JJ Mnyika (Mb) hana bei, ni CHADEMA hasa

JJ Mnyika (Mb) hana bei, ni CHADEMA hasa

Siasa ina mashujaa wake. Wanaohimili mikikimikiki ya kila wiki na mambo yao yanatiki. Mbunge John John Mnyika wa Kibamba kwa tiketi ya CHADEMA ni kati ya wanasiasa mashujaa hapa Tanzania. Mnyika hana bei,ni mwanaCHADEMA hasa.

Mnyika aliandamwa kwa lawama na kubanwa kipropaganda. Mnyika alisemwa amekasirika kwenda Lowassa CHADEMA,akawa kimya. Akasemwa anaumwa hata kuchanganyikiwa,akawa kimya. Akasemwa hamkubali Katibu wake Mkuu mpya,Dr. Mashinji,akawa kimya. Akaandikwa na kusemwa kuwa anajiandaa kuhama chama chake,akawa kimya.

Hata hapa Dodoma,alitajwatajwa kama mmoja wa watakaofanyiwa usajili tarehe 23 mwezi huu. Mnyika hajali wala kutikisika. Anaendelea kutekeleza majukumu yake muhimu ya chama chake kwa kusonga mbele kuelekea kwenye kilele. Mnyika si wa kawaida. Hajajibu wala kuyumbishwa na yaliyosemwa. Hana bei. Ni shujaa.

Amenikumbusha mbinu za kuishi Seminarini. Seminari aliyosoma Mnyika imempika. Imempa uhodari mahiri. Ukimya nao ni jibu mujarabu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)

Na akatoka na A's 9 ambapo hakuna mwana CCM nchi hii amewahi kuipata.
Hivi Lizaboni ulipata ngapi?
 
Vya CCM vinavyoendelea hapa

Mzee Tupatupa
Kuna mwanaccm mwenzako alileta uzi hapa kwamba kuna wanachama wa upinzani (chadema)wakiwemo wabunge watajiunga na magamba tarehe 23.Tetesi hizo niza kweli mzee wangu?
 
Wapo vijana wengi upinzani wana kiu ya mabadiliko na kuimaliza safari ya ushindi mnyika ni mmoja wapo
 
Tunahitaji kuona anawafanyia nini wananchi wa jimbo la kibamba waliompeleka mjengoni ,si wakati wa siasa sasa hivi ni uwajibikaji kwa wananchi wake sio blaa blaa tuu.
Vitendo kwanza, maneno baadae.
 
Siasa ina mashujaa wake. Wanaohimili mikikimikiki ya kila wiki na mambo yao yanatiki. Mbunge John John Mnyika wa Kibamba kwa tiketi ya CHADEMA ni kati ya wanasiasa mashujaa hapa Tanzania. Mnyika hana bei,ni mwanaCHADEMA hasa.

Mnyika aliandamwa kwa lawama na kubanwa kipropaganda. Mnyika alisemwa amekasirika kwenda Lowassa CHADEMA,akawa kimya. Akasemwa anaumwa hata kuchanganyikiwa,akawa kimya. Akasemwa hamkubali Katibu wake Mkuu mpya,Dr. Mashinji,akawa kimya. Akaandikwa na kusemwa kuwa anajiandaa kuhama chama chake,akawa kimya.

Hata hapa Dodoma,alitajwatajwa kama mmoja wa watakaofanyiwa usajili tarehe 23 mwezi huu. Mnyika hajali wala kutikisika. Anaendelea kutekeleza majukumu yake muhimu ya chama chake kwa kusonga mbele kuelekea kwenye kilele. Mnyika si wa kawaida. Hajajibu wala kuyumbishwa na yaliyosemwa. Hana bei. Ni shujaa.

Amenikumbusha mbinu za kuishi Seminarini. Seminari aliyosoma Mnyika imempika. Imempa uhodari mahiri. Ukimya nao ni jibu mujarabu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Umelala DOROOOhh! Propaganda zako za ''KIBAVIMCHWA'' HAZINA MASHIKO!!! leta Udaku wa mikocheni kwa KIONGOZI MKUU WA CHAMA!
 
Wakati nikiwa field fulani kuna mzee alinipa msemo wa kikwao ulionifurahisha sana. Alisema wawindaji ni waroho sana wa nyama na siku zote huomba kukutana na wanyama wakubwa kama nyati. Lakini akasema la kushangaza nyati akitokea wazee hao hukwea miti kwa woga na mbwa wao hufyata mikia.

Msemo huu umenikumbusha kelele zilizokuwa hapa Jf wakati Mnyika yuko kimya bize na kazi zake na kitabu. Wapo waliosema amekasirishwa na ujio wa nguri wa siasa kwenye chama chake, wapo waliosema ameudhiwa na kuondoka kwa baadhi ya wanasiasa ambao walikimbia mechi ya fainali (Uchaguzi mkuu). Wengine wakafikia hatua ya kusema atahama chama (Lukosi), wengine wakamzushia kuugua (Mungu apishe mbali).

Sasa ameibuka na kesi dhidi ya serikali kuminya demokrasia. Na kwa taarifa yenu huo ni mkakati namba moja. Mikakati inayofuata tunaomba msiombe 'PO' au kuhamisha magoli. Nilichojifunza Mnyika ni tishio na akipiga chafya 'nchi inaugua mafua'.

Stay tuned!
 
Mbona hajaonekana, tunasoma tu taarifa.
Najaribu ku-upload video yake kwenye simu nimeshindwa. Nikirudi ofisini ntatumia copmyuta ingawa najua kuna watu wanaweza kutuwekea hapa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom