Ndio mkuu. Watoto siku hizi wanaona vitu vya ajabu. Huko huko mapinga same day, ilikuwa jumamosi wakati natoka huko natafuta boda nikapita bar fulani barabarani wakawa wanasema leo ni siku sijui ya vijora kitu kama hicho.Na watoto wanaona. Aisee.
So mimi wakati nina move naelekea waliko boda boda, nikakutana sasa na kigoma kinapigwa kuelekea kwenye hiyo bar, madada hao sasa walivyokuwa wako nusu uchi, wanavyocheza, mara wakae barabarani watikise makalio kama kwenye singeli yani aibu sana.
Na imagine, asilimia kubwa ya waliokuwa wanawafuata nyuma ni watoto wadogo. Na huenda hata wazazi wao walikuwepo ila sidhani kama walikuwa wanashangaa.
Hawa watoto wanaharibika kwenye jamii na tunaona hatuchukui hatua. Watoto wetu wana information kubwa sana ambazo kipindi cha nyuma zilikuwa adimu kwa watoto kuwa nazo au kushuhudia mambo ya namna hiyo.