JK na Mangula/Mpasuko Mkubwa CCM NEC

JK na Mangula/Mpasuko Mkubwa CCM NEC

Nape nadhani atahamia CDM punde lowassa akitawazwa kuanza kampeni!!
CDM walisema hana number, na kw aujinga kanyea kambi.Kama bado ni mamluki wa CDM basi atakuwa proof nzuri kuwa CCM ni very Vulnerable.Kama hadi Speaker wa Bunge 6 alikuwa na kadi ya CCM ,ni mbunge na speaker wa CCM, ni candidate wa urais wa CCM yet alitumikishwa na CDM .Siwezi ishangaa CCM ,kama jimama lenye kila aina ya hela jeuri, nguvu mbele ya wanaume.Halafu linachapwa makofi na kimwana mdogo kadiri apendavyo, huku linabaki lia kuwa haliachiki ng`o.
 
Kwa mujibu wa kada wa CCM ambaye ni mjumbe wa NEC ambaye amavujisha siri hii, inasemekana kuwa Mh Mangula alipotoa kauli ya kukataza wanaccm kujinadi kabla ya kipindi cha uchaguzi alisababisha Mh.Lowasa na wengine wengi wenye uchu na madaraka 2015 kuchukizwa na kauli hiyo na kuamua kufanya kila namna kahakikisha Mangula anadhibitiwa vema ama anafanyiwa kila namna hadi ajiunge na kambi ya Lowassa ili apunguze msuli dhidi ya harakati za mbunge huyu wa monduli.

Kwa mujibu wa kikao cha JK na wabunge kilichofanyika dodoma hivi majuzi, JK amedhihirisha kwenda kinyume na msimamo wa Mangula kwa kutoa amri kuwa wanaccm wanaotaka kuwania nafasi za urais na ubunge kupitia ccm ni ruksa kuanza kujipitisha kwa wapiga kura.
Kauli hii tata ya Mwenyekiti wa ccm mrisho jakaya kikwete imeshangaza wengi hasa baada ya kudhihirisha kuwa ni kauli inayopingana na maazimio ya awali yaliyopitishwa na kikao cha Nec yaliyotangazwa na Mangula ambaye ni m-nec wa ccm.

Viunga vya ccm vya ndani kabisa vinapasha kuwa baada ya JK kuonyesha wazi kuwa anasupport harakati za kujinadi zinazofanywa na Lowasa pamoja na wanasiasa wengi wa ccm kumesababisha mpasuko wa hatari ndani ya ccm ambapo mwisho wa siku tutajionea jinsi Mh. Mangula pia anajisalimisha kwa Lowassa mithili ya mbwa koko aliyekutana na chatu na wengine watasambaratika kila mmoja kivake bila kujitambua.

Huu unaitwa ni mpasuko ndani ya ccm kwasababu makada maarufu wameshaanza kutupiana maneno makali hasa baada ya wengine kugundua kuwa wanatumiwa vibaya na JK mithili ya mbuzi wa kafara.
Nape Nnauye ni Kada mashuhuri wa ccm ambaye ameonekana dhahiri kutetereka na mwenye hofu kubwa hasa baada ya kumuona JK akimsifia Lowasa hadharani na akimpa ruhusa ya kujinadi kwa wapiga kura kwa ajili ya urais 2015.

Wachambuzi wa maswala ya siasa wanakiri kuwa JK ameanza kudhihirisha kuwa anamsanifu Membe na na nia yake kuu ni kumrithisha Lowasa kiti cha kugombea urais 2015 kupitia CCM.

Makambi yote ya ccm yaliyokua yakiwania nafasi ya uwakilishi wa rais yameanza kuyumba gafla baada ya kutatanishwa na msimamo wa nwenyekiti wa CCM Mh.Mrisho Jakaya Kikwete juu ya nafasi ya urais 2015,

' wengi walidhani kuwa JK amemsaliti Lowasa na kuunga mkono kambi ya Membe kumbe la hasha bado JK anamuandalia makao Lowassa'. Hayo ni maneno ya kiongozi wa Nec aliyekuwa akichekelea mtafaruku huu mkubwa unaodhihirisha kuwa JK kama mwenyekiti wa ccm amepanic kutokana na speed ya CHADEMA hadi amejikuta akitoa maagizo yanayopishana wazi kabisa na maazimio ya NEC ya ccm yaliwekwa hadharani hapo awali na Mangula.

My take.
Wale makada waccm wanautumika kama big.G huu ndo muda wao maalum wa kutemwa rasmi na JK pamoja na viongozi wengine wa ccm wenye uchu wa madaraka.

Sakata hili pia linadhihirisha kuwa JK amewaingiza mkenge puppets wengi sana wa ccm.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
mkuu huoni hata aibu swala hili nape kaliongelea sana mpaka kwenye vyombo vya habari kweli wewe upo nyuma katika kutafuta habari.
 
CDM (The badger) haoni hata haja ya kujali nani anachaguliwa ktk hii kambi dhaifu na tamu kutafuna.Kwani siku anataka lunch hahitaji kujua kama ni black mamba, green mamba, cobra, au nani, yeye atavuta kunzi apopote kama anayevuta spagheti vile..Si Lowassa huyu huyu alikwend ameru kwa mbwembwe kuwa yeye ni wa vitendo.Baada ya kuwagaragaza CCM ktk uteuzi wa Sioyi. Alichoambulia ni kuingia kimaficho ktk chumba cha kuhesabu kura ili akabadili matokeo, magari yalipasuliwa na mwisho sioi akakubali matokeo.SIjui kama hiyo habari hata kama iliwahi somwa tena.CCM hata revision hawataki sikia.

Ukiacha Mdhaliliko alioupata kwenye RICHIMOND , Kusema ule ukweli mahali pengine alipodhalilika Lowasa ni Arumeru , usifanye Mchezo na CDM aisee , hao jamaa hawajali Mvi za Mtu ! Ukiwakalia kwenye 18 lazima wakubutue !
 
Hivi Kamanda James Ole Milya (cjui nimepatia hili jina lake!!) bado ana access na info za ndani ya CCM?!
 
Ha! ha! ha! ha!ha1 ha! ha! ha! one sana, kama vipi mjipange na propagnga zenu. CCM ni chama dume haipasuki
Unjaua, you know, nyinyi watu mburula sana !

Kama vipi jipangeni mrudi na santuri nyingine
sauti ya Umeme NY
 
Last edited by a moderator:
Ukiacha Mdhaliliko alioupata kwenye RICHIMOND , Kusema ule ukweli mahali pengine alipodhalilika Lowasa ni Arumeru , usifanye Mchezo na CDM aisee , hao jamaa hawajali Mvi za Mtu ! Ukiwakalia kwenye 18 lazima wakubutue !

Haha sijui atakuwa wapi kusililizia kura za urais?Kama magamba watampitisha.Monduli hakuna kura nyingi na akiondoa nyumba inaungua.Atakuwa jiko kuu?CDM watakuwa na bigi screen inayotangaza kura toka vituoni.Kwa kila mkoa.Akija lazimisha matokeo ya mwisho.Atawajua watu wa mbeya, arusha mwanza, wataenda dar kwa miguu.

Arusha mjini Vijana wanamtafuta sana wamdake na kumaliza game ktk eneo la kuhesabu kura.Arumeru walikosa gari yake wakaharibu ingine.NIlikuwa AR ktk uchaguzi Lemo aliopiga bao.VIjana walisema ndiye aliyeshikilia matokeo masaa kadhaa, na walikuwa wanamsubiri wamalizie game.Walikuwa wakiapa mchana kuwa ipo siku ataangamia ktk eneo la matokeo.

Huwa wanatrack sana farsi mweupe anavyojichomoza kulazimisha ushindi.
 
Mgawanyiko bado, mgawanyiko utaonekana dhahiri kwenye bunge la bajeti la mwaka 2015. Mambo bado, na kutakuwa na kambi tatu tu. Na nawakumbusha tu kuwa hela zitamwagwa sana mwaka 2015, mfumuko wa bei utaongezeka, na wachache wataneemeka, lakini kumbukeni wahenga walisema, wapambanapo mafahali wawili, ziumiazo ni nyika

Usisahau mkuu, VITA YA PANZI...FURAHA KWA KUNGURU....!!!
 
Mchezo JK anaoucheza hapa ni kutaka Lowassa ABWETEKE na kuachana na plan B. Sio mwepesi kama tunavyodhania mpaka kwamba "better the devil you know"

Nyie watumnataka Kiongozi wetu akumbane na kipigo cha mama yeyoo kama kile cha mzee wauwazi na ukweli cha kutengua nyonga? Mama Mwanaasha kesha onyesha kila dalili kuwa anamuunga mkono "kaka" BM achukue mikoba na ndio maana hata katika NEC kwa kushirikiana na mtoto wa kufikia wakamuunga mkono waziwazi.
Sasa kama mkulu anaanza kuonyesha kumpaisha EL si kutatokea tafrani jumba kuu? Sitaki kumwona mzee wetu "mpendwa" naye anatembelea fimbo kama ilivyotokea wakati wa ukweli na uwazi.
Wamama wanapiga siku hizi,hamjaona mama wa Tangawizi alitaka kmshushia kipigo mnadhimu wa upinzani na kama sio yeye kukomaa na kusema "wewe, mie sio Katapila! Mie ni buldozer! Hali ingeluwa mbaya sana. Mama wa Tangawizi ni noma hata "mwanae yule Bonge mvaa macheni" kashindwa kurudi Mvumi kwa Mzee "Katapila" kwa kumuogopa mama, amebaki mjini anapiga mizinga kwa kujikombakomba. Bendera lazima apeperushe BM,chezea mama mkuu wewe!
 
Mimi si mwana ccm, nionavyo ni kuwa angalau MEMBE anaheshima kidogo mbele ya jamii ya watanzania ukilinganisha na LOWASA miongoni mwa wana ccm wanaotajwa tajwa kuwa na nia ya kutaka kupanga magogoni. Mshambulizi dhidi ya lowaza ikiwa ataomba na kupewa ridhaa na wanachama wa ccm kuiwakilisha ccm kwenye mbio za kwenda mtaa wa luthuli aka magogoni yatakuwa mazito na ya silaha za maangamizi yatakayosababisha chama kupoteana na wanachama wake.
Lowasa atashindwa kwa aibu kubwa afadhali atakavyoshindwa membe.
chezea watanzania weye!

LUGHA HII WATAIELEWA WENYE MASIKIO

Yes! Bt wenywe hawaamini
 
Ha! ha! ha! ha!ha1 ha! ha! ha! one sana, kama vipi mjipange na propagnga zenu. CCM ni chama dume haipasuki
Unjaua, you know, nyinyi watu mburula sana !

Kama vipi jipangeni mrudi na santuri nyingine
sauti ya Umeme NY

Ndo umekuja na ID mpya baada ya ban!?bonge bana
 
Last edited by a moderator:
Lowassa awe rais, FISADI, MDINI, MKABIRA, MBAGUZI, MWIZI WA PESA ZA TZ, MTAFUTA SIFA MAKANISANI, HAIWEZEKANI, kama kuna mtu mbaya ktk viongozi wangu wa ccm ni lowassa shida zote hizi bila lowassa zingetoka wapi?
 
Mgombea wa kuchongwa alikuwa anasemwa na Nape ni Lowassa au kuna mwingine?
 
Mchezo JK anaoucheza hapa ni kutaka Lowassa ABWETEKE na kuachana na plan B. Sio mwepesi kama tunavyodhania mpaka kwamba "better the devil you know"

Kama ana akili Lowassa mpaka muda huu lazima awe na plan "B" kwasababu hawa magamba wenzie lazima watamMALECELA!!!!!
 
Wanaoona mwenyekiti wa CCM amekosea kutoa ruhusa watu wajinadi hawako sawa. Kwa jinsi siasa zinavyoendelea Tanzania, ni vizuri wakajitokeza kama watu wanne wa CCM kuanza kujinadi ili kupima upepo kupitia kura za maoni na mitandao ya kijamii vinginevyo uteuzi wa dakika za mwisho bila kufanyiwa utafiti unaweza kuizika CCM kama KANU ilivyozikwa kule Kenya.
 
Lowasa ni chaguo la Mungu Acheni kupingana naye

Mlianza kusema hayo hayo kwa Rais Kikwete, na sasa mnaendeleza kwa Mh Lowasa, tafadhali msimhusishe MUNGU na mambo ya TAMAA zenu wenyewe. Bora mfanye siasa zenu bila kutaja jina lake.
 
Mbona hii itakuwa A BLESSING IN DISGUISE kama CCM watafanya hii TECHNICAL ERROR ya kumsimaisha Lowassa badala ya Membe.

Let's keep our fingers crossed JK amusimamishe Lowassa
 
Ivi ile miezi 6 ya Mangula inaisha lini?

CCM huwa hawamaanishi wanachokisema ..................... miezi 6 inaweza kuwa namaana ya miaka 6 au hata 60. Si unakumbuka kauri na Nyerere baada ya vita vya Kagera alipotutangazia miezi 18 ............... mpaka leo miaka zaidi ya 30 bado uchumi ni mbovu tu!!
 
"wengi walidhani kuwa JK amemsaliti Lowasa na kuunga mkono kambi ya Membe kumbe la hasha bado JK anamuandalia makao Lowassa'.

Bwana Kiluilui, hapa hakuna uhakika kabisa, kwa sababu Kikwete ni kati ya watu ambao hawana guts za konyesha msimamo wao mapema, subiri mwakani ndo utajua mkuu!
 
Back
Top Bottom