Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Kwanza naomba radhi kwa Mods na members wote kwani najua JF haina itikadi ya kisiasa. Kama mjuavyo kuwa CHADEMA katika mikoa kadhaa ya Tz, Moro ikiwepo, bado inajitahidi katika kukubaliwa zaidi. Nawaomba wanachama, wafuasi na wapenda maendeleo wote mkoani hapa na Tz nzima watakaoguswa kujitolea, wajitolee katika kusaidia juhudi za CDM hapa Moro.Kwa sasa ipo mipango kazi miwili ambayo inahitaji michango ya kimawazo, kiushauri na kifedha. Nawaomba watakaoguswa kujitolea katika haya watembelee ofisi za chama mkoa pale mjini au kwa maelezo zaidi wanitumie private message.