Huu ni wakati muhimu kwa vyama vya siasa kujipanga vyema, maana uchaguzi mkuu ni msimu wa mavuno—wakati wa kuuza sera kwa wananchi na kuona matokeo yake. Ukizubaa, umeliwa.
Changamoto ipo kwa CHADEMA na kampeni yao ya "Bila Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi." Kaulimbiu hii ni tamu, inavutia kisiasa, lakini haina uzito wa utekelezaji kwa sababu hakuna mwenye uwezo wa kuzuia uchaguzi nchini. Kuendesha kampeni kama hii ni kujihatarisha kisiasa na kujiweka katika nafasi ya kushindwa bila mapambano.
Lissu anapaswa kujitafakari binafsi na kichama kuhusu mustakabali wa CHADEMA anayokitaka. Ikiwa ataendelea kung'ang'ania msimamo huu, matokeo yatakuwa:
Changamoto ipo kwa CHADEMA na kampeni yao ya "Bila Mabadiliko, Hakuna Uchaguzi." Kaulimbiu hii ni tamu, inavutia kisiasa, lakini haina uzito wa utekelezaji kwa sababu hakuna mwenye uwezo wa kuzuia uchaguzi nchini. Kuendesha kampeni kama hii ni kujihatarisha kisiasa na kujiweka katika nafasi ya kushindwa bila mapambano.
Lissu anapaswa kujitafakari binafsi na kichama kuhusu mustakabali wa CHADEMA anayokitaka. Ikiwa ataendelea kung'ang'ania msimamo huu, matokeo yatakuwa:
- Uchaguzi utafanyika bila kujali msimamo wake, na hatakuwa na uwezo wa kuuzuia.
- Kwa kususia, CHADEMA itapoteza hata jimbo moja walilonalo, na ACT au chama kingine kitapata fursa ya kuwa chama kikuu cha upinzani.
- CHADEMA kitapoteza mvuto, ruzuku itakoma, migogoro itaibuka na kuota mizizi.
- Lissu atakapogundua makosa yake, atakuwa amechelewa kurekebisha mambo.