Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 242
Rais Kikwete aumbuka
Na Saed Kubenea
KUMBE Rais Jakaya Kikwete hakusoma sheria aliyosaini kwa mbwembe.
Sasa baada ya kugundua kasoro zake anataka ikarabatiwe kwa njia ya
kanuni, MwanaHALISI limeelezwa.
Hilo liligundulika katika mkutano wa wajumbe wa Halmashauri Kuu
(NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wenyeviti na makatibu wa wilaya
uliomalizika wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.
Taarifa za ndani zinasema, bila aibu na hasa kwa ujasiri wa
kiongozi mkuu wa nchi, Rais Kikwete alimuuliza Philip Marmo, waziri
wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, maana ya baadhi ya vifungu katika
sheria hiyo.
Lakini katika hali ambayo haikutegemewa, Marmo alijibu kana kwamba
anamkejeli rais, jambo ambalo lilistua wajumbe wa kikao hicho cha
juu cha utekelezaji wa sera za chama.
MwanaHALISI limeelezwa kwamba Rais Kikwete alistushwa na kifungu
cha sheria kinachotaka mgombea kuwasilisha katika ofisi za msajili,
taarifa ya fedha atakazotumia.
Kifungu hicho kinatoa siku saba kabla ya siku ya mwisho ya NEC
kutangaza majina ya wagombea.
Kifungu kingine kinachodaiwa kumstua kinahusu idadi ya wajumbe wa
kampeni. Kwa CCM, yenye hata vikundi vya ngoma na nyimbo kama ToT,
kuweka timu ndogo kunaweza kupunguza shamrashamra na kuathiri
kampeni.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa, ilikuwa baada ya rais kupitia maeneo
hayo, alimuuliza Waziri Marmo iwapo kile alichokuwa akifafanua
kimetokana na sheria iliyopitishwa.
Naye Marmo, akiongea kwa sauti ya unyenyekevu alijibu, hiki
ndicho ulichosaini.
Kwa kauli ya Marmo, Rais Kikwete alionekana kustuka na kusema, kama
hali ni hivyo, basi sheria itakuwa imeingilia hata mchakato wa
wagombea ndani ya vyama, kimeeleza chanzo chetu.
Taarifa zinamnukuu rais akihoji kwa nini sheria imekwenda mbali
mno na kuagiza papohapo kuwa wahusika waangalie ambapo sheria
inaingiliana na watengeneze kanuni zitakazoleta nafuu.
Rais amenukuliwa akimwagiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutengeneza
kanuni vizuri ili kuondoa mwingiliano unaoleta ugumu wa
utekelezaji.
Hoja ya maelekezo ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi ilikuwa
moja ya ajenda za kikao cha NEC, wenyeviti na makatibu wa CCM
wilaya kutoka kote nchini.
Tarehe 17 Machi mwaka huu, Rais Kikwete alisaini hadharani na kwa
mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ikulu Dar es Salaam ambapo
hafla hiyo ilihudhuriwa na majaji, wabunge, viongozi wa serikali na
vyama vya siasa, mabalozi na waandishi wa habari.
Hata hivyo, sheria hii imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya siasa na
wanaharakati, kabla na baada ya kusainiwa kuwa itakuwa ya udhibiti
kwa wenye msimamo tofauti na watawala.
Aidha, siku tatu baada ya sheria hiyo kusainiwa, mbunge wa Karatu
(CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitupa kombora kwa kusema sheria
aliyosaini rais ilikuwa na vipengele ambavyo havikujadiliwa bungeni
na kwamba viliingizwa kinyemela.
Ubishi wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Frederick Werema
kwamba hakukuwa na chochote kilichofanywa kinyemela ndio umekuza
hoja ya Dk. Slaa na kufanya achimbue zaidi kshfa hiyo.
Katika kufukua, Dk. Slaa amekwenda hadi kwenye kumbukumbu za bunge
(Hansard) na kuthibititisha kuwa Kifungu 7 (3) ambacho kimo katika
sheria aliyosaini rais hakikujadiliwa bungeni na hivyo
hakikurekodiwa katika hansard.
Mtunga sheria huyo kutoka Karatu amesema pia kuwa chochote
kilichojadiliwa bila kuamuliwa na bunge kilikuwa kinatarajiwa tu
katika kanuni au fafanuzi za au ainisho za maneno na taratibu
lakini siyo katika vifungu vya sheria.
Katika majibu yake kwa kauli za Dk. Slaa, Jaji Werema alitetea
serikali na kuthibitisha kuwa kifungu hicho kiliwekwa na waziri
Marmo.
Dk. Slaa amesema katika andishi maalum, Hakuna mwenye mamlaka,
hata rais hana mamlaka hayo, sembuse waziri.
Baada ya mjadala katika Kamti ya Bunge zima, maneno yakikubaliwa
ndiyo hayo yanaingia kwenye sheria na serikali haina mamlaka ya
kwenda kuyarekebisha inavyotaka. Ndiyo maana ya kusema kifungu
kimepitishwa, ameeleza Dk. Slaa.
Akiweka msisitizo, Dk. Slaa anasema, Kitendo cha kuchomeka
kinyemela ni kitendo kibaya sana na kinapaswa kulaaniwa, kwa
sababu, kwa utaratibu huu wataalam wanaweza kuipeleka nchi pabaya
kwa kupenyeza jambo lolote wanalotaka wao hata kama halijajadiliwa
au limekataliwa na Bunge.
Dk. Slaa anafafanua hatua ya serikali ya kuingiza mambo kinmyemela
katika sheria kuwa ni kosa la jinai na kusema hata kifingu
walichochomeka kinyemela kina madhara makubwa.
Kifungu kilichoongezwa na serikali kinataka timu ya kampeni
kukaguliwa na watendaji wa serikali ya CCM.
Kampeni ndiyo inayobeba mikakati na siri yote ya uchaguzi.
Haiingii akilini kabisa kuwa serikali (pengine unayotaka kuiondoa
kwenye uchaguzi ambayo ndio haki ya msingi ya kila mgombea) ndiyo
inaweka mkono wake kwenye udhibiti wa mikakti hiyo, anafafanua Dk.
Slaa.
Anasema kuweka kifungu kama hicho ni wenda wazimu, kwa mtu yeyote
aliyefikiria jambo hilo, au anaandika tu kutoka mezani na au hajui
maana halisi na majukumu yake.
Kutokana na kuibuka kwa kashfa hii, serikali sasa imeamua sheria
hiyo irejeshwe bungeni ili kufanyiwa marekebisho yanayostahili.
Naye Dk. Slaa tayari ametoa pendekezo: Namna pekee ya kuepukana na
athari hiyo ni kwa serikali kukiri imefanya makosa, na ndio
ustaarabu bila kutafuta visingizio.
Anasema serikali iwasilishe kwenye Mkutano wa 19 wa Bunge hili
ulioanza jana, kitu kinachoitwa Miscellaneous Amendment
marekebisho ya sheria mbalimbali na au ikichelewa sana katika
Bunge la Bajeti.
Wachunguzi wa mambo wanasema Rais Kikwete atakuwa amesikitishwa
sana na hatua ya wasaidizi wake ya kumchomekea vitu ambavyo
baadaye vinamomonyoa hadhi yake kama mkuu wa nchi.
Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wamempotosha au wameshindwa kumsaidia
rais, ni pamoja na Jaji Werema ambaye ametetea uingizaji kinyemela
kipengele ambacho hakikujadiliwa bungeni.
Mwingine anayetajwa ni waziri Marmo ambaye ambaye nduye hasa
ametajwa kubuni na kuingiza maneno ya kifungu kinacholaaniwa.
Source: Mwamahalisi Issue No. 184
Na Saed Kubenea
KUMBE Rais Jakaya Kikwete hakusoma sheria aliyosaini kwa mbwembe.
Sasa baada ya kugundua kasoro zake anataka ikarabatiwe kwa njia ya
kanuni, MwanaHALISI limeelezwa.
Hilo liligundulika katika mkutano wa wajumbe wa Halmashauri Kuu
(NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wenyeviti na makatibu wa wilaya
uliomalizika wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.
Taarifa za ndani zinasema, bila aibu na hasa kwa ujasiri wa
kiongozi mkuu wa nchi, Rais Kikwete alimuuliza Philip Marmo, waziri
wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, maana ya baadhi ya vifungu katika
sheria hiyo.
Lakini katika hali ambayo haikutegemewa, Marmo alijibu kana kwamba
anamkejeli rais, jambo ambalo lilistua wajumbe wa kikao hicho cha
juu cha utekelezaji wa sera za chama.
MwanaHALISI limeelezwa kwamba Rais Kikwete alistushwa na kifungu
cha sheria kinachotaka mgombea kuwasilisha katika ofisi za msajili,
taarifa ya fedha atakazotumia.
Kifungu hicho kinatoa siku saba kabla ya siku ya mwisho ya NEC
kutangaza majina ya wagombea.
Kifungu kingine kinachodaiwa kumstua kinahusu idadi ya wajumbe wa
kampeni. Kwa CCM, yenye hata vikundi vya ngoma na nyimbo kama ToT,
kuweka timu ndogo kunaweza kupunguza shamrashamra na kuathiri
kampeni.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa, ilikuwa baada ya rais kupitia maeneo
hayo, alimuuliza Waziri Marmo iwapo kile alichokuwa akifafanua
kimetokana na sheria iliyopitishwa.
Naye Marmo, akiongea kwa sauti ya unyenyekevu alijibu, hiki
ndicho ulichosaini.
Kwa kauli ya Marmo, Rais Kikwete alionekana kustuka na kusema, kama
hali ni hivyo, basi sheria itakuwa imeingilia hata mchakato wa
wagombea ndani ya vyama, kimeeleza chanzo chetu.
Taarifa zinamnukuu rais akihoji kwa nini sheria imekwenda mbali
mno na kuagiza papohapo kuwa wahusika waangalie ambapo sheria
inaingiliana na watengeneze kanuni zitakazoleta nafuu.
Rais amenukuliwa akimwagiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutengeneza
kanuni vizuri ili kuondoa mwingiliano unaoleta ugumu wa
utekelezaji.
Hoja ya maelekezo ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi ilikuwa
moja ya ajenda za kikao cha NEC, wenyeviti na makatibu wa CCM
wilaya kutoka kote nchini.
Tarehe 17 Machi mwaka huu, Rais Kikwete alisaini hadharani na kwa
mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ikulu Dar es Salaam ambapo
hafla hiyo ilihudhuriwa na majaji, wabunge, viongozi wa serikali na
vyama vya siasa, mabalozi na waandishi wa habari.
Hata hivyo, sheria hii imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya siasa na
wanaharakati, kabla na baada ya kusainiwa kuwa itakuwa ya udhibiti
kwa wenye msimamo tofauti na watawala.
Aidha, siku tatu baada ya sheria hiyo kusainiwa, mbunge wa Karatu
(CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitupa kombora kwa kusema sheria
aliyosaini rais ilikuwa na vipengele ambavyo havikujadiliwa bungeni
na kwamba viliingizwa kinyemela.
Ubishi wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Frederick Werema
kwamba hakukuwa na chochote kilichofanywa kinyemela ndio umekuza
hoja ya Dk. Slaa na kufanya achimbue zaidi kshfa hiyo.
Katika kufukua, Dk. Slaa amekwenda hadi kwenye kumbukumbu za bunge
(Hansard) na kuthibititisha kuwa Kifungu 7 (3) ambacho kimo katika
sheria aliyosaini rais hakikujadiliwa bungeni na hivyo
hakikurekodiwa katika hansard.
Mtunga sheria huyo kutoka Karatu amesema pia kuwa chochote
kilichojadiliwa bila kuamuliwa na bunge kilikuwa kinatarajiwa tu
katika kanuni au fafanuzi za au ainisho za maneno na taratibu
lakini siyo katika vifungu vya sheria.
Katika majibu yake kwa kauli za Dk. Slaa, Jaji Werema alitetea
serikali na kuthibitisha kuwa kifungu hicho kiliwekwa na waziri
Marmo.
Dk. Slaa amesema katika andishi maalum, Hakuna mwenye mamlaka,
hata rais hana mamlaka hayo, sembuse waziri.
Baada ya mjadala katika Kamti ya Bunge zima, maneno yakikubaliwa
ndiyo hayo yanaingia kwenye sheria na serikali haina mamlaka ya
kwenda kuyarekebisha inavyotaka. Ndiyo maana ya kusema kifungu
kimepitishwa, ameeleza Dk. Slaa.
Akiweka msisitizo, Dk. Slaa anasema, Kitendo cha kuchomeka
kinyemela ni kitendo kibaya sana na kinapaswa kulaaniwa, kwa
sababu, kwa utaratibu huu wataalam wanaweza kuipeleka nchi pabaya
kwa kupenyeza jambo lolote wanalotaka wao hata kama halijajadiliwa
au limekataliwa na Bunge.
Dk. Slaa anafafanua hatua ya serikali ya kuingiza mambo kinmyemela
katika sheria kuwa ni kosa la jinai na kusema hata kifingu
walichochomeka kinyemela kina madhara makubwa.
Kifungu kilichoongezwa na serikali kinataka timu ya kampeni
kukaguliwa na watendaji wa serikali ya CCM.
Kampeni ndiyo inayobeba mikakati na siri yote ya uchaguzi.
Haiingii akilini kabisa kuwa serikali (pengine unayotaka kuiondoa
kwenye uchaguzi ambayo ndio haki ya msingi ya kila mgombea) ndiyo
inaweka mkono wake kwenye udhibiti wa mikakti hiyo, anafafanua Dk.
Slaa.
Anasema kuweka kifungu kama hicho ni wenda wazimu, kwa mtu yeyote
aliyefikiria jambo hilo, au anaandika tu kutoka mezani na au hajui
maana halisi na majukumu yake.
Kutokana na kuibuka kwa kashfa hii, serikali sasa imeamua sheria
hiyo irejeshwe bungeni ili kufanyiwa marekebisho yanayostahili.
Naye Dk. Slaa tayari ametoa pendekezo: Namna pekee ya kuepukana na
athari hiyo ni kwa serikali kukiri imefanya makosa, na ndio
ustaarabu bila kutafuta visingizio.
Anasema serikali iwasilishe kwenye Mkutano wa 19 wa Bunge hili
ulioanza jana, kitu kinachoitwa Miscellaneous Amendment
marekebisho ya sheria mbalimbali na au ikichelewa sana katika
Bunge la Bajeti.
Wachunguzi wa mambo wanasema Rais Kikwete atakuwa amesikitishwa
sana na hatua ya wasaidizi wake ya kumchomekea vitu ambavyo
baadaye vinamomonyoa hadhi yake kama mkuu wa nchi.
Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wamempotosha au wameshindwa kumsaidia
rais, ni pamoja na Jaji Werema ambaye ametetea uingizaji kinyemela
kipengele ambacho hakikujadiliwa bungeni.
Mwingine anayetajwa ni waziri Marmo ambaye ambaye nduye hasa
ametajwa kubuni na kuingiza maneno ya kifungu kinacholaaniwa.
Source: Mwamahalisi Issue No. 184