JK: Hatutaki Rais mzee 2015

Uchaguzi wa 2010 umedhihirisha nini? Tusidanganyane hapa. Ukweli ni kuwa Chadema ina safari isiyo na mwisho kabla ya kuchukua urais.

safari ya aina hiyo haipo kawadanganye huko facebook,kwa mtu anayejua ni wapi anaenda lazima atafika mwisho wa safari,unachotakiwa kuthibitisha hapa ni kivipi cdm imepoteza au haijui huko iendako hadi safari hiyo isiwe na mwisho.katika kujibu remember to attach with evidence....
 
Kama kweli Kikwete ametamka hivyo, nafikiri atakuwa anazungumza kama mwenyekiti wa chama na kwa niaba ya chama chake lakini kama anazungumza kama Rais wa JMT atakuwa anakiuka misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (KJMT) ambayo aliapa kuilinda na kuiheshimu.


Sifa za mtu kugombea na kuchaguliwa kuwa Rais wa JMT ziko wazi ndani ya katiba na JK hana mamlaka ya kujifinyangia sifa nyingine nje ya hizo (Ibara ya 39 ya KJMT inaweka wazi juu ya sifa hizo).
 
Sasa kama ni kweli - alisema hivyo - na anaamini hivyo kwanini yeye mwenyewe na makamu wake wasijiuzulu sasa ili kutuondolea kutawaliwa na RAis Mzee?
Mkuu ina maana hujaisoma picha tu mpaka leo? Anzia kikao cha NEC ya CCM, then kurudiwa kwa uchaguzi wa mgombea Aru meru Mash. From there you might come up with something in your mind!
 
JK huwa hajui anaongea nini?alijinadi mwaka 2005 kuwa ni kijana matokeo yake ni mautumbo matupu..yaani ni bora kuchagua rais mzee kama mugabe akawa na akili kuliko kijana mwenye kazi ya kuchekacheka na kujipaka ma carolite...
 
PIa swala la kuwa na Afya njema ni muhimu kwa rais na sio umri tu, Kwani gharama za India ni kubwa sana. pia asiwe vasco dagama , budget yetu kiduchu

Nakubaliana na wewe kuwa afya njema kwa Rais wa nchi ni muhimu hivyo wagombea hawana budi kupimwa na kujulikana wazi kuwa afya zao hazina mgogoro; lakini pia niongezee kuwa hakuna uhusianao kati ya umri wa mtu nakuwa na afya duni kwani kuna vijana wenye afya zilizozorota na vijana wenye afya njema,pia wazee wenye afya njema na wengine wenye afya zilizozorota!! Zitto na Chami walikuwa India karibuni kwa matibabu na hao ndio mnaowaita vijana!! Juu ya hayo uadilifu pia kama afya, kuna vijana wasio waadilifu na wazee waadilifu; una habari ya dollar millioni moja alizoletewa January Makamba azitumie wakati wa uchaguzi 2010 ili apite ubunge lakini azirudishe pindi angechaguliwa kuwa waziri wa nishati!! Hapo sijazungumzia ya Zitto na hongo za Dowans!!
 
radhia@ unakeraaaaaaaaaaa, naonauna mawazo yako km kiroboto vilee!!!
 



Mimi nionavyo kigezo cha kupata Rais bora ni zaidi ya umri tu,ikiwa ni pamoja na busara na akili iliyotulia.Mh.akitaja umri mzee kwasasa basi, aangalie hata kwa mawaziri,wakuu wa mikoa,wakurugenzi,mabalozi na wateule wengine wa Rais kuwa kwasasa hawana sifa ya kuongoza zama hizi.Huo utakuwa ujumbe uliokuwa umebebwa na hotuba yake.
 
Watu wanaendeshwa kwa hisia na si uhalisia, tufike wakati tuheshimu mawazo ya watu kwani pindi atapotoa mawazo yake si lazima yakubalike na si lazima watu washangae kwani yeye amezungumza kama ni mtanzania mwenye haki ya kuongelea mwenendo wa taifa lake.

pia kusema rais ajaye awe kijana haina maana yeye ajiuzulu wadhifa wake kwani inawezekana kaona matatizo yanayomkuta na uwezo wake dhahifu wa kuweza kukabiliana nayo hivyo anajaribu kuweka mwanga kwa siku za usoni kwani unapojikwaa inama na utoe jiwe mwingine asije jikwaa kwenye jiwe hilo.

Umri wa kupiga kura unaweza kubaki 18 lakini umri wa kugombea urais ushuke mpaka miaka 30. ni mawazo yangu tu naruhusu mgongano wa mawazo
 
Kikwete anafikiri anaweza kuongea lolote bila kuangalia matokeo yake??hajui kwamba yeye ni publick figure??huyu mzee hajitambui kabisa!
 
rais ni taasisi nyeti na muhmu mno wanajf,kwa mawazo yangu tu madogo,suala la umri linamata sana,rais kijana hafai na rais mzee sana naye hafai,hivyo basi atleast kuanzia miaka 50-70 wapewe nafasi,
 
Kikwete hawezi kutuchagulia wananchi Rais ajaye, asitumie udhaifu wake kwamba wazee wote watakuwa na uwezo kama wake.
 
...kama aliyasema yaliyonukuliwa sisi neutrals tunamchukulia JK alikuwa anamaanisha "hatutaki mgombea uraisi mzee ccm 2015".

so, am not bothered at all by JK's comments (if he ever made them that is) because 2015 president is unlikely to come from his ccm.
 
Wazazi huyu Jua anaongea nini kwani hajui maana ya uraisi anagalia navyo watesa watanzania wananchi wamekondeana maana lishe mbovu wazazi idhaa bei ju kilasiku.....watu wanalia maisha magumu yeye anakenua meno.... hawezi kutu chagulia raisi
 
Hatutaki wazee kama kina Sitta na Mwandosya tunataka vijana kama kina Lowassa.

Tatizo jinginehili, kwani hamna wengine mpaka huyo EL;Kukariri kubaya sana, Tulimkariri huyumaandazi anayetuongoza sasa ndo katufikisha hapa
 
sasa naona january na zitto wamelewa sifa, wanafikiri kila wanachoongea ni sahihi. Swala la umri mkubwa ni muhimu sana katika ngazi kubwa kama ya uraisi wa nchi. tunajua matatizo ya vijana. Na kama wanataka urais si wasubiri. Na JK kama kaongea hivyo naona kachanganyikiwa. Tuache ubaguzi wa wazee na vijana ni kosa kubwa sana. na sio kitu cha kushabikia kwa sisi vijana, tukumbuke Leo kijana kesho utakuwa mzee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…