Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Watu wengi wanapolala huota ndoto. Baadhi ya ndoto ni za kawaida, nyingine zinatoka kwa Mungu, na nyingine hutokana na akili zetu wenyewe. Lakini pia zipo ndoto zinazotokana na shetani. Ndoto za kishetani huleta hofu, mateso na kumfanya mtu akate tamaa. Ndoto za kishetani hazifurahishi bali zinakera na kuumiza moyo. Hii hapa ni mifano ya ndoto za kishetani:
Hebu tujifunze sasa jinsi ya kuzizuia ndoto hizo za kishetani
(a) Hakikisha unaishi maisha matakatifu
Dhambi huwapa mapepo nafasi ya kuwaingia watu na kuwatesa ndotoni. Kwahiyo mtu anayeishi maisha ya ulevi, uasherati, chuki, uongo na dhambi nyingine kama hizo, anakuwa ameacha mlango wazi wa kushambuliwa na shetani na mapepo yake katika ndoto. Kwahiyo kama umekuwa ukiishi dhambini, ili uweze kuzuia ndoto za kishetani, tubu dhambi zako na uanze kuishi maisha ya utakatifu mbele za Mungu.
(b) Omba kabla ya kulala
Maombi ni silaha kubwa ya kiroho. Kabla hujalala, omba na kumkabidhi Mungu roho yako, akili yako na mwili wako. Omba damu ya Yesu ikufunike kwa imani unapolala.
Huu hapa mfano wa sala: “Ee Mungu ninalala sasa. Naomba unifunike kwa damu ya Yesu Kristo. Nazuia mapepo na nguvu za giza kuja kunisumbua ndotoni, kwa Jina la Yesu, amen.”
(c) Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku
Neno la Mungu ni nuru. Likiangazia akili yako, giza haliwezi kuendelea. Soma Zaburi, hasa Zaburi ya 91, 27, au 23 kabla ya kulala. Zaburi hizo zitakupa amani na kuzuia usiote ndoto mbaya.
(d) Imba nyimbo za sifa na kuabudu
Sifa za Mungu zinamfukuza shetani. Nyimbo za kumtukuza Mungu zikijaa ndani ya moyo wa mtu, hata katika ndoto atakuwa katika hali ya amani.
(e) Takasa mazingira unayolala
Mazingira unayolala yanaweza kukuletea usumbufu wa kiroho. Hivyo uwe makini na picha unazobandika ukutani, picha unazotazama kwenye mitandao, miziki na vitu vinavyovuta roho za giza nyumbani kwako. Omba na kutakasa chumba chako kwa jina la Yesu Kristo.
(f) Funga na kuomba
Ukiona ndoto za kishetani zinajirudia rudia, ongeza gia ya maombi - funga na kuomba. Maombi ya kufunga humfanya mwamini kuwa na nguvu za rohoni na kufunga milango yote ya giza.
Usizipuuze ndoto za kishetani. Ndoto hizo ni mojawapo ya mbinu za shetani za kukuletea hofu, kukurudisha nyuma kimaisha na kukutesa. Lakini kama tulivyoona, kwa jina la Yesu Kristo tunaweza kuzuia ndoto za kishetani. Tangu nilipozijua siri hizo za kuzuia kuota ndoto za kishetani, nimekuwa nikiota ndoto za mafanikio, sherehe na ushindi.
Ukiyazingatia hayo, hutababaishwa tena na ndoto mbaya unapolala, bali utakuwa ukiota ndoto za amani, furaha na baraka kutoka kwa Mungu. Ulale unono usiku wa leo, katika Jina la Yesu, amen.
- Kuota unakimbizwa na wanyama wakali kama nyoka, mbwa au simba.
- Kuota unazama majini au unazuiliwa na nguvu za ajabu.
- Kuota unafanya tendo la ndoa na mtu asiye mume au mke wako (ndoto za mapepo ya mahaba – incubus/succubus).
- Kuota unaona mazishi, makaburi au watu waliokufa.
- Kuota unapigwa, unachinjwa au kushikwa na nguvu zisizo za kawaida.
- Kuota umefukuzwa shule au kazini bila sababu (ndoto za kurudishwa nyuma kimaendeleo).
- Kuota unakula chakula kisichojulikana.
Hebu tujifunze sasa jinsi ya kuzizuia ndoto hizo za kishetani
(a) Hakikisha unaishi maisha matakatifu
Dhambi huwapa mapepo nafasi ya kuwaingia watu na kuwatesa ndotoni. Kwahiyo mtu anayeishi maisha ya ulevi, uasherati, chuki, uongo na dhambi nyingine kama hizo, anakuwa ameacha mlango wazi wa kushambuliwa na shetani na mapepo yake katika ndoto. Kwahiyo kama umekuwa ukiishi dhambini, ili uweze kuzuia ndoto za kishetani, tubu dhambi zako na uanze kuishi maisha ya utakatifu mbele za Mungu.
(b) Omba kabla ya kulala
Maombi ni silaha kubwa ya kiroho. Kabla hujalala, omba na kumkabidhi Mungu roho yako, akili yako na mwili wako. Omba damu ya Yesu ikufunike kwa imani unapolala.
Huu hapa mfano wa sala: “Ee Mungu ninalala sasa. Naomba unifunike kwa damu ya Yesu Kristo. Nazuia mapepo na nguvu za giza kuja kunisumbua ndotoni, kwa Jina la Yesu, amen.”
(c) Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku
Neno la Mungu ni nuru. Likiangazia akili yako, giza haliwezi kuendelea. Soma Zaburi, hasa Zaburi ya 91, 27, au 23 kabla ya kulala. Zaburi hizo zitakupa amani na kuzuia usiote ndoto mbaya.
(d) Imba nyimbo za sifa na kuabudu
Sifa za Mungu zinamfukuza shetani. Nyimbo za kumtukuza Mungu zikijaa ndani ya moyo wa mtu, hata katika ndoto atakuwa katika hali ya amani.
(e) Takasa mazingira unayolala
Mazingira unayolala yanaweza kukuletea usumbufu wa kiroho. Hivyo uwe makini na picha unazobandika ukutani, picha unazotazama kwenye mitandao, miziki na vitu vinavyovuta roho za giza nyumbani kwako. Omba na kutakasa chumba chako kwa jina la Yesu Kristo.
(f) Funga na kuomba
Ukiona ndoto za kishetani zinajirudia rudia, ongeza gia ya maombi - funga na kuomba. Maombi ya kufunga humfanya mwamini kuwa na nguvu za rohoni na kufunga milango yote ya giza.
Usizipuuze ndoto za kishetani. Ndoto hizo ni mojawapo ya mbinu za shetani za kukuletea hofu, kukurudisha nyuma kimaisha na kukutesa. Lakini kama tulivyoona, kwa jina la Yesu Kristo tunaweza kuzuia ndoto za kishetani. Tangu nilipozijua siri hizo za kuzuia kuota ndoto za kishetani, nimekuwa nikiota ndoto za mafanikio, sherehe na ushindi.
Ukiyazingatia hayo, hutababaishwa tena na ndoto mbaya unapolala, bali utakuwa ukiota ndoto za amani, furaha na baraka kutoka kwa Mungu. Ulale unono usiku wa leo, katika Jina la Yesu, amen.