frozen
Senior Member
- Aug 12, 2010
- 135
- 32
Kuna maneno mengi yanayosemwa kuhusu siasa..oh siasa mchezo mchafu, oh siasa hili. Kifupi mimi nlikuwa mmoja wa watu niliye mkubali jk ktk uchaguzi wa mwaka 2005. Japokuwa sikuwa na taarifa zake nyingi katika utendaji wake kabla ya kugombea uraisi, katika kampeni zile kwa lugha yake ya upole na kwa kutotumia lugha kali na ahadi tele za kuwapa watanzania maisha bora nikamwona mtu muungwa ambaye anania ya dhati ya kuwakomboa watanzania.
Lakini baada ya kipindi chake cha miaka mitano nikapata picha halisi ya JK kama ni mtu mnafiki na anayeweza kutumia lugha yake vema na sura yake kulaghai wananchi wake, na mtu ambaye anakiburi na jeuri ya chini chini na vijembe vilivyo jificha.
Katika uchaguzi wa mwaka jana bwana huyu alitumia picha mbalili mbali kulaghai watu, kama utakumbuka kulikuwa na mabango lukuki ya kimuonesha akiwabeba watoto, akiwasaidia wakinamama kuwabebesha ndoo za maji, akisalimiana na walemavu..na picha nyingine nyingi zikimpambanua kama mtu anayejali, na kweli akapata kura kutoka kwa akina mama, walemavu na wadanganyika wengine.
Ni kweli kuna mazuri mengi umefanya lakini jk, unaiua Tanzania kmya kimya, inawezekana unajua hili au haujui,mambo ya udini yanayozungumziwa leo mwanzilishi wake ni wewe, migomo ya wanafunzi,walimu, na wafanyakazi yaliyotokea na yanayokuja mwazilishi wake ni wewe, angalia kilichotokea igunga na mabo yako ya kujivua gamba, mabilioni ya pesa yakatumika katika uchaguzi ule pasipo sababu yoyote ya msingi, na unafiki uliofanywa na viongozi kuwapata wadanganyika wawachague watu wapate ulajo..
Angalia kinachotokea arusha leo, inawezekana haujali lakini ipo siku tu hutaamini sumu hii uliyoleta itakapo kurudia. Watu wamechoka na wanahasira kwa kuwadanganya na kuwafanya kuwa watoto wadogo. Uungwana kama mambo huwezi waachie wengine, au omba msaada usaidiwe au kili kushindwa usaidiwe na sisi wananchi tutakuelewa ndugu badala ya kutupeleka kama gari bovu.
Hakika kila chenye mwanzo huwa na mwisho,yuko wapi gadaffi,mmbaraka wa misri na viongozi wengine ambao walikuwa wanajiona wao ni Mr Right? hakika Tanzania inamatatizo mengi sana kwa sasa na nchi ipo ipo tu mpaka tunapewa masharti ya ajabu ajabu tu kupewa misaada.
Hasira zote juu ya serikali yako, ni kwa sababu ulitudanganya, ulijifanya Masiha wakiti wewe hauna uwezo huo, kwa nini uliwadanganya JK?
Lakini baada ya kipindi chake cha miaka mitano nikapata picha halisi ya JK kama ni mtu mnafiki na anayeweza kutumia lugha yake vema na sura yake kulaghai wananchi wake, na mtu ambaye anakiburi na jeuri ya chini chini na vijembe vilivyo jificha.
Katika uchaguzi wa mwaka jana bwana huyu alitumia picha mbalili mbali kulaghai watu, kama utakumbuka kulikuwa na mabango lukuki ya kimuonesha akiwabeba watoto, akiwasaidia wakinamama kuwabebesha ndoo za maji, akisalimiana na walemavu..na picha nyingine nyingi zikimpambanua kama mtu anayejali, na kweli akapata kura kutoka kwa akina mama, walemavu na wadanganyika wengine.
Ni kweli kuna mazuri mengi umefanya lakini jk, unaiua Tanzania kmya kimya, inawezekana unajua hili au haujui,mambo ya udini yanayozungumziwa leo mwanzilishi wake ni wewe, migomo ya wanafunzi,walimu, na wafanyakazi yaliyotokea na yanayokuja mwazilishi wake ni wewe, angalia kilichotokea igunga na mabo yako ya kujivua gamba, mabilioni ya pesa yakatumika katika uchaguzi ule pasipo sababu yoyote ya msingi, na unafiki uliofanywa na viongozi kuwapata wadanganyika wawachague watu wapate ulajo..
Angalia kinachotokea arusha leo, inawezekana haujali lakini ipo siku tu hutaamini sumu hii uliyoleta itakapo kurudia. Watu wamechoka na wanahasira kwa kuwadanganya na kuwafanya kuwa watoto wadogo. Uungwana kama mambo huwezi waachie wengine, au omba msaada usaidiwe au kili kushindwa usaidiwe na sisi wananchi tutakuelewa ndugu badala ya kutupeleka kama gari bovu.
Hakika kila chenye mwanzo huwa na mwisho,yuko wapi gadaffi,mmbaraka wa misri na viongozi wengine ambao walikuwa wanajiona wao ni Mr Right? hakika Tanzania inamatatizo mengi sana kwa sasa na nchi ipo ipo tu mpaka tunapewa masharti ya ajabu ajabu tu kupewa misaada.
Hasira zote juu ya serikali yako, ni kwa sababu ulitudanganya, ulijifanya Masiha wakiti wewe hauna uwezo huo, kwa nini uliwadanganya JK?