Jinsi ya kupata ufadhili wa mradi(individual project)

Jinsi ya kupata ufadhili wa mradi(individual project)

vangamwi6

New Member
Joined
Aug 1, 2016
Posts
3
Reaction score
2
habarini wadau! msaada jinsi ya kupata ufadhili wa mradi binafsi katika masuala ya ufugaji, concept note ishaandaliwa ila sijajua naanzia wap kuipeleka.Asanteni
 
Nadhani waone Benki ya wakulima Tz wanaweza kukupa maelekezo zaidi
 
Kama kuna cha maana nimesoma Jamii Forum Mwaka huu ni pamoja na thread hii japo bado watu hawajafunguka zaidi
Mbona yapo mengi tu au huna muda wa kusoma dada yangu?
 
Ingawa fadhili za miradi ya ufugaji ni migumu bado una nafasi ya kufanikiwa wazo lako, unaweza ukajaribu kuintergrate kilimo na ufugaji, maana itakuwa double profit na vyote vinategemeana, lakini kama ukisimamia ufugaji pekee bado utakuwa na changamoto maana uwekezaji wa mifugo bado unaonekana kama suala traditional kwa nchi yetu kwamba kila mtu anaweza kufanya kazi hiyo lakini bila kuzingatia tija. Nakushauri tembelea chama cha wafugaji Tanzania (CCWT) wanaweza kukuunganisha na mashirika ambayo hushirikiana nayo.
 
ningepata jina la agency hiyo nadhan ingekuwa jibu tosha la mradi wangu.
Nafikri atakuwa anamaanisha "African challenge fund" hebu ingia Google utafute hilo jina watakuletea maelezo yote!
 
Nimevutiwa na hii mada
TIB wanatoa hii huduma japo kwa mbinde sana
Siku hizi naona watu wengi wanakimbilia Benki ya Wanawake pale na wanapatiwa mitaji mizuri tu na kama wakikupitisha basi wanakupa hadi wataalamu wa kukuongoza ili ufanikiwe na wao wasipate hasara
 
Mkuu Mimi nahitaji kama m 80 kwa kuweka dhamana yangu but cna mtaji wa kuanza nao naweza kupata
 
Back
Top Bottom