sijui nini
JF-Expert Member
- Sep 29, 2010
- 2,553
- 1,285
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete, amesema serikali haina uwezo wa kutoa huduma za jamii bure na amewashangaa wanasiasa wanaopita wakiwadanganya wananchi kuwa iwapo wakichaguliwa watatoa huduma hizo bure.
Aliyasema hayo jana katika kata ya Mchanngimbore jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma katika siku yake ya pili ya kampeni katika mkoa huo.
Kikwete alisema serikali ilishajaribu sera hiyo ya huduma bure lakini ilishindwa kwani bidhaa ziliadimika na huduma nyingi zilishindwa kutolewa.
Alisema licha ya maendeleo yaliyofikiwa tangu Uhuru, Tanzania bado ni nchi maskini na haiwezi kutoa huduma bure kama baadhi ya watu wanavyowaahidi wananchi katika kampeni zao.
Alisema CCM inaahidi mambo yanayotekelezeka na kwamba imejitahidi kuhakikisha yale yote yaliyoahidiwa mwaka 2005 katika Ilani yake yametimizwa.
Alisema serikali iliahidi kujenga shule za sekondari kila kata na imefanikiwa kufanya hivyo na sasa kila kata ina shule mbili za sekondari, jambo ambalo awali lilionekana kama haliwezekani.
Alisema serikali imejitahidi kwa kiwango kikubwa kuboresha elimu ya msingi na sekondari na hivi sasa wanafunzi wengi wanapata nafasi ya kwenda shule tofauti na ilivyokuwa mwaka 2005.
CHANZO.
Haya sasa...
Aliyasema hayo jana katika kata ya Mchanngimbore jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma katika siku yake ya pili ya kampeni katika mkoa huo.
Kikwete alisema serikali ilishajaribu sera hiyo ya huduma bure lakini ilishindwa kwani bidhaa ziliadimika na huduma nyingi zilishindwa kutolewa.
Alisema licha ya maendeleo yaliyofikiwa tangu Uhuru, Tanzania bado ni nchi maskini na haiwezi kutoa huduma bure kama baadhi ya watu wanavyowaahidi wananchi katika kampeni zao.
Alisema CCM inaahidi mambo yanayotekelezeka na kwamba imejitahidi kuhakikisha yale yote yaliyoahidiwa mwaka 2005 katika Ilani yake yametimizwa.
Alisema serikali iliahidi kujenga shule za sekondari kila kata na imefanikiwa kufanya hivyo na sasa kila kata ina shule mbili za sekondari, jambo ambalo awali lilionekana kama haliwezekani.
Alisema serikali imejitahidi kwa kiwango kikubwa kuboresha elimu ya msingi na sekondari na hivi sasa wanafunzi wengi wanapata nafasi ya kwenda shule tofauti na ilivyokuwa mwaka 2005.
CHANZO.
Haya sasa...