Jiwe la sumu ya nyoka

Jiwe la sumu ya nyoka

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,104
Reaction score
828,989
Ni tiba ya vizazi na vizazi isiyothaminiwa wala kutangazwa kama zilivyo dawa za kihindi kizungu na kichina... Ugunduzi wa mwafrika Mmasai... Jiwe la sumu limesaidia kuokoa watu wengi sana hasa wale wa vijijiji
Sifahamu vema siri iliyomo kwenye hili jiwe dogo ambalo huwekwa kwenye jeraha bichi linalovuja damu, jeraha litokanalo na kuumwa na nyoka, nge au buibui... Unapoliweka hapo halibanduki mpaka linyonye sumu yote kwenye jeraha na likimaliza kazi hudondoka lenyewe
Likishadondoka unatakiwa kuliweka kwenye maziwa ili nalo kulitoa sumu liliyoinyonya wengine wanaita kulisafisha tayari kwa matumizi tena
IMG_20170905_132102.jpg
IMG_20170906_074419_081.jpg
huyo mjamaa hapo juu alining'ata usiku wa kuamkia jana, mida yetu ile..... Saa tisa kasoro! Nilistukia tu maumivu makali sana
Haraka sana nikatafuta tochi kali na kumulika,! Mungu ni mwema nikamkuta ni jamaa anajitahidi kutoroka! Nikamuwahi na kumpa haki yake RIP
NIiliwahi hospital nikapata tiba ya kizungu na mchana wa jana nimeweka hili jiwe ambalo mpaka sasa limeng'ang'ana... Kwahiyo sumu bado ipo
Ni tiba ya ajabu hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja mkuu

scratch my back & i'll scratch yours
 
Mkuu Mshana hiyo ni chemistry ambayo wazee wetu waliitumia nadhani bila wao kujua ni nini hasa kilikuwa kinatokea ni kama walivyokuwa wakibeba ndoo kichwani,ukiweka zinga/kata maana yake unapunguza pressure kwa kuongeza surface area ya kichwa,au unapopuliza moto unaongeza supply ya oxygen,back to Jiwe la nyoka japo siwezi kukumbuka vizuri maana elimu niliyokuwa napewa ilikuwa informal kidogo ,lile jiwe ni strongest reducing au oxidizing agents ambalo hutumiwa kureduce au kuoxiidiz sumu toka mwilini(sikumbuki vzuri) na kama sikosei lile jiwe potassium permanganate na watu wa chemistry mnajua ina oxid state ya +7
 
Ndio una miguu mizuri ivyo

sent from my iPhone 7 nimeinunua SAPNA pale Posta mtaa SAMORA
 
Kwa jinsi ninavyojua ni kwamba hilo jiwe lina vitundu vidogo vidogo vingi sana ambavyo si rahisi kuonekana kwa macho (microscopic pores) na hivyo kuwa na tabia ya kufyonza vimiminika kama maji, damu e.t.c. sasa unapokuwa umeng'atwa na nyoka na kuilipachika hilo jiwe unalifanya lianze kufyonza damu ambayo ina sumu ya nyoka kupitia vitundu vya meno ya nyoka na hivyo kupunguzaa sumu.

By the way, huyo noka sio hatari sana. U are very lucky mkuu!

Usisahau kukata kucha, unasaidia kupunguza encounters za nyoka. Hahahahaha...jus kidding bro!
 
Back
Top Bottom