Jinsi ya kuwa gentleman

Jinsi ya kuwa gentleman

4 sure chief
Ni suala la ustaarabu na uungwana mkuu. Tena mambo hayo hua hayafundishwi darasani, si unaona kama wewe hapo unajisikia vibaya na unajizuia kabisa kufanya jambo litakalowakera watu wengine.

Huo ndio ustaarabu na uungwana. Kwa maneno mengine hiyo ndio tabia njema
 
Kuna jamaa alienda kula kwenye mgahawa mmoja msafi sana. Baada ya kula akaenda kunawa katika sinki la kunawia na alipoona lilivo safi akaanza ku shout

Akawageukia watu waliokua wanakula na kusema kwa sauti "Hivi ndio mgahawa unavotakiwa kua, yaani msafii. Sio kama kule kwengine mara ukute makohozi mara makamasi, vyooni watu wameharisha hawajamwaga maji"

Pamoja na kwamba katoa sifa nzuri panapostahili sifa je huyu nae anaingia kwenye kundi la waungwana(gentlemen)?
Alikua anataka kutapisha walaji[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna jamaa alienda kula kwenye mgahawa mmoja msafi sana. Baada ya kula akaenda kunawa katika sinki la kunawia na alipoona lilivo safi akaanza ku shout

Akawageukia watu waliokua wanakula na kusema kwa sauti "Hivi ndio mgahawa unavotakiwa kua, yaani msafii. Sio kama kule kwengine mara ukute makohozi mara makamasi, vyooni watu wameharisha hawajamwaga maji"

Pamoja na kwamba katoa sifa nzuri panapostahili sifa je huyu nae anaingia kwenye kundi la waungwana(gentlemen)?
Hapana hafai kuingia kwenye kundi la Waungwana
 
uzi mzurii na unafundisha.

Sio unajiita getleman unapga chafya ukiangalia hapo chini km imenyesha mvuaa, uso nao haufai, pua na mdomo km unapiga unda.

Ukitaka kujua sura halisi ya mwenza wako akizeeka subiri apige chafya
Umekufundisha nn?
 
uzi mzurii na unafundisha.

Sio unajiita getleman unapga chafya ukiangalia hapo chini km imenyesha mvuaa, uso nao haufai, pua na mdomo km unapiga unda.

Ukitaka kujua sura halisi ya mwenza wako akizeeka subiri apige chafya
Buhahahahahahaha nimecheka kifala yani
 
Image may contain: 1 person, sitting and shoes


Maisha halisi ya Gentleman.

1. Gentleman hupendelea kusema ‘tafadhari’ na ‘asante’
2. Gentleman kamwe hawezi kuicheka au kuidharau imani ya wenzake katika dini, siasa, michezo au kitu kingine chochote kile.
3. Gentleman mara kwa mara hubeba handkerchief (Kitambaa kidogo cha jasho) na yuko tayari kumpa mtu mwingine, hasa hasa msichana anayelia na kutokwa na mchozi kwa ajili ya kujifutia.
4. Gentleman kamwe hawezi kuubamiza mlango mbele ya wasichana, wavulana au watu wazima.
5. Gentleman kamwe hawezi kufanya utani juu ya ngozi, jinsia au dini.
6. Gentleman hujua kusimama katika foleni na kusubiri zamu yake ifike.
7. Gentlman mda wote yuko tayari kupeana mikono na watu kwa moyo mmoja.
8. Gentleman mara kwa mara viatu vyake huwa visafi na kucha zak kuziacha safi muda wote.
9. Gentleman huomba msamaha na kukubali kosa mara anapogundua kwamba amefanya kosa.
10. Gentleman huwa apigani au kuchonganisha ugomvi au fujo za aina yoyote ile.
11. Gentleman anajua jinsi ya kuwafanya wengine wajisikie huru.
12. Gentleman anapougua mafua, mara kwa mara hujitenga na wenzake kwa kuogopa kuwaambukiza ugonjwa huo.

GENTLEMAN NA MATUMIZI YAKE YA SIMU

Ingawa simu zimekuwa kila sehemu katika ulimwengu wa sasa, gentleman hujitahidi kutumia simu yake katika tabia nzuri. Anajua kwamba ingawa watu wengi wanafahamu kwamba simu ni lazima zitumiwe, hiyo kwake hawezi kuwafanyia watu karaha kutokana na uwepo wa simu yake katika matumizi yake.
Mara nyingi sana Gentleman anapopokea simu yake huwa haongei kwa sauti ya juu hasa anapokuwa katika sehemu iliyokuwa na mkusanyiko mkubwa wa watu. Hufanya hivi kwa sababu huwa hapendi kuwasumbua watu wengine kwa kelele za suati yake.
Anapokuwa katika kikao cha biashara na mara simu yake inapoita kwa ghafla, mara zote huomba radhi kwa kusema ‘excuse me’ na kisha kuipokea simu hiyo. Huwa hapigi simu yoyote mara anapokuwa katika kikao, na kama akifanya hivyo basi hufanya hivyo kutokana na mada ambayo inazungumziwa mahali hapo na anahijika mtu fulani kutoa maelezo na hayupo hapo.

SEHEMU AMBAZO MARA KWA MARA GENTLEMAN HUTUMIA SIMU YAKE.

* Hutumia simu yake katika kipindi ambacho yupo peke yake.
* Hutumia simu yake katika kipindi ambacho anaona kwamba hakuna mtu karibu yake ambaye
anaweza kumsumbua kutokana na sauti yake.
* Kama ni daktari, basi huiacha simu yake ofisini na kuipokea akiwa kule kule ofisini kwa kuhofia
kuwasumbua wagonjwa na watu wengine.
* Kama ni baba wa familia, mara kwa mara hutumia simu yake kuwasiliana na watoto wake au mfanyakazi wake wa ndani wa nyumbani pamoja na mkewe.

SEHEMU AMBAZO GENTLEMAN HAWEZI KUTUMIA SIMU YAKE.

* Anapokuwa nyuma ya msikani katika kipindi ambacho anaendesha gari au chombo chochote kile.
* Anapokuwa katika ibada, matamasha mbalimbali, sehemu za kuangalia sinema.
* Anapokuwa katika mghahawa.
* Anapokuwa katika chumba ambacho ni maalumu kwa kumsubiri mtu fulani, katika ofisi ya mtu yeyote yule na chumba cha mtihani.
* Anapokuwa katika foleni ya aina yoyote ile ambayo mara kwa mara watu uhitaji utulivu kwa ajili ya kuwasikiliza wahusika.
* Anapokuwa katika lifti, au hadi awe peke yake.
* Anapokuwa katika GYM.
* Anapokuwa katika basi au treni.
* Katika sehemu yoyote ile ambayo imeandikwa kwamba ‘Matumizi ya simu hayaruhusiwi’.
* Gentleman huwa hapigi picha ovyo kwa kutumia simu yake.
* Hawezi kutembea huku akiwa anatuma meseji kwa kutumia simu yake.

Itaendelea kesho.
Kumbe watu wenye tabia Kama hizi ndio hua tunaitwa magentleman, nashukuru mleta uzi kwa kujua nami nimo kwenye kundi hilo
 
Hapo kwenye KUPIGA kelele sasa mwanaume mzima anaongea Kama kafungiwa spika kifuani alafu yupo ofisini Ila Kama yupo gengeni ofisi nzima inatamalaki sauti yake Hana utulivu katika maongezi sauti ya kawaida awezi ongea ,anaongea Hadi mishipa ya uso ina msimama ,non stop utasema asha ngedere aliyekulia mwananyamala
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Kuongea uongo na vitu vya hovyo hovyo ili kujitetea ,hata Kama Ni kweli Kuna Mambo gentleman uwezi ongea kulinda heshima yako ,Mana maneno unayoongea ya mtu pia yanaweza kukuvua nguo wewe mwenyewe hahaha
 
Naona umetaja sifa za wanaume wa Daaslam wanaoshinda Saloon kutengeneza kucha na kusugua magaga.
Et Jantrumen kamwe hachafuki kucha! Labda jatrumeni wa kubeba vibegi vya akina Wema Sepenga.
Mwanaume wa Kweli hapangiwi kitu, muda wote ni Mapambano tu maisha yasonge.
hivi kwanini watu wa mikoani huchukulia uchafu wa mwilini na kuwa rough kimavazi kama sifa ya mwanaume?.

hii imekuwa ikinichanganya sana.
 
Uzi mzuri...ila mtu kuweza kuwa na sifa zote hizo ni ngumu...
 
uzi mzurii na unafundisha.

Sio unajiita getleman unapga chafya ukiangalia hapo chini km imenyesha mvuaa, uso nao haufai, pua na mdomo km unapiga unda.

Ukitaka kujua sura halisi ya mwenza wako akizeeka subiri apige chafya
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
ghafla nikajua jinsi ya kuwa gentamycine.

good bro but,hapo no 2,kwenye leso unataka ma gent tuaibike,utoe leso yako mfukoni umpe demu anayelia wa dsm aipokee afutie machozi[emoji23][emoji23][emoji23]bro hauko serious.

hawezi ipokea.labda akujue.
Gentamcyine anawatambalizia mapopoma comments za kutosha kwa kutumia ile Id yake ya sasa.
 
Back
Top Bottom