PSPA Pure'12 udsm
JF-Expert Member
- Jan 11, 2013
- 834
- 450
Ndugu Wana-bodi
Nawasalim sana!
Kutokana na hali ya ajira nchini kuwa mbaya kiasi cha kutisha, huku serikali kama mwajiri mkuu na chombo pekee nchini cha kuzalisha fursa za ajira nchini kutokua na chembe ya dalili za kufanya jitihada za makusudi za kupunguza kama sio kumaliza kabisa janga hili, binafsi nimepata wazo la kujikusanya wahanga wa janga hili, yaani wahitimu wa vyuo vikuu,diploma,cheti ufundi na mafunzo mbalimbali wasiokua na ajira na kufanya yafuatayo;
1. Kuunganisha nguvu za pamoja na kuwa na sauti moja yenye nguvu na kuunda umoja wetu (Association). Hii itaakisi majitaji ya wahanga wa ajira popote Tanzania walipo kwa nia ya ku-pressurise serikali ifanye juhudi za kupunguza janga hili.
2. Kufanya Press Conference ya vyombo mbalimbali vya habari. Wote tunajua kwamba hiki ni kipindi cha bunge la bajeti. Press conference yetu ipaze sauti kwa serikali kuhusu tatizo la ajira, hivyo bajeti ilenge zaidi namna ya kutatua kero hii kwani na sisi tuna haki ya kulitumikia taifa hili kupitia fursa za ajira zinazoendana na ujuzi wetu.
3. Tunatambua kwamba mwaka huu 2014 na 2015 kutafanyika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Tuwaambie kabisa, kama hali itaendelea kuwa hivi hivi, wategee ushiriki wetu utakua wa kutosha sana unaolenga zaidi kuwaelimisha wananchi kuhusu utendaji mzuri wa serikali yao sikivu. Hivyo cha kinachoongoza serikali kisijisumbue hata kupiga kampeni maana kitakuwa kimepita bila kupingwa.
NB: Naomba hoja za maboresho na mapendekezo.
0718-257680
UPDATES
....................................
Kuhusu kujiunga.
1. Nimetoa namba ya simu hapo, naomba walio tayari tupange kukutana tarehe 18/5 2015 Napendekeza iwe pale mabibo hostel .
2. Nasikia kundi kikundi chenye mrengo na welekeo kama huu,nomba nao wanitafute kupitia namba hapo juu. Tutaungana nao ili kuwa na sauti ya pamoja.
3. Nitoe wito kwa wadau wote wahanga na wale waliopo makazini na media pia kutuunga mkono katika kufikisha sauti zetu kwa serikali. Mwalimu Nyrerere ashawahi kusema "No one is free if others are oppressed".
Nawasalim sana!
Kutokana na hali ya ajira nchini kuwa mbaya kiasi cha kutisha, huku serikali kama mwajiri mkuu na chombo pekee nchini cha kuzalisha fursa za ajira nchini kutokua na chembe ya dalili za kufanya jitihada za makusudi za kupunguza kama sio kumaliza kabisa janga hili, binafsi nimepata wazo la kujikusanya wahanga wa janga hili, yaani wahitimu wa vyuo vikuu,diploma,cheti ufundi na mafunzo mbalimbali wasiokua na ajira na kufanya yafuatayo;
1. Kuunganisha nguvu za pamoja na kuwa na sauti moja yenye nguvu na kuunda umoja wetu (Association). Hii itaakisi majitaji ya wahanga wa ajira popote Tanzania walipo kwa nia ya ku-pressurise serikali ifanye juhudi za kupunguza janga hili.
2. Kufanya Press Conference ya vyombo mbalimbali vya habari. Wote tunajua kwamba hiki ni kipindi cha bunge la bajeti. Press conference yetu ipaze sauti kwa serikali kuhusu tatizo la ajira, hivyo bajeti ilenge zaidi namna ya kutatua kero hii kwani na sisi tuna haki ya kulitumikia taifa hili kupitia fursa za ajira zinazoendana na ujuzi wetu.
3. Tunatambua kwamba mwaka huu 2014 na 2015 kutafanyika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Tuwaambie kabisa, kama hali itaendelea kuwa hivi hivi, wategee ushiriki wetu utakua wa kutosha sana unaolenga zaidi kuwaelimisha wananchi kuhusu utendaji mzuri wa serikali yao sikivu. Hivyo cha kinachoongoza serikali kisijisumbue hata kupiga kampeni maana kitakuwa kimepita bila kupingwa.
NB: Naomba hoja za maboresho na mapendekezo.
0718-257680
UPDATES
....................................
Kuhusu kujiunga.
1. Nimetoa namba ya simu hapo, naomba walio tayari tupange kukutana tarehe 18/5 2015 Napendekeza iwe pale mabibo hostel .
2. Nasikia kundi kikundi chenye mrengo na welekeo kama huu,nomba nao wanitafute kupitia namba hapo juu. Tutaungana nao ili kuwa na sauti ya pamoja.
3. Nitoe wito kwa wadau wote wahanga na wale waliopo makazini na media pia kutuunga mkono katika kufikisha sauti zetu kwa serikali. Mwalimu Nyrerere ashawahi kusema "No one is free if others are oppressed".