JK Kawageuka Museveni,Kagame?

JK Kawageuka Museveni,Kagame?

WOWOWO

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2011
Posts
599
Reaction score
457
SADC yatengea waasi wa M23 Sh160 bilioni

viongoziSADC.jpg

JUMUIYA ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), imepanga kutumia dola 100 milioni za Marekani kukabiliana na kundi la waasi wa M23 Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Kiwango hicho ni sawa na Sh160 bilioni (dola moja kwa Sh1,600), kinatazamiwa kutumika kugharimia operesheni za vikosi vya kulinda amani ya jumuiya hiyo, ambavyo vinakusudiwa kutumwa eneo hilo lenye uasi.

Viongozi wa SADC waliokutana Dar es Salaam kwa kikao cha dharura kujadilia hali ya amani nchini DRC, walikubaliana kugharimia kikosi hicho na wamewaonya waasi hao kuondoka maeneo wanayokalia. Kikosi hicho kisichofungamana na upande wowote kinatazamiwa kutumwa Mashariki kwa Congo wakati wowote, baada ya kukamilika kile kilichoelezwa hatua za awali za utendaji ambazo zinaratibiwa na asasi ya ulinzi na amani (troika), ambayo inasimamiwa na Tanzania, Namibia na Afrika Kusini.

Tanzania na Afrika Kusini zimeahidi kuchangia sehemu kubwa ya gharama kufanikisha operesheni za kikosi hicho, uamuzi ambao umepongezwa na nchi wanachama wa SADC. Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa vikosi vya SADC kutumwa nchi wanachama kuzima uasi.

Akitangaza maazimio ya kikao hicho, Rais Jakaya Kikwete alisema nchi kumi eneo la Maziwa makuu zimekubaliana kuunda jeshi hilo, litakalokuwa na askari 4,000 kukabiliana na ghasia na vita ya mara kwa mara Mashariki mwa Congo.

"Kimsingi tumekubaliana kuunda jeshi na jukumu letu la kwanza litakuwa kwenda kusimamia hali ya amani huko Congo, pande zote zimekubaliana kuchangisha fedha kuliwezesha jeshi hilo kuendesha operesheni zake kwa ufanisi zaidi," alisema Rais Kikwete.

Alisema kikao cha viongozi wa SADC wamelaani vikali hujuma zinazoendelezwa na waasi wa M23, ambao hivi karibuni walifaulu kuteka mji wa Goma na maeneo mengine ya jirani.
Source:
Sadc yatengea waasi wa M23 Sh160 bilioni - Kimataifa - mwananchi.co.tz

My Take:
Ni juzi tu JK kahudhuria kikao cha Kampala akiwa na Kagame na mwenzake Yoweri Museveni na kukubaliana Joseph Kabila kuingia kwenye mazungumzo na Waasi wa M23 na baadhi ya maazimio ambayo wadadisi wengi wa mgogoro wa Goma, DRC waliyaona ya kitoto na yaliyolenga kuwabeba waasi hao wa M23 ambao kwa mujibu wa Taarifa za kichunguzi za UN wanatajwa kusaidiwa na Rwanda pia Uganda.

Wadadisi wengi walienda hatua moja mbele na kuhoji uhalali wa Museveni na Kagame ambao kimsingi ni watuhumiwa katika mgogoro huo kuwa mstari wa mbele kusaka suluhu na hata kuratibu mazungumzo kati ya Kinshasa na waasi hao.

Swali langu ni je kwa maazimio hayo ya SADC kuunda jeshi huru kukabiliana na Waasi wa M23 kinyume na makubaliano ya Kampala, JK kawageuka Museveni na Kagame? Au katika kikao hicho alikosa ujasiri wa kuwaambia hawa jamaa HAPANA lazima operesheni za waasi zikome Goma? Na nini hatma ya mahusiano kati ya Dar es Salaam, Kampala na Kigali?

NB: Naunga mkono wazo hili la SADC ingawa limekuja kwa kuchelewa. Tazameni picha hapo juu JK anaonekanaje?
 
Malawi nao watatoa wanajeshi kwenda Congo.Lazima tukubali ustawi wa Congo una faida kubwa sana kwetu kiuchumi kuliko hata Kenya.
Tumejiandaaje kufaidika kiuchumi ktk Congo itayostawi.

Bila kusita namuunga mkono Rais Kikwete kwa maamuzi haya!
 
Sikubaliani na Kagame/Museveni kumshurutisha Kabila awe na power sharing na M23. Wanaongoza through fear mongering na ukabila ... wananchi wa Congo wapewe elimu ya political process kama njia ya kupata serikali wanayoitaka.
Vita inawaathiri wanawake na watoto .... soi it's a noble thing to go and protect our neighbors and let these people know that enough is enough!
 
Ni ajabu sana Kagame na Museven wanatuhumiwa kusaidia waasi wa M23 na haohao (watuhumiwa) ndiyo wako moto kweli kutafuta suluhu DRC.Ati wanajifanya kuratibu mazungumzo kati ya Waasi na Serikali ya Kinshasa. Kweli kuna suluhu hapo? Si kutaka kumtesa na kumbana Joseph Kabila kuishia kuruhusu nchi kukaliwa na waasi hawa?

Ninachoshindwa kuelewa ni kitendo cha JK kuafikiana na akina Museveni na leo ghafla anaingia makubaliano mengine na SADC tena yenye kutengua makubailiano ya Kampala. Je JK hakuona tatizo katika maazimio ya Kampala? Alizidiwa nguvu na akina Kagame? Maswali ni mengi hapa.
 
Mambo makubwa kama haya ni vema kushirikiana ikiwezekana at least viongozi tisa,maadam wakuu hawa wamekubaliana kwa nia moja ni jambo jema ambalo lanaweza kuwa darasa kwa wenzetu wa afrika magharibi kwa mfano mgogoro wa sasa ulipo mali na baadhi ya mapinduzi ya kijeshi yasiyo na tija.
 
Za kuambiwa changanya na zako huyo ndio jk..amechukua za akina M7 akachanganya na za kwake akapata za SADC.!
 
Kumbe tz nayo inaweza toa misimamo kama USA hivi ya afrika..inafariji sana
 
Sikubaliani na Kagame/Museveni kumshurutisha Kabila awe na power sharing na M23. Wanaongoza through fear mongering na ukabila ... wananchi wa Congo wapewe elimu ya political process kama njia ya kupata serikali wanayoitaka.
Vita inawaathiri wanawake na watoto .... soi it's a noble thing to go and protect our neighbors and let these people know that enough is enough!
So far Jk amecheza kama pele!

Suala la DRC linaudhi sana, na wanaoliendekeza ni Kagame na kwa mbali Museveni.

Kwamba Tanzania has openly decided to back Kabila ni kuonyesha kwamba sasa enough is enough.
Tanzania imeahidi kupeleka jeshi la kulinda amani, lakini tunajua sote kuwa hpo Goma situation ni volatile.
Na mpaka tume jiorodhesha kushiriki kijeshi inamaana uelekeo wa diplomasia kwa Kagame na Museveni umjionyesha wazi.

Lazima tumpe tafu kijana wa Kunduchi, Kabila.

Ni wazi kuwa hao M23 ni outfit ya Kagame, bika ubishi.
Museveni amelielewa vizuri hilo somo na ndio maana aling'aka hata kwenye kikao cha SADCC, na baadaye kutokomea na kususia sherehe za Uhuru wa Tanzania za miaka 51!

Kagame na Museveni wanajua wazi kuwa world opinion is against them.
Vichwa maji Bob Mugabe wa Zimbabwe na Dos Santos wa Angola walihisiwa kukaribishwa kuwadunda hao M23, kwa hata msaada wa nchi nyingine.

Na hapo ndo hawa waHima wakatambua kuwa mambo yanaanza kuwa geuka, wakawaondoa M23 harka sana.

All this time tanzania has kept off the game, but I dont think it will be for much longer.
 
WOWOWO,
Unaposema JK kawageuka Museveni na Kagame inamaana walikuwa pamoja hapo mwanzo...JK anachofanya ni kuakikisha Congo inakuwa tayari ni mpango wa viongozi wa afrika kupambana na migogoro.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo la DRC na maamuzi ya SADC ni zaidi ya Rwanda na Uganda. UN wana kikosi cha kulinda usalama pale nafikiri kikubwa Africa kama sio duniani. UN wanatumia fedha nyingi kwa shughuli hii! Ajabu ni kuwa mambo haya yanatokea mbele ya kikosi hiki! Maamuzi ya SADC ni kuwaambia UN you have failed us...lakini wakati huo huo wanataka wapate support ya UN. Je hii itawezekana tuwe na vikosi viwili vyenye mandate ya UN - na sijui Kama mandate ya hivi vikosi zitatofautiana. Kuna suala la funding, bila support ya UN je SADC wataweza kumudu kwa muda mrefu? Tujue hii si kazi ya mwezi mmoja inaweza kuchukua miaka na ni aghali siyo kwa fedha tu Bali hata maisha ya vijana wetu.
 
acha woga. waache waende izo gharama zote zitalipwa na UN .jk sio mjinga kupeleka wanajeshi wake kongo kwa gharama za nchi. mfano Tulivyoenda Comoro mapesa tuliyolipwa mungu ndio anajua.tatizo mafisadi wengi.
mfano mwingine wanajeshi wa kenya walipoingia somalia sasa UN inawalipa gharama zote na wanapeta.hongera muhesimiwa rais.
 
REPUBLIC OF KIVU
Why not?Leo kuna Sudan Kaskazini na Sudani Kusini,Binafsi naiona Congo ni kubwa mara mbili na robo ya Ethiopia kiasi kuwa Utajili mali ya asili yake auwafaidishi wakongomani kwa kuwa augawiki ipasavyo.Nimepata kusikia ujio wa NCHI INAITWA KIVU kwa mwenendo huu naona kuna haki pia ya kuhoji umma wa kama Nchi iyo iwepo au la!!!Watanzania kwenda huko ni kwenda kutuliza kwa muda kisha baada ya miaka kadha wa kadha kinanuka upya!!!
 
WOWOWO,
Unaposema JK kawageuka Museveni na Kagame inamaana walikuwa pamoja hapo mwanzo...JK anachofanya ni kuakikisha Congo inakuwa tayari ni mpango wa viongozi wa afrika kupambana na migogoro.

Mkuu Ritz sisemi JK alikuwa pamoja na Museveni au Kagame.Read between the lines maelezo yangu. JK alishiriki kikao cha Kampala na kufikia maazimio kadhaa dhidi ya Kinshasa na waasi wa M23 lakini leo kayaweka pembeni maazimio hayo na kuja na azimio la kuunda Jeshi la kudhiti rebel militias Kivu chini ya SADC.

Nimeeleza kuunga mkono wazo hili lakini nikahoji sababu ya JK kuunga mkono maazimio ya Kampala wakati hakuyaafiki, je ilitokana na yeye kuzidiwa nguvu na akina Kagame na Museveni? Mbona chini ya SADC amekuja na mpango tofauti na ule wa Kampala?
 
Last edited by a moderator:
Achana naye watu wengine kuelewa mambo hadi mifano 10 ubaoni. Wapi panaonyesha JK alikuwa pamoja na M7 na KGM zaidi ya mazungumzo ya Kampala? Usipoteze muda na Vilaza.
 
JK kastukia dili za kina M7 na Kagame. hao wanataka kufanya mazumgumzo ili kundi hilo lijumuishwe ktk serikali ya Congo na wao kina M7 waendelee kuiba rasilmali za DRC
 
Kitu kimoja kiko wazi na kitasumbua kwa muda mrefu saaaana KAGAME, KABILA (Hipolite) na MUSEVENI ni ndg wa damu na M23 ni watu wao MLENGWA Ni mali asili ya DRC hilo wacongo wanalijua vizuri. Kupanda kwa uchumi wa RWANDA ni matokeo ya uporaji huko DRC, M23 NI MAYARISHO YA HUYU KIJANA ANAPOONDOKA MADARAKANI AWE NA VITU VYA KUMFANYA AISHI VIZURI NA UMILIKI WA MALI NYINGI huku hao ndg zake wakifaidi umeme na madini ya bure na kumlinda.
 
Unadhani Congo isipokuwa stable mtu wangu malori yake ya Mafuta yatafanya kazi gani?
 
Back
Top Bottom