Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
Maisha halisi ya Gentleman.
1. Gentleman hupendelea kusema ‘tafadhari’ na ‘asante’
2. Gentleman kamwe hawezi kuicheka au kuidharau imani ya wenzake katika dini, siasa, michezo au kitu kingine chochote kile.
3. Gentleman mara kwa mara hubeba handkerchief (Kitambaa kidogo cha jasho) na yuko tayari kumpa mtu mwingine, hasa hasa msichana anayelia na kutokwa na mchozi kwa ajili ya kujifutia.
4. Gentleman kamwe hawezi kuubamiza mlango mbele ya wasichana, wavulana au watu wazima.
5. Gentleman kamwe hawezi kufanya utani juu ya ngozi, jinsia au dini.
6. Gentleman hujua kusimama katika foleni na kusubiri zamu yake ifike.
7. Gentlman mda wote yuko tayari kupeana mikono na watu kwa moyo mmoja.
8. Gentleman mara kwa mara viatu vyake huwa visafi na kucha zak kuziacha safi muda wote.
9. Gentleman huomba msamaha na kukubali kosa mara anapogundua kwamba amefanya kosa.
10. Gentleman huwa apigani au kuchonganisha ugomvi au fujo za aina yoyote ile.
11. Gentleman anajua jinsi ya kuwafanya wengine wajisikie huru.
12. Gentleman anapougua mafua, mara kwa mara hujitenga na wenzake kwa kuogopa kuwaambukiza ugonjwa huo.
GENTLEMAN NA MATUMIZI YAKE YA SIMU
Ingawa simu zimekuwa kila sehemu katika ulimwengu wa sasa, gentleman hujitahidi kutumia simu yake katika tabia nzuri. Anajua kwamba ingawa watu wengi wanafahamu kwamba simu ni lazima zitumiwe, hiyo kwake hawezi kuwafanyia watu karaha kutokana na uwepo wa simu yake katika matumizi yake.
Mara nyingi sana Gentleman anapopokea simu yake huwa haongei kwa sauti ya juu hasa anapokuwa katika sehemu iliyokuwa na mkusanyiko mkubwa wa watu. Hufanya hivi kwa sababu huwa hapendi kuwasumbua watu wengine kwa kelele za suati yake.
Anapokuwa katika kikao cha biashara na mara simu yake inapoita kwa ghafla, mara zote huomba radhi kwa kusema ‘excuse me’ na kisha kuipokea simu hiyo. Huwa hapigi simu yoyote mara anapokuwa katika kikao, na kama akifanya hivyo basi hufanya hivyo kutokana na mada ambayo inazungumziwa mahali hapo na anahijika mtu fulani kutoa maelezo na hayupo hapo.
SEHEMU AMBAZO MARA KWA MARA GENTLEMAN HUTUMIA SIMU YAKE.
* Hutumia simu yake katika kipindi ambacho yupo peke yake.
* Hutumia simu yake katika kipindi ambacho anaona kwamba hakuna mtu karibu yake ambaye
anaweza kumsumbua kutokana na sauti yake.
* Kama ni daktari, basi huiacha simu yake ofisini na kuipokea akiwa kule kule ofisini kwa kuhofia
kuwasumbua wagonjwa na watu wengine.
* Kama ni baba wa familia, mara kwa mara hutumia simu yake kuwasiliana na watoto wake au mfanyakazi wake wa ndani wa nyumbani pamoja na mkewe.
SEHEMU AMBAZO GENTLEMAN HAWEZI KUTUMIA SIMU YAKE.
* Anapokuwa nyuma ya msikani katika kipindi ambacho anaendesha gari au chombo chochote kile.
* Anapokuwa katika ibada, matamasha mbalimbali, sehemu za kuangalia sinema.
* Anapokuwa katika mghahawa.
* Anapokuwa katika chumba ambacho ni maalumu kwa kumsubiri mtu fulani, katika ofisi ya mtu yeyote yule na chumba cha mtihani.
* Anapokuwa katika foleni ya aina yoyote ile ambayo mara kwa mara watu uhitaji utulivu kwa ajili ya kuwasikiliza wahusika.
* Anapokuwa katika lifti, au hadi awe peke yake.
* Anapokuwa katika GYM.
* Anapokuwa katika basi au treni.
* Katika sehemu yoyote ile ambayo imeandikwa kwamba ‘Matumizi ya simu hayaruhusiwi’.
* Gentleman huwa hapigi picha ovyo kwa kutumia simu yake.
* Hawezi kutembea huku akiwa anatuma meseji kwa kutumia simu yake.
Itaendelea kesho.