bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 495
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya leo, Jumanne, Agosti 9, 2011, amempokea mgeni wake, Rais wa Jamhuri ya Somalia, Mheshimiwa Sheikh Sharif Sheikh Ahmed, ambaye amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Kikwete. Baadae jioni leo, Rais Kikwete atamfuturisha mgeni wake ikiwa ni baada ya mazungumzo rasmi. Futari ya Rais Kikwete na Sheikh Sharif pamoja na mazungumzo rasmi ya kiserikali yatafanyika Ikulu jijini Dar es salaam. Rais huyo wa Somalia ataondoka kesho jumatano kurejea kwao.
My Take: Futari ya Rais JK na Sheikh Shariff inafanyika huku Taifa likiwa katika kizungumkuti cha shida ya mafuta na huku serikali ikiwa haijatoa kauli yoyote kwa wiki zima sas!!!!!