Jinsi ya kumzunguka Dalali

Jinsi ya kumzunguka Dalali

Yaani madalali wamekuwa kero miji mingi Tanzania hasa jiji la Dar, wiki chache zilizopita gazeti moja liliripoti kuwa kuna madalali mpaka ikulu wanaotapeli watu kwa kusema wanawatafutia ajira ofisi ya raisi.

Sasa wewe ukitaka kumzunguka dalali, unaweza sema unataka kiwanja then yeye ataenda kukuonyesha hicho kiwanja na baada ya yeye kukuonyesha hicho kiwanja unamwambia ngoja nikafikirie then ndani ya wiki hii nitakutafuta.

Baada ya hapo we kesho yake unarudi mpaka kwenye kile kiwanja unawauiliza majirani nani ni mmiliki wa hicho kiwanja utaambiwa ni fulani na anaishi wapi na utaomba namba yake ya simu kisha unampigia simu unamueleza shida yako, mtapanga jinsi ya kuonana kisha unafanya manunuzi. Utakaposhangaa ni pale mwenye kiwanja atakwambia kiwanja anauza milioni 8 wakati dalali alikwambia kinauzwa milioni 20.

NB: Tumia ujanja huo au unaofanana na huo na unaweza kuuboresha zaidi katika madalali wa kila aina waotaka pesa za bure kwa kushinda vijiweni

nina ndugu yangU mmojA alifanyA kamA unavyosemA alipelekwA kiwanjanI akapaonA nA kuahDI kuwA atakujA kulipA afteR one week.kesho yake tU akajA akanunuA kiwanjA kwa muhusikA basi wale madalali baadA yA kuckiA kuwA kimeuzwA bacI walimfuatiliziA mpakA nyumbanI kwAKE wakapafam tenA walikujA wenGI nA kwA sharI ,jamaA akawA hanA namnA akawapA fedhA kidogo nA wakaondokA binafsi KiukwelI cwakubalI nawaonA kamA ni dhulmA wakatI mwingne wanapatA helA kumshndA hatA mwenyE malI yakE.
 
Nyumba moja ataonyesha kwa watu hata 20 kwa siku!

Na kila mtu anatoa pesa ya miguu !!!! Dalali akiona kaishiwa pesa ya kunywa pombe anakupeleka kwenye nyumba ambayo tayari keshaweka mpangaji, wakati huyo mpangajia akiwa kazini, mnaishia kuizunguka nyumba na kuingalia kwa nje, mkiaachana baada kupata pesa ya miguu, anakupigia nakukuambia kuwa mwenye nyumba keshaipangisha.
 
Yaani madalali wamekuwa kero miji mingi Tanzania hasa jiji la Dar, wiki chache zilizopita gazeti moja liliripoti kuwa kuna madalali mpaka ikulu wanaotapeli watu kwa kusema wanawatafutia ajira ofisi ya raisi.

Sasa wewe ukitaka kumzunguka dalali, unaweza sema unataka kiwanja then yeye ataenda kukuonyesha hicho kiwanja na baada ya yeye kukuonyesha hicho kiwanja unamwambia ngoja nikafikirie then ndani ya wiki hii nitakutafuta.

Baada ya hapo we kesho yake unarudi mpaka kwenye kile kiwanja unawauiliza majirani nani ni mmiliki wa hicho kiwanja utaambiwa ni fulani na anaishi wapi na utaomba namba yake ya simu kisha unampigia simu unamueleza shida yako, mtapanga jinsi ya kuonana kisha unafanya manunuzi. Utakaposhangaa ni pale mwenye kiwanja atakwambia kiwanja anauza milioni 8 wakati dalali alikwambia kinauzwa milioni 20.

NB: Tumia ujanja huo au unaofanana na huo na unaweza kuuboresha zaidi katika madalali wa kila aina waotaka pesa za bure kwa kushinda vijiweni

Tofautisha udalali na utapeli hata majembe ni madalali
 
Kiukweli hawa jamaa wababoa na kila kukicha wanazidi kuongezeka na kujikita kila mahali. Hata sokoni ukienda mkulima/mfanya biashara hana nafasi ya kuamua bei bali madalali.

Siwapendi na nikishajua na deal na dalali siendelei tena na hiyo biashara.
Najua hata humu wapo, hapo juu nimewasoma na nitaendelea kuwasoma lakini siwapendi. Jitu zima linakaa mjini halifanyi kazi unasubiri mtu ahame uanze kudalalia chumba. Jenga yako.

Kwa kweli mimi natumia kanuni kama yako, nikishajua kuwa kuna dalali kati hata kama kitu nakihitaji sihangaiki tena. Yaani hata kukata ticket ya basi dalali? Kuna maeneo nikitokeaga madalali wanakaa mbali kabisa na huwa nawaambia wasinikaribie.
 
mi ndio ninavyofanya hivi muda mrefu sana nilishangaa kiwanja dalali anasema million 30 wakati mwenye kiwanja anataka million 5 tu nilimalizana naye mwenye kiwanja kila kitu ,
 
Madalali ni muhimu, cha msingi ni kuwa mjanja wa kupima thamani halisi ya unachotaka kununua, kama mimi wakati wa kununua kiwanja changu, nilimuomba dalali nimpe hela yake tuliyokubaliana lakini nibagain na muuzaji kwa bei halisi, hiyo najua kabisa udalali nimelipa kiasi gani
 
Hakuna dalali wa Tanzania unayeweza kumzunguka hivyo, kama huitaki amani fanya hivyo unavyoshauri, kwa sababu uwepo wa dalali unasababishwa na mwenye kitu ambacho kinauzwa au nyumba kupangishwa. Dalali akikuonyesha kiwanja, nyumba, au nyumba ya kupanga ujue wazi amepatana na hao wenye mali hizo na jinsi atakavyolipwa, mara nyingi madalali wanapata cha juu pande zote kwa mwenye kitu na anayehitaji hicho kitu.

Ukiwa na mpango wa kumzunguka dalali ujue wewe na mwenye mali mnajitafutia matatizo na kukosa amani kwa dalali, madalali ni washenzi na hawana utu ukimzunguka tu na ukafanya dili na mwenye mali ujue dalali atawasumbua na utampa tu cha juu chake.

Ukitaka mambo yako yaende sawa kama unatafuta kitu au kununua kitu ni bora umuone moja kwa moja mwenye mali na dalali asihusishwe.
 
Shekifu alikuwa meneja wa RTC Dodoma,mkuu wa mikoa mbalimbali ila ni mweupe sana
 
Unajidanganya tu ndugu hakuna kitu kama hicho dalali hadhulumiwi pesa yake hata siku moja vinginevyo unatafuta vita yani hautokaa kwa amani eneo hilo iwe ni nyumba ya kupanga ay kiwanja kwa sababu dalali mpaka anampeleka mteja eneo la kiwanja jua fika amekabidhiwa na mwenye kiwanja eneo hilo atafute mteja wakiwa katika makubaliano ya ten percent ya mauzo ni hakhi y adalali sasa dalali akupeleje harafu umzunguke ndugu yangu utarogwa utafanyiwa kila visa kwanza unaweza usijenge kabisaaaaaa. Wewe kama unaweza tafuta kiwanja mwenyewe bila dalali uone kama utapata. Msidhalau madalali wana umuhimu mkubwa sana katika jamii hizo hizo kasoro nyingine zinalekebishika kama za kuongeza bei nk endapo tu serikali itaingilia kati katika kusajiri madalali wote wawe wanalipa kodi ili mapato ya serikali yaongezeke
 
Waulize kina prof.Muongo madalali wa vitalu vya gesi na umeme wa mafuta wakuambie umuhimu wao.Tusingechimba gesi Tanzania
 
Mimi sina shida na dalali, tena naona wanasaidia sana kwa kuwa nikishampa mahitaji yangu namuachia kazi yeye na mimi naendelea na shughuli zangu za kila siku bila kupata headache ya namna navyoweza kupata hitaji langu. Tatizo naloliona madalali wetu tofauti na wa nchi zilizoendelea ni kwamba biashara inafanyika kisiri pasipo uwazi kwamba dalali anastahili kupata asimilia ngapi ya mauzo. Utakuta biashara ya kiwanja mwenye eneo kapata asilimia 30 na dalali asilimia 70. Serikali inabidi ilione hili na ilitungie sheria kama hazipo ili iwe wazi kwamba kwa biashara yoyote atakayoifanikisha dalali rasmi aliyesajiliwa atapata asilimia kadhaa. Hii itawaepushia hata hao madalali kuzungukwa baada ya kusota kumuonyesha mtu anachokitaka.
 
Yaani madalali wamekuwa kero miji mingi Tanzania hasa jiji la Dar, wiki chache zilizopita gazeti moja liliripoti kuwa kuna madalali mpaka ikulu wanaotapeli watu kwa kusema wanawatafutia ajira ofisi ya raisi.

Sasa wewe ukitaka kumzunguka dalali, unaweza sema unataka kiwanja then yeye ataenda kukuonyesha hicho kiwanja na baada ya yeye kukuonyesha hicho kiwanja unamwambia ngoja nikafikirie then ndani ya wiki hii nitakutafuta.

Baada ya hapo we kesho yake unarudi mpaka kwenye kile kiwanja unawauiliza majirani nani ni mmiliki wa hicho kiwanja utaambiwa ni fulani na anaishi wapi na utaomba namba yake ya simu kisha unampigia simu unamueleza shida yako, mtapanga jinsi ya kuonana kisha unafanya manunuzi. Utakaposhangaa ni pale mwenye kiwanja atakwambia kiwanja anauza milioni 8 wakati dalali alikwambia kinauzwa milioni 20.

NB: Tumia ujanja huo au unaofanana na huo na unaweza kuuboresha zaidi katika madalali wa kila aina waotaka pesa za bure kwa kushinda vijiweni

Mkuu sio rahisi kama unavyodhani. Kwanza wauzaji wa viwanja,nyumba au wapangishaji huwategemea sana madalali kuwa kama assessors wa wanunuzi/wapangaji. Dalali humhakikishia muuzaji au mpangishaji kuwa mnunuzi/mpangaji sio longolongo na hatamsumbua. Hivyo hata kama utapata bahati ya kupata mawasiliano ya mwenyewe atakuwa na wasiwasi na wewe kwa kuwa hujapitia kwa dalali (unless ana mpango wa kukwepa kumlipa dalali kamisheni yake).

Pili kama ulivyosema hapo kwenye red, hutokea madalali wakamwambia mwenye kiwanja/nyumba kuwa wao wana uwezo wa kutafuta mteja wa bei ya juu kuliko anayotaka muuzaji/mpangishaji, sasa unategemea mwenye mali atakataa hela zaidi?
 
Allah atunusuru na huo mtihani na pia atusamehe
Nimewaza sana nikaona hii haina tofauti saaaan na riba iliyo laaniwa
Yaani ni unyonyaji mkubwa mno...
 
nina ndugu yangU mmojA alifanyA kamA unavyosemA alipelekwA kiwanjanI akapaonA nA kuahDI kuwA atakujA kulipA afteR one week.kesho yake tU akajA akanunuA kiwanjA kwa muhusikA basi wale madalali baadA yA kuckiA kuwA kimeuzwA bacI walimfuatiliziA mpakA nyumbanI kwAKE wakapafam tenA walikujA wenGI nA kwA sharI ,jamaA akawA hanA namnA akawapA fedhA kidogo nA wakaondokA binafsi KiukwelI cwakubalI nawaonA kamA ni dhulmA wakatI mwingne wanapatA helA kumshndA hatA mwenyE malI yakE.

walimuokota wakitaka kujua namna ya trigger inavyofanya kaz waje na kihelele chao
 
Labda kama hicho kiwanja hakijakamatwa na dalali mzoefu. Dalali mzoefu huwezi kumzunguuka kitoto hivyo!..yeye ndio anamiliki kiwanja na mwenye mali anamsikikiza yeye!..mikataba yote anatengeneza dalali na mwenye mali anasikiliza tu! Wewe umekutana na dalali underground

Aisee kazi ipo!
Hawa jamaa wana u giniaz flani hivi wa kuzunguka akili ya mtu si bure!
 
Yaani madalali wamekuwa kero miji mingi Tanzania hasa jiji la Dar, wiki chache zilizopita gazeti moja liliripoti kuwa kuna madalali mpaka ikulu wanaotapeli watu kwa kusema wanawatafutia ajira ofisi ya raisi.

Sasa wewe ukitaka kumzunguka dalali, unaweza sema unataka kiwanja then yeye ataenda kukuonyesha hicho kiwanja na baada ya yeye kukuonyesha hicho kiwanja unamwambia ngoja nikafikirie then ndani ya wiki hii nitakutafuta.

Baada ya hapo we kesho yake unarudi mpaka kwenye kile kiwanja unawauiliza majirani nani ni mmiliki wa hicho kiwanja utaambiwa ni fulani na anaishi wapi na utaomba namba yake ya simu kisha unampigia simu unamueleza shida yako, mtapanga jinsi ya kuonana kisha unafanya manunuzi. Utakaposhangaa ni pale mwenye kiwanja atakwambia kiwanja anauza milioni 8 wakati dalali alikwambia kinauzwa milioni 20.

NB: Tumia ujanja huo au unaofanana na huo na unaweza kuuboresha zaidi katika madalali wa kila aina waotaka pesa za bure kwa kushinda vijiweni

Ushawahi kufanyiwa fujo nyumbani kwako? Fanya hiyo kitu kwa dalali mzoefu alieiona sura yako halafu kwenye hicho kiwanja ujenge ndio utaelewa kuwa madalali si watu wazuri. Ukitaka kumkwepa dalali, tafuta eneo mwenyewe bila kuhusisha mtu.
 
Na sk hz tra inawatambua

Kuna wakati fulani nilinunua kiwanja mahali fulani, kumbe nilitapeliwa, dalali ndie alienisaidia kurudisha pesa zangu baada ya yeye kutonywa na wenzie.
Alitafuta polisi, akawafuata walionitapeli na wakarudisha pesa. Sidhani kama ningezipata hizo pesa kama Nisingemtumia dalali kwa sababu bila yeye sikuwa na pa kuanzia kuwspata walionitapeli.
Dalali ana umuhimu wake, mzunguke ubaki peke yako kwenye biashara unayofanya na usiowajua ndio utaelewa ubaya na uzuri wake.
 
Unajidanganya tu ndugu hakuna kitu kama hicho dalali hadhulumiwi pesa yake hata siku moja vinginevyo unatafuta vita yani hautokaa kwa amani eneo hilo iwe ni nyumba ya kupanga ay kiwanja kwa sababu dalali mpaka anampeleka mteja eneo la kiwanja jua fika amekabidhiwa na mwenye kiwanja eneo hilo atafute mteja wakiwa katika makubaliano ya ten percent ya mauzo ni hakhi y adalali sasa dalali akupeleje harafu umzunguke ndugu yangu utarogwa utafanyiwa kila visa kwanza unaweza usijenge kabisaaaaaa. Wewe kama unaweza tafuta kiwanja mwenyewe bila dalali uone kama utapata. Msidhalau madalali wana umuhimu mkubwa sana katika jamii hizo hizo kasoro nyingine zinalekebishika kama za kuongeza bei nk endapo tu serikali itaingilia kati katika kusajiri madalali wote wawe wanalipa kodi ili mapato ya serikali yaongezeke
Hawana lolote nyie ndio mnalea hawa watu na serekali yetu imekaa kimya hata kodi hawalipi.Ila soon wasipokwenda na maendelea ya kielectronic watu watakuwa wanatumia mitandao kuuza na kununua vitu wao wabaki na miguu.Na kumbuka miaka ya nyuma mpaka kulipia vitu TRA dalali,sijui passport dalali sasa mambo yanaanza kubadilika kidogo kidogo.Mimi last year nilitaka kuuza gari langu wakaniambia mama hili gari bei yake ni milion tano nikawaambia tano siuzi nikaliweka kwenye mtandao nikauza clean seven milion bila dalali
 
Back
Top Bottom