Fernando sucre
JF-Expert Member
- Jul 14, 2018
- 293
- 344
Wakuu kipindi cha nyuma niliwahi pata binti wa Mbeya nikaishi naye huku nikiwa sijui ndugu yake yoyote.
Kuna kipindi akawa na kama kiburi ukimsemesha anaweza jibu ama la, nikavumilia siku moja asubuhi akakusanya vitu vyake huyo akasepa.
Bila kujua mimi siku hiyo nilipanga nihame hapo.mpango wa kuhama nilishindwa kumwambia coz alishaanza kiburi.
Kumbe jioni alirudi pale akakuta nimehama akanipigia na kuniambia ni mjamzito nikamwambia poa ila kwakua alishabadilika sikutaka kumuambia nilipohamia.
Akawa anapiga akijichekesha ili nimrudie wapi,baada ya miezi kadhaa akaniomba nauli arudi kwao Mbeya nikamtumia.
Akiwa Mbeya akasema kajifungua mtoto anaitwa Bahati wa kike.nikachangia mwanzoni matunzo ya mtoto kule,nikaja kusafiri kwenda nje nikakaa miaka 3 kurudi tigo washauza line yangu,
Nikasajili line nyingine kwa kuwa namba ya mama watoto nilikuwa nayo kichwani nikapiga anapokea mtu mwingine,anasema kauziwa na tigo kucheki jina tpesa kweli jina si la mama watoto.
Sasa kwao sipajui huko mbeya na hata yoyote wa kumpata.nisaidieni mawazo wakuu.
Kuna kipindi akawa na kama kiburi ukimsemesha anaweza jibu ama la, nikavumilia siku moja asubuhi akakusanya vitu vyake huyo akasepa.
Bila kujua mimi siku hiyo nilipanga nihame hapo.mpango wa kuhama nilishindwa kumwambia coz alishaanza kiburi.
Kumbe jioni alirudi pale akakuta nimehama akanipigia na kuniambia ni mjamzito nikamwambia poa ila kwakua alishabadilika sikutaka kumuambia nilipohamia.
Akawa anapiga akijichekesha ili nimrudie wapi,baada ya miezi kadhaa akaniomba nauli arudi kwao Mbeya nikamtumia.
Akiwa Mbeya akasema kajifungua mtoto anaitwa Bahati wa kike.nikachangia mwanzoni matunzo ya mtoto kule,nikaja kusafiri kwenda nje nikakaa miaka 3 kurudi tigo washauza line yangu,
Nikasajili line nyingine kwa kuwa namba ya mama watoto nilikuwa nayo kichwani nikapiga anapokea mtu mwingine,anasema kauziwa na tigo kucheki jina tpesa kweli jina si la mama watoto.
Sasa kwao sipajui huko mbeya na hata yoyote wa kumpata.nisaidieni mawazo wakuu.