amba.nkya
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 446
- 131
Katika hali isiyo ya kawaida mpinzani mkongwe, John Momose Cheyo ametamka rasmi kuwa rais JK ametimiza ahadi zake kwa wapiga kura na anawaonea huruma watakaojitokeza kuwania kinyang'ilo cha urais, 2010. Hii anamaanisha kuwa maisha bora kwa watanzania wote yamepatikana. Binafsi sikubaliani na kauli za Cheyo maana bado ahadi za JK kwa wananchi wake hazijatekelezwa kama alivyoahidi. Naawachia wana JF hapa jamvini kwa hoja zenu makini....mnasemaje?