PostGE2025 Jinsi Serikali ya Samia inavyotumia damage control kuepuka uwajibikaji

PostGE2025 Jinsi Serikali ya Samia inavyotumia damage control kuepuka uwajibikaji

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

KEKO JUU

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2025
Posts
592
Reaction score
1,835
Damage control ni neno linalotumika kumaanisha juhudi zinazofanywa ili kupunguza madhara, kudhibiti hali mbaya, au kuokoa taswira/nafasi baada ya jambo baya kutokea.

Baada ya mauaji ya halaiki kipindi cha uchafuzi wa Oktoba 29 , serikali ya samuya inatumia mbinu hizi kufanya damage control

Kukataa na Kupunguza Uwezekano wa Mauaji na Ukatili (Denial and Minimization)
Serikali ya Samia imekuwa ikitumia mkakati wa kukataa uwepo wa mauaji au kupunguza idadi yake ili kuepuka kuwajibika. Hii inafanywa ili kutoa picha kwamba matukio ni ya kawaida au yamesababishwa na "maadui wa nchi".

Mfano : Wakati wa hotuba yake ya kuapishwa, Rais Samuya alilaumu "maadui wa nje" (foreign actors) kwa kuwasha ghasia, huku akidai uchaguzi ulikuwa wa haki na uwazi. Hii ilikuwa hatua ya kutoa lawama kwa nje na kutoonyesha kosa la serikali.

Wakati wa ripoti ya CNN kuhusu mauaji baada ya uchaguzi na miili iliyopigwa na polisi, serikali ilitoa taarifa rasmi ikisema inachunguza na kuthibitisha maudhui ya hicho kabla ya kujibu. Hii ilikuwa damage control ya kununua muda bila kukiri au kukataa moja kwa moja, na kutoangalia madai maalum kama makaburi ya pamoja au miili iliyotoweka

BBC: Waziri wa Mambo ya Nje Mahmoud Thabit Kombo alikataa ripoti zilizothibitishwa na picha na video za askari wakipiga risasi kwenye umati, akisema hakuna vifo vilivyothibitishwa, licha ya ushahidi kutoka shirika la haki za binadamu la Kiafrika. Hii ililenga kupunguza shinikizo la kimataifa.

Udhibiti wa Habari na Udanganyifu wa Umma (Censorship and Narrative Control)
Kutoa Takwimu za Kudanganya: Serikali imekuwa ikitoa takwimu za madhara ya mali (kama pikipiki 2,268 zilizoharibiwa) badala ya idadi ya waliouawa, ili kubadilisha mazungumzo kutoka kwa vifo kwenda kwa "hasara za mali". Hii inaonyesha kuwa mali ni muhimu kuliko maisha, na inafaa kwa kutoa lawama kwa waandamanaji kama waharibifu.

Kugeuza mjadala (changing the narrative)
Mfano saiz analeta mjadala wa kuongea na wazee wa mchongo wa dar,ili kuwahadaa watu wasizungumzie kilichotokea kwenye uchafuzi.
Mbinu hizi zote tunazifahamu, sisi sio wahenga wa mi
aka ya tisini
 
Ukweli Mki ingia barabarani mtachezea ilo halihusiani kabisa na Damage control ila ni uhalisia.
Nchi haitaki kwenda kwenye upuuzi wenu wa October 29.
 
Ukweli Mki ingia barabarani mtachezea ilo halihusiani kabisa na Damage control ila ni uhalisia.
Nchi haitaki kwenda kwenye upuuzi wenu wa October 29.
Ila nchi inatulazimisha kutawaliwa kwa shuruti na wasio na ridhaa ya umma? Tuko tayari kufa, mmbaki nyie ambao mkitekwa mtaona sawa, ama kuwekewa viongozi kwenye chaguzi kiinimacho.
 
Ila nchi inatulazimisha kutawaliwa kwa shuruti na wasio na ridhaa ya umma? Tuko tayari kufa, mmbaki nyie ambao mkitekwa mtaona sawa, ama kuwekewa viongozi kwenye chaguzi kiinimacho.
Kama mmeamua kufa kwa mtimdo uo sisi hatuna namna ya kuwazuia kwakua kupanga nikuchagua.
 
Kama mmeamua kufa kwa mtimdo uo sisi hatuna namna ya kuwazuia kwakua kupanga nikuchagua.
Kupanga ni kuchagua ndug yangi. Na kwa waislam wanakwambia "kamaa tadinu tudani" utakavofanya ndio utafanyiwa.
 
Damage control ni neno linalotumika kumaanisha juhudi zinazofanywa ili kupunguza madhara, kudhibiti hali mbaya, au kuokoa taswira/nafasi baada ya jambo baya kutokea.

Baada ya mauaji ya halaiki kipindi cha uchafuzi wa Oktoba 29 , serikali ya samuya inatumia mbinu hizi kufanya damage control

Kukataa na Kupunguza Uwezekano wa Mauaji na Ukatili (Denial and Minimization)
Serikali ya Samia imekuwa ikitumia mkakati wa kukataa uwepo wa mauaji au kupunguza idadi yake ili kuepuka kuwajibika. Hii inafanywa ili kutoa picha kwamba matukio ni ya kawaida au yamesababishwa na "maadui wa nchi".

Mfano : Wakati wa hotuba yake ya kuapishwa, Rais Samuya alilaumu "maadui wa nje" (foreign actors) kwa kuwasha ghasia, huku akidai uchaguzi ulikuwa wa haki na uwazi. Hii ilikuwa hatua ya kutoa lawama kwa nje na kutoonyesha kosa la serikali.

Wakati wa ripoti ya CNN kuhusu mauaji baada ya uchaguzi na miili iliyopigwa na polisi, serikali ilitoa taarifa rasmi ikisema inachunguza na kuthibitisha maudhui ya hicho kabla ya kujibu. Hii ilikuwa damage control ya kununua muda bila kukiri au kukataa moja kwa moja, na kutoangalia madai maalum kama makaburi ya pamoja au miili iliyotoweka

BBC: Waziri wa Mambo ya Nje Mahmoud Thabit Kombo alikataa ripoti zilizothibitishwa na picha na video za askari wakipiga risasi kwenye umati, akisema hakuna vifo vilivyothibitishwa, licha ya ushahidi kutoka shirika la haki za binadamu la Kiafrika. Hii ililenga kupunguza shinikizo la kimataifa.

Udhibiti wa Habari na Udanganyifu wa Umma (Censorship and Narrative Control)
Kutoa Takwimu za Kudanganya: Serikali imekuwa ikitoa takwimu za madhara ya mali (kama pikipiki 2,268 zilizoharibiwa) badala ya idadi ya waliouawa, ili kubadilisha mazungumzo kutoka kwa vifo kwenda kwa "hasara za mali". Hii inaonyesha kuwa mali ni muhimu kuliko maisha, na inafaa kwa kutoa lawama kwa waandamanaji kama waharibifu.

Kugeuza mjadala (changing the narrative)
Mfano saiz analeta mjadala wa kuongea na wazee wa mchongo wa dar,ili kuwahadaa watu wasizungumzie kilichotokea kwenye uchafuzi.
Mbinu hizi zote tunazifahamu, sisi sio wahenga wa mi
aka ya tisini
"Damage control" haiwezi kufanikiwa sana kurekebishwa kuanzia reputation, credibility, public trust na public image vyote vimeharibika.

"Reputation" ni kwamba CCM na serikali yake waonekana ni watu wa hovyo kwa kufanya mauaji ya makusudi kwa wananchi waso na hatia na kujaribu kwa kiasi kikubwa kuficha mauaji hayo, ahsante kwa CNN kudadavua uovu huo.

"Credibilty" imeharibika sana khasa kutokana na maovu yote kuanikwa mbele ya uso wa Dunia. Serikali ya CCM bila haya wa soni ikamtuma balozi wake Ubelgiji kuanza kuandika barua za majibizano na Bunge la Ulaya na Umoja wa Ulaya. Ni vile tu bado uamuzi wa kusimamisha msaada wa fedha wategemea na uamuzi wa mwisho wa Kamisheni ya Ulaya, lakini hiyo itaonyesha ni kwa kiasi gani Umoja wa Ulaya ulivyo na Double Standards kwasababu tu Tanzania ni "strategic Partner", jambo litalozua hoja kwamba Umoja wa Ulaya waunga mkono mauaji ya halaiki.

"Public Image"ndo imekuwa mbaya sana Samia achorwa mapicha inoonyesha macho makubwa yalojaa damu na pembe kichwani. Ameharibu sana taswira yake na haiba yake pia kwamba alionekana mwenye huruma na upendo kumbe ni yule Delilah mwanamke aliemmaliza Samson. Samia ni sawa na Delilah kwenye biblia ambae alimdanganya Samson na kisha akamkata nywele zake na Samson guvu zikaisha.

Hivyo Zanzibar bila muungano na Tanganyika isingekuwa nchi yenye kujitegemea siku zote kwenye kila kitu na ilikuwa ikitegemea Muungano ili ipate manufaa kwa upande wake Lakini baadae Zanzibar imempata Delilah ambae amewarubuni watanganyika na kwenda kuuza rasilimali muhimu kama Bandari na Mbuga za wanyama na mwisho kawaua nguvu zao zote kwa uchaguzi haramu, Bunge haramu na serikali haramu.

"Public trust" ndo imeharibika vibaya mno kiasi cha watu kuanza kuamini watu wengine kama Dr Kitima kwani wasomi hawa ndo pekee wenye uwezo wa kuwatia moyo watanzania ambao kukweli imani na serikali yao imeondoka kwa asilimia 101. Ni hadi hapo serikali ambayo haipo madarakani kihalali itapojiuzulu na kupisha uchaguzi mwingine utaosimamiwa na vyombo vya kimataifa

Hivyo kufanya Damage Control ni moja ya mikakati waloweka kwanza wamemtuma Mwigulu Nchemba awe atoa matamko, pia wakawatuma wale mashekhe, wakamtuma Gerson Msigwa na baadhi ya watu fulanifulani watengeneze "narrative" lakini imebuma.

Lakini serikali bado yashindwa kutambua kwamba haina uhalali wa kuwepo kwasababu wametumia hila kuwepo madarakani kupitia CCM kumpitisha kimagumashi mgombea wake wa uraisi, kupitisha majina ya watu anowataka yeye mgombea uraisi na pia kutumia udanganyifu kwenye zoezi zima la uchaguzi.

Kwahiyo mleta mada, usemapo hii ni "damage control" sidhani kama ni hivyo ila ni kutapatapa na kuhangaika kwao kwani "damage control" hufanywa na serikali ambayo ipo madarakani kihalali na hufanya "damage control" kwa kutoa matamko rasmi ya serikali, ili kurudisha imani kwa wapiga kura ambao waloipigia kura serikali hiyo kweye uchaguzi huru na wenye haki.
 
"Damage control" haiwezi kufanikiwa sana kurekebishwa kuanzia reputation, credibility, public trust na public image vyote vimeharibika.

"Reputation" ni kwamba CCM na serikali yake waonekana ni watu wa hovyo kwa kufanya mauaji ya makusudi kwa wananchi waso na hatia na kujaribu kw akiasi kikubwa kuficha mauaji hayo, ahsante kwa CNN kudadavua uovu huo.

"Credibilty" imeharibika sana khasa kutokana na maovu yote kuanikwa mbele ya uso wa Dunia. Serikali ya CCM bila haya wa soni ikamtuma balozi wake Ubelgiji kuanza kuandika barua za majibizano na Bunge la Ulaya na Umoja wa Ulaya. Ni vile tu bado uamuzi wa kusimamisha msaada wa fedha wategemea na uzmuzi wa mwisho wa Kamisheni ya Ulaya, lakini hiyo itaonyesha ni kwa kiasi gani Umoja wa Ulaya ulivyo na Double Standards kwasababu tu Tanzania ni "strategic Partner", jambo litalozua hoja kwamba Umoja wa Ulaya waunga mkono mauaji ya halaiki.

"Public Image"ndo imekuwa mbaya sana Samia achorwa mapicha inoonyesha macho makubwa yalojaa damu na pembe kichwani. Ameharibu sana taswira yake na haiba yake pia kwamba alionekana mwenye huruma na upendo kumbe ni yule Delilah mwanamke aliemmaliza Samson. Samia ni sawa na Delilah kwenye biblia ambae alimdanganya Samson na kisha akamkata nywele zake na Samson guvu zikaisha.

Hivyo Zanzibar bila muungano na Tanganyika isingekuwa nchi yenye kujitegemea siku zote kwenye kila kitu na ilikuwa ikitegemea Muungano ili ipate manufaa kwa upande wake Lakini baadae Zanzibar imempata Delilah ambae amewarubuni watanganyika na kwenda kuuza rasilimali muhimu kama Bandari na Mbuga za wanyama na mwisho kawaua nguvu zao zote kwa uchaguzi haramu, Bunge haramu na serikali haramu.

"Public trust" ndo imeharibika vibaya mno kiasi cha watu kuanza kuamini watu wengine kama Dr Kitima kwani wasomi hawa ndo pekee wenye uwezo wa kuwatia moyo watanzania ambao kukweli imani na serikali yao imeondoka kwa asilimia 101.
Ni hadi hapo serikali ambayo haipo madarakani kihalai itapojiuzulu na kupisha uchaguzi mwingine utaosimamiwa na vyombo vya kimataifa

Hivyo kufanya Damage Control ni moja ya mikakati waloweka kwanza wamemtuma Mwigulu Nchemba awe atoa matamko, pia wakawatuma wale mashekhe, wakamtuma Gerson Msigwa na baadhi ya watu fulanifulani watengeneze "narrative" lakini imebuma.

Lakini serikali bado yashindwa kutambua kwamba haina uhalali wa kuwepo kwasababu wametumia hila kuwepo madarakani kupitia CCM kumpitisha kimagumashi mgombea wake wa uraisi, kupitisha majina ya watu anowataka yeye mgombea uraisi na pia kutumia udanganyifu kwenye zoezi zima la uchaguzi.

Kwahiyo mleta mada, usemapo hii ni "damage control" sidhani kama ni hivyo ila ni kutapatapa na kuhangaika kwao kwani "damage control" hufanywa na serikali ambayo ipo madarakani kihalali na hufanya "damage control" kwa kutoa matamko rasmi ya serikali, ili kurudisha imani kwa wapiga kura ambao waloipigia kura serikali hiyo kweye uchaguzi huru na wenye haki.
Sahihi 💯💯
 
Back
Top Bottom