katibu mkuu Taifa.. chama ambacho hakina kbs mtandao wa wanachama popote, kimeshindwa kuwashawishi hata majirani kujiunga nacho... Mzee cheyo na UDP yake ni ccm kwa 100% .. sasa wanaitwaje kwenye kujadiri katiba mpya wkt vinawakilishwa na baba yao ccm???
Uchaguzi uliopita kituo alichopiga kura Cheyo na mkewe walipata kura 1 na hakuna iliyoharibika... akili mu kichwa...
 
Wanaoridhiana ni wale waliokoseana au kuwa na uhasama, sasa John Cheyo na chama chake hakijawahi kuwa na matatizo na CCM au ameona buyu la asali limempita🐒
 
February 2023
Iringa , Tanzania

MBOWE AKIZUNGUMZA KATIKA HAFLA




Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Mh. Freeman Mbowe akizungumza katika hafla maalum jioni ya leo mjini Iringa alipokutana na wanaCHADEMA kuashiria kupiga hodi katika kanda ya Nyasa akiwa njiani pamoja na msafara wake akielekea Sumbawanga kwa ziara ya kikazi.
 
15 January 2023
Makambako, Iringa


UJENZI WA OFISI YA KUBWA YA CHAMA CHA CHADEMA JIMBO LA MAKAMBAKO UNAENDELEA KWA KASI



Mikutano ya hadhara itakuwa katika eneo hili na ujenzi unaenda kwa kasi kukaribisha na kupokea ugeni wa kitaifa toka makao makuu ya CHADEMA.

Wanachama jimbo la Makambako wamesema wanajitolea kwa moyo mmoja huku wakiwa na furaha kwa kutembea vifua mbele kukijenga chama kwa ajili ya kizazi cha sasa na kizazi kinachokuja ...
 
Bila ya mantiki...
Kwenye maridhiano kuhusu Ukweli na Haki Yafanyike baada ya Rais SSh kuwa nje ya Nyadhifa yake. Iwe ni 2025 au 2030.... Ikiwa na maana waliohusika kwa namna moja au nyingine wawe nje ya mfumo unaoweza legeza Haki kutendeka. Wawepo nje ya mapazia.

Vilevile Kuhusu Katiba

Vyama vikubaliane kwa pamoja, watoe tamko la pamoja kulinusuru Taifa hili kutoka kwa mikono ya mabeberu na Vibaraka hai wa Ukoloni Mamboleo, ambao wansubiri kwa hamu kutumia mwanya unaojitokeza kupenyeza Ajenda zao.

Kwa sasa bunge linaweza kujikita kuboresha kanuni za Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi.

Naungana na Mzee Mapesa, Kwani
Sioni sababu ya kuharakisha mambo muhimu ya Taifa kwasababu ya Majabali wawili wa CHADEMA. Ikiwa ni pamoja na CCM? mapendekezo ya Mzee Mapesa yazingatiwe.

TL, Mbowe, Ndio tunawaonea huruma ya mateso mliyopata, lakini kwa sasa kuna mamluki na vibaraka wa mabeberu wanaotaka kutumia mwanya huu kuweza kuingiza ajenda zao, je mnataka kwenda na historia kama wawezeshaji? Sidhani.

Upo uwezekano wa vishinikizo.?..sawa, tunaheshimu Demokrasia? basi, tuanze kwenye vyama vya Siasa vyote nchini....kabla hatujaenda na hayo Kitaifa. Wakati huo tukiwa tunalinda a "Sovereign State"

Tutafika,
Kitaeleweka

.
Kila mjadala wa katiba ukifika mnaanza kutisha watu mara mabeberu, mara ushoga utaingizwa kwenye katiba mara muungano utavunjwa!! Why? Mbona mara ya mwisho mlifuta maoni yote ya Warioba mkaweka yenu? Kwani mtashindwa kufuta hizo "ajenda" za mabeberu?

Mnapoingia mikataba ya kifisadi na mabeberu mnatumia katiba Gani? Ila ikitakiwa kubadilishwa mnakua wakali!!
 
15 January 2023
Makambako, Iringa


UJENZI WA OFISI YA KUBWA YA CHAMA CHA CHADEMA JIMBO LA MAKAMBAKO UNAENDELEA KWA KASI



Mikutano ya hadhara itakuwa katika eneo hili na ujenzi unaenda kwa kasi kukaribisha na kupokea ugeni wa kitaifa toka makao makuu ya CHADEMA.

Wanachama jimbo la Makambako wamesema wanajitolea kwa moyo mmoja huku wakiwa na furaha kwa kutembea vifua mbele kukijenga chama kwa ajili ya kizazi cha sasa na kizazi kinachokuja ...

Safi sana, Chadema ipo very organized nafurahi kuona ofisi zinajengwa karibu Kila wilaya nchini. Tukimalize tujenge na makao makuu mapya tuweke heshima kwa Hawa CCM!!!
 
CHADEMA KILOMBERO WAZIDI KUIMARISHA CHAMA



Vifaa vya kusaidia kasi ya kukiendeleza chama kama vifaa vya uenezi ku print kadi za kidijitali, katiba za chama, machapisho ya chama na sasa bendera 100 kwa viongozi wa jimbo la CHADEMA Kilombero mkoa wa Morogoro nchini Tanzania.

Baada ya hapo shamrashara za nyimbo za asili ya wanaCHADEMA wa Kilombero zilifuata baada ya shughuli hiyo muhimi kukamilishwa ya kuimarisha chama .
 
7 February 2023
Mbalizi, Mbeya Mjini

CHADEMA NA CCM WAKUTANA KATIKA SHUGHULI YA KIJAMII KATA YA NSALALA MBEYA VIJIJINI



Viongozi mbalimbali wa chama cha Mapinduzi CCM na chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mbeya, wapimana nguvu kwenye msiba wa Mzee Raphael Sanga wakati wakitoa heshima za mwisho, Mzee Raphael ambaye alifariki usiku wa kuamkia February 05,2023 na kuagwa February 06,2023 nyumbani kwake Mapelele kata ya Nsalala jimbo la Mbeya vijijini
 
VIKUNDI VYA KUHAMASHISHA UHAI WA CHAMA CHA CHADEMA NA NYIMBO ZA KUHAKIKISHA CHAMA HAKIPOI, KINASHIRIKI SIASA BILA KUISHIWA PUMZI YA KISIASA

 
09 December 2019

FREEMAN MBOWE AKIMSHAURI MWENYEKITI WA CCM KUHUSU MARIDHIANO, SIKU YA MAADHIMISHO YA KUSHEHEREKEA UHURU WA TANGANYIKA



Freeman Mbowe akimueleza Rais John Pombe Magufuli kuwa anayo dhamana ya kuhakikisha sio tu demokrasia inalindwa na kukuzwa, bali pia uwepo wa haki na usawa kwa wote bila kujali tofauti zao.

“Nimeshiriki maadhimisho haya ya tarehe 9 Disemba mwaka huu 2019 jijini Mwanza kuthibitisha misingi ya umoja, mshikamano na undugu miongoni mwa Watanzania.

Nakuomba mheshimiwa Rais kutumia nafasi na dhamana yako kulinda demokrasia. Kusiwe na wanaofurahi huku wengine wakilalamika,” amesema mwenyekiti wa CHADEMA taifa Mh. Freeman Mbowe.
 
Back
Top Bottom