JK; Viongozi wala rushwa kuiangusha CCM uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na 2015!!

Mimi nimezipenda sana nukuu hizi kama nilivyozisoma kwenye gazeti la mwananchi."Kama hatutabadilika katika suala la rushwa mwaka 2015 tutakuwa na wakati mgumu sana na kama mwaka huo tutafanikiwa kuishika Serikali, basi mwaka 2020 hatutarudi tena madarakani. "Najua rushwa ipo na mnaendelea kupokea shilingi laki mbili za airtime (muda wa mawasiliano), ndugu zangu hatutafika ama wengine watavuka na wengine kukwama," , "Viongozi wa chama ndio mmekuwa mawakala wa kusambaza rushwa bila hata aibu. Nawaombeni tubadilike, kama tutaendelea hivi hali yetu itakuwa ngumu sana katika chaguzi mbalimbali, nawaambieni," "Tuna vijana wengi kutoka katika vyuo mbalimbali ambao wanaweza kufanya kazi kwa uadilifu wa hali ya juu, hivyo hatuna budi kuachana na hawa wala rushwa ambao watatupotezea sifa yetu kwa wananchi"
"Tukipoteza urais ndiyo tumekwisha na chama kinaweza kufa.","Wenzenu wakiendelea kutembelea wanachama na kuitisha mikutano, nyie mnabakia kuimba wembe ni uleule ushindi, shauri yenu mtakatwa,"


 
Li waziri lake la nishati halijui hilo,pinda juzi ameongeza tena mikataba mingine na wachina sijui ni ya miaka mingapi.
 
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania mh Jakaya Mrisho Kikwete,amekiri kuwa viongozi wala rushwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ndio watakao isababishia anguko ktk uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015!!

Alihoji na kuuliza kuwa viongozi wanaotoa mikataba ya miaka 200 kwa makampuni huwa kweli wana akili timamu?

Chanzo; Radio free Afrika tuzungumze magazeti!!


Hao mafisadi yeye ndiye kawalea,na anaendelea kuwakumbatia hadi sasa,huyu si mwenyekiti wa ccm,ni Majanga alipaswa kuwa amewawajibisha hao wala rushwa na mafisadi.
 
Sasa watu wanaakili(wameshaamka) nimeipenda hii kumbe awamu zilizopita waliongoza majuha ndio maana rais jirani aliwahi kumwambia nyerere anaongoza maiti
 
“Wapo watu ambao wanadai kuwa chama kitafia mikononi mwangu, nataka niseme kuwa hakifii mikononi mwangu, kitafia mikononi mwenu,” alisisitiza
Kama makampuni yanapewa mikataba ya miaka 200 na viongozi walio katika serikali yako bila we kujua!!!!!!!!!
Hivi hawa wasaidizi wako watakupotosha mpaka lini?,maana hata issue ya Katiba walikudanganya.........PULL THEM OUT,vinginevyo historia itakuhukumu Mzee.
 
hakika nawaambieni IPO siku ccm watamkimbuka sana kikwete na kauli same.anawaonya sana lakini hawasikii.tusimlaumu sana kikwete maana mfumo unamfunga ktk maamuzi.bt IPO siku watajua aliyokua anamaanisha
 
kweli JK katabiri anguko la ccm, ukoo wa panya na rafiki wa ibilisi kwa heri, Karibu CDM 2015

JK hana Uhakika kama watarudi madarakani 2015, huyu Mtoto wa Mwandosya anapata wapi kiburi cha kudai ni Lazima washinde 2015! Ajue kwamba Watz wa sasa wameamka, kuiba kura haitakuwa rahisi kama anavyodhani.
 
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania mh Jakaya Mrisho Kikwete,amekiri kuwa viongozi wala rushwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ndio watakao isababishia anguko ktk uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015!!

Alihoji na kuuliza kuwa viongozi wanaotoa mikataba ya miaka 200 kwa makampuni huwa kweli wana akili timamu?

Chanzo; Radio free Afrika tuzungumze magazeti!!

JK wakati unautafuta urais vijana wengi sana tulikusapoti bila kujal itikadi za vyama vyetu, tulikuwa, na kwa kweli ulionesha, matumaini makubwa sana kwa kizazi cha sasa. yan sijui hata nini kilikubadilisha mzee wangu!! sijui ndo huko kutekwa na mafisadi kwa kukuingiza kwenye mikataba mbalilmbal ya kifisadi au vip hata silewi ila kiukweli umetuangusha sana. muda wako umekatika na yale matumaini yote tuliyowekeza kwako hakuna chochote kilichotokea, si kwenye uchumi na wala si kwenye fituboli...kwa mda uliobaki ungetuwekea basi walau hata miundombinu ya kutupeleka walau kOMBE LA MATAIFA YA aFRIKA miaka kumi ijayo BASI MKUBWA! na miundimbinu nina maana kweli ya miundombinu na si kutuletea maximo sehemu isiyokuwa na mfumo.
 
Mi nafikiri ni hali mbaya ya watanzania kimaadili tulivyoporomoka tunajali mambo yetu binafsi kuliko ya jamii na hii hata kiingie chama kingine cha siasa kama watanzania wenyewe hatubadiliki basi tutaishia hivihivi kulaumu mawaziri,wabunge au watumishi wa serikali kwa ujumla...
 
SWALI
Kwa nn mh.Kikwete anafikiri kuwa CCM ikikosa urais inaweza kufa?
Urais unakiwezesha vp ccm kuendelea kuwepo?
 
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania mh Jakaya Mrisho Kikwete,amekiri kuwa viongozi wala rushwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ndio watakao isababishia anguko ktk uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015!!

Alihoji na kuuliza kuwa viongozi wanaotoa mikataba ya miaka 200 kwa makampuni huwa kweli wana akili timamu?

Chanzo; Radio free Afrika tuzungumze magazeti!!
Huu ni ukweli mchungu sana kwa wanaCCM, ambao hakujawahi kutokea Kiongozi yeyote wa chama hicho, aliyewahi kuthubutu kutamka hadharani, kama alivyotamka yeye hadharani.

Ni dhahiri basi watu wa TISS tayari weshampa taarifa za kiintelejensia kuwa uwezekano wa CCM kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ni finyu kama vile NGAMIA KUPENYA KWENYE TUNDU LA SINDANO!!

Inabidi watanzania wote kwa ujumla wetu tumpongeze JK kwa ujasiri wake na kuthubutu kutoa tamko ambalo tokea nchi yetu iingie kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, hakujawahi kutokea kiongozi yeyote wa chama hicho, aliyewahi kutamka hadharani kuwa upo uwezekano wa CCM kushindwa na vyama vya upinzani, katika uchaguzi wowote, na badala yake tumezizoea kauli za mara kwa mara za viongozi wakubwa wa CCM, wakitamka kuwa CCM itaendelea kutawala, hata kwa miaka mingine 200 ijayo!!

Nadhani JK baada ya kupata uhakikisho huo kutoka kwenye taasisi yake muhimu ya TISS, anachojaribu kufanya kwa sasa ni kuwaandaa kisaikolojia viongozi wenzake, wayakubali matokeo yoyote yatakayotokea, badala ya kuamua kuwa ving'ang'anizi wa kutokubali kushindwa, na hivyo kuliepusha kuliingiza Taifa kwemye umwajikaji wa damu.

Pia nadhani lengo la JK, ni kuacha Legacy, ambayo siyo tu itamwachia heshima kubwa kwa Umma wa watanzania, bali anajiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa tozo la MO Ibrahim ya donge nono la dola za kimarekani milioni 5, tuzo ambayo hutolewa kwa kiongozi aliyeondoka vyema madarakani, tuzambayo imeshindwa kupata mshindi kwa kipindi cha miaka minne mfululizo!!
 
Back
Top Bottom