Malawi nao watatoa wanajeshi kwenda Congo.Lazima tukubali ustawi wa Congo una faida kubwa sana kwetu kiuchumi kuliko hata Kenya.
Tumejiandaaje kufaidika kiuchumi ktk Congo itayostawi.
Bila kusita namuunga mkono Rais Kikwete kwa maamuzi haya!
Tatizo la DRC na maamuzi ya SADC ni zaidi ya Rwanda na Uganda. UN wana kikosi cha kulinda usalama pale nafikiri kikubwa Africa kama sio duniani. UN wanatumia fedha nyingi kwa shughuli hii! Ajabu ni kuwa mambo haya yanatokea mbele ya kikosi hiki! Maamuzi ya SADC ni kuwaambia UN you have failed us...lakini wakati huo huo wanataka wapate support ya UN. Je hii itawezekana tuwe na vikosi viwili vyenye mandate ya UN - na sijui Kama mandate ya hivi vikosi zitatofautiana. Kuna suala la funding, bila support ya UN je SADC wataweza kumudu kwa muda mrefu? Tujue hii si kazi ya mwezi mmoja inaweza kuchukua miaka na ni aghali siyo kwa fedha tu Bali hata maisha ya vijana wetu.
Mkuu Ritz sisemi JK alikuwa pamoja na Museveni au Kagame.Read between the lines maelezo yangu. JK alishiriki kikao cha Kampala na kufikia maazimio kadhaa dhidi ya Kinshasa na waasi wa M23 lakini leo kayaweka pembeni maazimio hayo na kuja na azimio la kuunda Jeshi la kudhiti rebel militias Kivu chini ya SADC.
Nimeeleza kuunga mkono wazo hili lakini nikahoji sababu ya JK kuunga mkono maazimio ya Kampala wakati hakuyaafiki, je ilitokana na yeye kuzidiwa nguvu na akina Kagame na Museveni? Mbona chini ya SADC amekuja na mpango tofauti na ule wa Kampala?
Mkuu Ritz sisemi JK alikuwa pamoja na Museveni au Kagame.Read between the lines maelezo yangu. JK alishiriki kikao cha Kampala na kufikia maazimio kadhaa dhidi ya Kinshasa na waasi wa M23 lakini leo kayaweka pembeni maazimio hayo na kuja na azimio la kuunda Jeshi la kudhiti rebel militias Kivu chini ya SADC.
Nimeeleza kuunga mkono wazo hili lakini nikahoji sababu ya JK kuunga mkono maazimio ya Kampala wakati hakuyaafiki, je ilitokana na yeye kuzidiwa nguvu na akina Kagame na Museveni? Mbona chini ya SADC amekuja na mpango tofauti na ule wa Kampala?
Ni ajabu sana Kagame na Museven wanatuhumiwa kusaidia waasi wa M23 na haohao (watuhumiwa) ndiyo wako moto kweli kutafuta suluhu DRC.Ati wanajifanya kuratibu mazungumzo kati ya Waasi na Serikali ya Kinshasa. Kweli kuna suluhu hapo? Si kutaka kumtesa na kumbana Joseph Kabila kuishia kuruhusu nchi kukaliwa na waasi hawa?
Ninachoshindwa kuelewa ni kitendo cha JK kuafikiana na akina Museveni na leo ghafla anaingia makubaliano mengine na SADC tena yenye kutengua makubailiano ya Kampala. Je JK hakuona tatizo katika maazimio ya Kampala? Alizidiwa nguvu na akina Kagame? Maswali ni mengi hapa.
Mnyonge mnyongeni ila mpeni haki yake!!!!!!!1
JK hakukubaliana na hao jamaa [M7 na Kg]. Kumbukeni jambo moja kwamba kabla hajaenda uganda alishasema tanzania itasaidia kutoa walinzi wa amani. lakini baada ya kile kikao cha uganda M7 kama mwenyekiti wa kile kikao alitoa maazimio ambayo hayakuwa na kipengele hata kimoja kilichotoka Tanzania. Tafsiri yake ni rahisi sana kwamba KAgame na M7 walimgeuka JK wakijua yeye ni kilaza watampelekapeleka tu bila kujua kwamba Tanzania bado ina marafiki wengi na wanaoiheshimu. Kawasiliana na Angola, Msumbiji, Sauth Africa, Zimbabwe na Namibia wakakubaliana kuwadhibiti hawa majambazi wawili. Kilichofuatia JK katumia mlango wa nyuma kuwadhibiti M7 na Kagame [jikumbushe udharura wa hicho kikao cha SADC kilichotanguliwa na kamati ya SADC ya ulinzi na usalama]. JK played a very smart game on this! we must aknowledge and praise his move!!.....
Mpaka lini Museveni na Kagame wataendelea kuogopwa kama ni mabwana wakubwa?
Mkuu hawa hawaogopwi,nadhani kila nchi inaangalia maslahi yake ikijiingiza kwenye huo mgogoro.Lakini huwa nahisi ipo siku hawa wataitenga Tanzania kwenye hiyo EAC maana huko tuendako tutatofautiana kwenye mengi.
REPUBLIC OF KIVU
Why not?Leo kuna Sudan Kaskazini na Sudani Kusini,Binafsi naiona Congo ni kubwa mara mbili na robo ya Ethiopia kiasi kuwa Utajili mali ya asili yake auwafaidishi wakongomani kwa kuwa augawiki ipasavyo.Nimepata kusikia ujio wa NCHI INAITWA KIVU kwa mwenendo huu naona kuna haki pia ya kuhoji umma wa kama Nchi iyo iwepo au la!!!Watanzania kwenda huko ni kwenda kutuliza kwa muda kisha baada ya miaka kadha wa kadha kinanuka upya!!!
Mkuu MTAZAMO, uhuru wa nchi za kiafrika nyingi umekuwa dhaifu kwa kufikiria kwamba baada ya kutangazwa tu, wakoloni walikoma kufikiria jinsi ya kuzinyonya nchi hizi. Hili ndo limepelekea kujikuta kwenye ukoloni mambo leo bila kijijua. Kikubwa hapa ni kuulinda uhuru daima na milele. How?
Kuwa na uchumi imara.
Kuwa na elimu bora.
Kuwa na afaya bora.
Kuwa na umoja katika nchi ili kunapotokea adui, anakuwa adui wetu wote kama nchi.
Kuwa na jeshi la kutosha.
Na mambo mengine kibao.
Kwa hiyo, lazima tujiwekeze kwenye hivyo vitu kwani huji M25 inaweza kutengezwa na hao watu ikaelekezwa Tanzania kama wanaona ndo kikwazo kwa kile wanachotaka. Lazima tuwe tayari kujilinda kwa kila kitu.
Tungekuwa na AU imara Afrika ingetulia.Utulivu ndio msingi wa maendeleo na kama mnao utulivu na hamjaendelea ni debate nyingine!
Tuna AU dhaifu kuliko hata OAU ilivyokuwa pamoja na mapungufu yake.
Mnyonge mnyongeni ila mpeni haki yake!!!!!!!1
JK hakukubaliana na hao jamaa [M7 na Kg]. Kumbukeni jambo moja kwamba kabla hajaenda uganda alishasema tanzania itasaidia kutoa walinzi wa amani. lakini baada ya kile kikao cha uganda M7 kama mwenyekiti wa kile kikao alitoa maazimio ambayo hayakuwa na kipengele hata kimoja kilichotoka Tanzania. Tafsiri yake ni rahisi sana kwamba KAgame na M7 walimgeuka JK wakijua yeye ni kilaza watampelekapeleka tu bila kujua kwamba Tanzania bado ina marafiki wengi na wanaoiheshimu. Kawasiliana na Angola, Msumbiji, Sauth Africa, Zimbabwe na Namibia wakakubaliana kuwadhibiti hawa majambazi wawili. Kilichofuatia JK katumia mlango wa nyuma kuwadhibiti M7 na Kagame [jikumbushe udharura wa hicho kikao cha SADC kilichotanguliwa na kamati ya SADC ya ulinzi na usalama]. JK played a very smart game on this! we must aknowledge and praise his move!!
Sikubaliani na Kagame/Museveni kumshurutisha Kabila awe na power sharing na M23. Wanaongoza through fear mongering na ukabila ... wananchi wa Congo wapewe elimu ya political process kama njia ya kupata serikali wanayoitaka.
Vita inawaathiri wanawake na watoto .... soi it's a noble thing to go and protect our neighbors and let these people know that enough is enough!
Mkuu wanaoifaidi Congo ni wageni, je itakuwa hivyo mpaka lini?Huwa sielewi hii kitu,tuna ndoto ya kuunganisha bara la Afrika huku tukiendelea kuligawa vipande! Kesho mtaigawa Kivu alafu baadae Kivu na Congo zitaomba kujiunga EAC ambayo tunaota ije kuwa nchi moja what a dream!!!
Ni tamaa za viongozi tu,Kwa mfano Tanzania ni nchi kubwa sana pia kuliko zote EA,unadhani mkuu DSN tukitofautiana solution itakuwa kuigawa pia?
Kongo ni ya Wakongo tuwaache waamue wenyewe bila kuwaingilia na cha kuwasaidia ni kuimarisha usalama na kulijenga upya jeshi lao ili lisimamie usalama bila kuingiliwa na watawala wenye uchu.
Pamoja na hayo yote naomba mnijuze: Inakuwaje nchi kubwa na yenye maliasili nyingi kama DRC inatishiwa na "KANCHI" kama Rwanda?
WOWOWO, naomba nikukumbushe kwamba hivi ni vikao viwili tofauti na JK siyo muwakirishi wa SADC kwenye EAC na vivyo hivyo kinyume chake. Kwa hiyo JK anakwenda kama fresh member kwenye EAC na SADC. Kama EAC inahitaji muwakirishi kwenye SADC itapeleka itatuma mjumbe wake na vivyo hivyo kwa SADC kwenye EAC. Kama EAC members wake ni Museven na Kagame ambao wanakuwa karibia theluthi ya wanachama wote, huoni wanaweza kuinfluence matokeo ya mkutano wote. JK hahitaji kubishana na watu ambao anajua kabisha upande wao katika mgogoro. Alichokifanya JK ni sahihi kabisa kuonyesha kwamba anakerwa na tabia zao za udumila kuwili. Nani kigeu geu hapa, JK anayefanya maamuzi yanayooneka kwa uwazi kabisa kwa kutangazwa na vyombo vya habari au Kagame na Museveni wanaowaunga mkono waasi, M23, halafu kwenye vyombo vya habari wanakataa. Dawa ya jeuri ni kuwa jeuri zaidi yake. Big up JK. Kwanza muonyeshe Kagame kwamba anaongoza mkoa mmoja tu kwa Tanzania wakati wewe unaongoza nchi kubwa mara hamsi ya kwake kwa dharau zake alizowahi kuwa nazo. Kwa kifupi, Kagame na Museveni kwa support ya USA na Ulaya wamekuwa na kiburi sana kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati. Sasa wataona moto wake, na hao washirika wao [USA na Ulaya] kwa kuwa wanatabia ya ku-use na ku-abuse, very soon watawatupa kama kondom iliyotumika. Ndipo Rwanda itarudi tena kwenye dimbwi la ukabila tena.