Joah makini vs Fid.Q

Fid is a real MC

Jamaa anaongea vitu vya msingi na sio mpenda misifa, the dude is humble and down to earth.


Huyo mwingine bishoo, copying Jigga kila kitu hata kutembea kwenye stage, the dude is not real, na kitu nyingine ni kuwa kwenye nyimbo zake anasifia na ku glorify bangi na cocain.........he's fukcin gabbage to me.
 
Fid is a real MC.

Huyo mwingine bishoo, copying Jigga kila kitu hata kutembea kwenye stage, the dude is not real, na kitu nyingine ni kuwa kwenye nyimbo zake anasifia na ku glorify bangi na cocain.........he's fukcin gabbage to me.

True dat. Kajamaa is jigga wannabe!

Ngosha anajitaidi.
 
Ngosha yupo juu sana. Sikiliza album zake, Vina Mwanzo, Kati na Mwisho & Propaganda - ametema sense ya kutosha. Jana kadrop single mpya na video yake, Ielewe Mitaa, album mpya yaja, KitaaOlojia.

Nikumbushe album ya Joh Makini inaitwaje? Nigga he is so lame, trynna copy Jay Z all the way, take a seat son ~> __/
 
Wanalilia jina mfalme na wote wako chini ya mfalme...nway,wote wakali ingawa pia wote wameishiwa mistari ya msingi.
Fid anaweza kuonekana mkali kwa mtu asiye msomaji wa vitabu kwa sababu mistari yake mingi ni repetition ya misemo,semi na methali zilizo kwenye vitabu,anachofanya ni kuunganisha,kwa upande mwingine Joh nae amezidisha kuiga hasa kwenye nyimbo zake za hivi karibuni.Hata hivyo kwenye content na delivery,Joh tops.
If am forced to chøose I won't hesitate to go for the old Joh Makini yule wa lines kali kama kwenye Hao,Mfalme na Stimu zimelipiwa.
 
fid q ni noma. hata akiwa jukwaani anatisha. mistali ya fid ni mizito kulinganisha na mistali ya joh. fid anazungumzia jamii lakini joh mistali yake ni ya kujisifia mwenyewe, mfano anajiita yeye ni mwamba wa kaskazini wakati kaskazini kuna miamba kibao kama JCB. fid ana pumzi kuzidi joh. show za joh akiwa jukwaani unaskia "twende..twende..twendee..siwaskii..dj zima mziki" hapo pumzi zinakuwa zimemuishia. lakini fid anakamua mwanzo mwisho kwa beat tu.safi sana fid. Mia
 
Mwisho wa wote ni Roma mkatoliki anawachana watu wote bila kujali chocho
 
Fid Mkali sana ukisikiliza ngoma ya Proffessional + video yake utakubali yule jamaa anajua,massive hits!!Ngosha...
 
fid q ni noma. hata akiwa jukwaani anatisha. mistali ya fid ni mizito kulinganisha na mistali ya joh. fid anazungumzia jamii lakini joh mistali yake ni ya kujisifia mwenyewe, mfano anajiita yeye ni mwamba wa kaskazini wakati kaskazini kuna miamba kibao kama JCB. fid ana pumzi kuzidi joh. show za joh akiwa jukwaani unaskia "twende..twende..twendee..siwaskii..dj zima mziki" hapo pumzi zinakuwa zimemuishia. lakini fid anakamua mwanzo mwisho kwa beat tu.safi sana fid. Mia

ulitaka amsifie jcb au kina knucle 2 knucle? Kila ,msanii ana fleva yake
 
Hao mabwana wote ni "wakali", na kwasasa ni kama mafahali wawili wasiopikika, kila mtu anakitaka "kiti". Tatizo lao kubwa wote wanaimba kitu wasichokiamini, matokeo yake ni hawana hadhi sana mbele ya wafuatiliaji wa "real hiphop" Kwanza wote wanalegeza sana, hawakazi kama ilipokuwa pale mwanzo mfano, msikilize Fid Q wa kipindi kile yupo na "heartfull Dodgerz" ie (wakina mapacha, Big 4 the geez, spado J, J murder na Sqeezer) huwezi kumlinganisha na Fid wa saiv. Joh makini wa saiv huwezi kumlinganisha na Joh makini wakipindi kile cha "hawapendi", "hao" kipindi hicho anatolewa na Prof Ludigo. Kuthibitisha hilo, Fid Q alimkana mwanae wa toka enzi za utoto "Kiraka Rado".... hili lilinithibitishia u-blazameni wa Fid kwa kiasi kikubwa sana, Kwenye Track ya "hao" Joh Makini aliziponda sana Tuzo za kill, na baadae alikataa hata kushirikishwa kwenye hizo tuzo ila baadae kuthibitisha kuwa alikuwa hajui anachopigania na wala alikuwa hajui anapigana na nani akageuka kuwa mpiga debe wa hizo tuzo tena hadi kushiriki kwenye ule wimbo mbovu wa "kill all star 2010". Hoja kuu ya utetezi marazote imekuwa eti wasanii wetu ni njaa, hiyo kweli! Lakini huwezi kujiita mwanaharakati wakati hujazijua changamoto za hizo harakati zako, kwahyo hapo ni bora anyejitambulisha kama yeye ni **** toka mwanzo na akabaki na ufala wake hivyohivyo, kuliko hawa wanafiki. Wote (Fid na Joh) wanataka tuwatambue kama ma-legend wa hiphop ya bongo, wakati hawana mpango unaofahamika wa kuacha legacy yoyote. Wameingia kwenye game wamakuta "hiphop haiuzi" ndio msemo unaokandamiza kazi zao, na wao wamejiunga kwenye huo wimbo eti kwa kususia kutoa album au kuzisambaza wao wenyewe kitu ambacho hakijaonyesha ukombozi kwa wadogo zao, sawa basi wao wameshindwa kuanzisha harakati hizo za kimapinduzi ya soko lakini je wametoa support gani kwa wanaofanya hizo harakati mfano wa Sugu (au hata Kala Pina aliwahi kujaribu), si Joh wa Fid waliowahi kuunga mkono hizo harakati za hao watu kwa wazi wazi, wanogopa watabaniwa na watakula wapi..... ndio jibu! Basi hamna mkali hapo ni waganga njaa tu kama "bongofleva" wengine. Ok msije mkaniambia natoka nje ya mada, lakini ni bora tufafanue vitu kwa undani japo kidogo katika kuonye kitu bora zaidi kuliko kushabikia kishabiki kila kitu unacholetewa. Kwa kurudi kwenye swali, umezungumzia ukali katika maeneo ya "style", "lyrics" na "ryhmes". Kwa sababu hawa ni watu ambao wametokea kwenye upenzi wa ndani sana wa hiphop, hivyo vitu wote wanavyo japo Fid ana-added advantage sababu ni anasoma sana vitabu hivyo mara zote anaonekana kumzidi Joh. Papo hapo Joh anakitu "elimu ya mtaa" ambayo ni kitu muhimu sana kwenye hiphop, ndio maana mistari ya Joh inagusa sana watu wa mtaa, pia binafsi Joh amekuwa ananikuna sana coz marazingine amekuwa sio muoga kuuchana mfumo husika anaoona haujakaa poa ie "wasomi bado watumwa kwa wanasiasa....."track ya karibu tena kwenye show za joh". Lakini ili kuutendea haki huu mjadala nadhani tungeangalia pia wanavyomeet "5 mic" kama element kuu za hiphop, wote wanapwaya sababu kuna makosa mengi yanatokana na mfumo wetu wa kimuziki, hivyo nyimbo zao zinakosa element za "dj", "graffit" na "black dancing" Mwisho nimalizie tu kuwa hawa majaa kwangu hamna mkali ni wa kawaida sana ukiingia kwenye content ya track zao, wanaimba vitu vyepesi sana, nadhani nimeathirika na kusikiliza watu kama wakina; "Hashimu Dodo (Bongo psychological)", "Salu-T", "Kwanza unit (Zavara na wenzake)", "Magazijuto", "Himamu Abas (underground souls)" "Kurasa", "A-bass", "Solo thang"...... hii kwa bongo tu, sasa ukisikiliza watu wa mtoni kama "Gangstarr (Guru), Rakim, Jeru, Nas, Rza na Gza, Pharaoh, Roots, Blackstar, Canbus nk nk nk..." kwa sasa kuna vijana wanatoka kwa "Duke", One, Stereo, Mpita, Nick Mbishi. Mtaa bado una azina kubwa sana, wanaosema hiphop ime/inakufa inabidi wajikaze sana!
 
Back
Top Bottom