Mzizi wa Mbuyu
JF-Expert Member
- May 15, 2009
- 7,323
- 6,810
Nimeona ndugu zangu muipate hii, ni stori ya kweli kabisa iliyo wahi kunitokea, japo kuna jina hapa nimelitumia kama langu lakini siyo. Endeleaaah!
Katikati ya miaka ya tisini baada yakumaliza kidato cha sita, nilikuwa naishi na wazee wangu maeneo ya Tegeta jijini Dar es salaam huku nikisubiri kujiunga na chuo kimoja hivi jijini DSM, kuna tukio ambalo lilinifedhehesha sana ingawa ni kama nilijitakia, ndugu zanguni hebu fuatilieni tukio hili.
Nyumbani kwa mjomba wangu maeneo ya Kinondoni kulikuwa shughuli(sherehe) iliyo tukutanisha ndugu wengi hata wale wa mikoani pia walikuja mjini kujumuika na wakawa wanalala palepale kwa mjomba kinondoni.
Nikipindi ambacho, nilikuwa naanza kujua kunywa pombe, na pale zilikuwepo kibao!
Basi bwana, pale jirani na kwa mjomba kulikuwa na dada mmoja hivi mzuri ile mbaya alikuwa anaitwa Suzy,yeye alikuwa amemaliza kidato cha nne hivyo akawa yupo tu nyumbani kwao.Kwasababu ya shughuli ile aliombwa awe analala pale pale kwa mjomba ili kusaidia kazi mbalimbali na kweli akakubaliwa akawa analala pale.
Sasa, unajua tena ujana bwana (labda na safari nilizo zitandika), ilikuwa ni muda mrefu sana toka nilipofanya mchezo ule wa kikubwa mara ya mwisho zile za ujanani ilikuwa niko form five! fikiria hapa nazungumzia habari ya baada ya kumaliza form six!! Lilishakuwa jangwa sasa!! Haukuwa ukame wa kawaida!! Mida ya jioni ilipofika ktk pishana pishana nikaanza kurusha ndogondogo, . Siunajua mie nilikuwa nimemaliza form six yeye form four tuu basi ikawa ndiyo silaha!
English nyiingi you know, eeh if I could do do do, I could be that, then you know, here I am ..yaani akazimia mwenyewe na kulainika maana nilimpigisha shule kali mno!
Ilipofika saa moja hivi usiku nikapata nafasi ya kusimama nae hivi kwenye kagiza ka michongoma, we bwanaawee ujana hatari kwelikweli! Bunduki ilikuwa imekasirika vibaya sana, kidogo ijifyatue! nikambembeleza sana tumalize hata palepale fasta lakini akagoma kabisa, badala yake akanipa mpango huu; Yaani usiku nisiondoke kwenda Tegeta nyumbani nilale pale kwa mjomba, kisha akanielekeza kona anayolala sebuleni pamoja na akina mama wageni waliokuwa wanalala sebuleni. Ilikuwa ni kona ya kulia ukitoka kwenye korido chini ya swtchi za taa na feni, niende nikamuamshe pale watu watapokuwa wamelala, nikaona ni mpango safi kabisa! Moyo ukatulia kidogo lakini ile nguzo ya moto ikwa inaendelea kuwaka huku nikihisi inatoa machozi mepesi kwa hasira!!
Ilipofika muda wa wageni wa hapahapa Dar kuondoka nikapiga chenga hadi ikakubaliwa nilale pale hadi kesho yake asubuhi ndiyo niende nyumbani. Nikaona safi, nikawa hatua moja mbele ya mafanikio.
Ilipofika muda wa kulala mie nililala chumbani na ndugu wengine wa kiume wageni kwa wenyeji, tulijazana mle. Kutokana na ulevi watu hawakuchukua raundi wakapitiwa na usingizi wa pono! Mie kamanda, waapi nilikuwa mkavu safari hii bunduki ikitweta kwa hasira, baada ya kama saa nzima na nusu hivi nikainuka taratibu na kuanza kunyata kuelekea sebuleni ambako kulikuwa kimya kabisa mudahuo .nyatu, nyaat! Nyaaatu!...
Nikafika ile sehemu aliyolala Suzy salama, alikuwa amejifunika shuka nyeupe hivi. Pale mahali palikuwa na kagiza kidogo watu woote mle walikuwa wamelala, nadhani ilkuwa ni fofofo. Nikainama, pale kwenye kona tu kutoka kwenye korido nikampigapiga tarrriibu Suzy kwenye bega,..alishtuka kidogo lakini akaendelea kulala. Nikabadilisha mwelekeo nikampapasa kwenye makalio tarratiibuuu huku niki sema Ssssssuuuzzzyhhh.. (yaani kwa sauti ya chini iliyoelekea kwenye sikio lake moja kwa moja) huku upigaji wa kiwowo chake ukiendelea ila safari hii nikijitaja jina .ni mimi Masanilo, Masnilooo, Massssannn! Sssuuu twende basi! Nikapiga kwa nguvu zaidi baada ya kuona hastuki.
Hapa ndipo ulipo nikuta mkasa, kwasababu aliinuka ghafla na kuwasha taa.. Dah! Hakuwa Suzy bwana alikuwa shangazi yangu mke wa mjomba! Akasema pumbavvv kumbe ndiyo michezo yenu hii! Yaani wewe una . Hakumalizia, wala sikumsubiri amalizie . Nikachomoka kwa spidi ya ajabu! badala ya kutokea mlango wa jikoni, nikatokea palepale kwenye mlango wa sebule na kwa mwendo wa kutembelea vidole gumba vya miguu, amini usiamini walikuwa watu lundo lakini sikumkanyaga wala kugusa mtu! Nahapo ndipo nilipogundua kuwa kumbe ile nguzo kuu haina lolote mbele ya hofu, maana ilanguka ghafla na kwa kishindo tuu!! (Nikaisikia ikipiga kwenye paja langu la kulia inakopenda kulalia!) Kwisha! Ikawa nguzo ya Uji!
Basi bwana kwa mjomba hakukulalika tena, nikaanza kuhangaika kutafuta mahala pa kulala maana ilikuwa usiku sana, nisingeweza kufika Tegeta usafiri haukuwepo!
Nisiwachoshe wapendwa, nilikuja gundua baadae kuwa kumbe mke wa mjomba usiku ule akaona ni vema akalala na kina mama wageni pale sebuleni na akachagua ile sehemu ya Suzy kwasababu ilkuwa rahisi kutoka kwenda chumbani sasa akawa amemhamisha Suzy pale, agh! Nae Suzy kumbe alikuwa amepanga kutolala ili nikitokea tu kwenye kona aamke anifuate, lakini du! Akapitiwa eti na usingizi!!
Nasikia kina mama waliamshwa wakapewa kisa kizima, ! Mjomba alipoambiwa alicheka ssanaa! Na mengine meengi yakasemwa. Yaani niacheni tu jamani niliona soni kweli!
Jina la Masanilo siyo halisi nimelitumia tu ili story ieleweke sawasawa.
Katikati ya miaka ya tisini baada yakumaliza kidato cha sita, nilikuwa naishi na wazee wangu maeneo ya Tegeta jijini Dar es salaam huku nikisubiri kujiunga na chuo kimoja hivi jijini DSM, kuna tukio ambalo lilinifedhehesha sana ingawa ni kama nilijitakia, ndugu zanguni hebu fuatilieni tukio hili.
Nyumbani kwa mjomba wangu maeneo ya Kinondoni kulikuwa shughuli(sherehe) iliyo tukutanisha ndugu wengi hata wale wa mikoani pia walikuja mjini kujumuika na wakawa wanalala palepale kwa mjomba kinondoni.
Nikipindi ambacho, nilikuwa naanza kujua kunywa pombe, na pale zilikuwepo kibao!
Basi bwana, pale jirani na kwa mjomba kulikuwa na dada mmoja hivi mzuri ile mbaya alikuwa anaitwa Suzy,yeye alikuwa amemaliza kidato cha nne hivyo akawa yupo tu nyumbani kwao.Kwasababu ya shughuli ile aliombwa awe analala pale pale kwa mjomba ili kusaidia kazi mbalimbali na kweli akakubaliwa akawa analala pale.
Sasa, unajua tena ujana bwana (labda na safari nilizo zitandika), ilikuwa ni muda mrefu sana toka nilipofanya mchezo ule wa kikubwa mara ya mwisho zile za ujanani ilikuwa niko form five! fikiria hapa nazungumzia habari ya baada ya kumaliza form six!! Lilishakuwa jangwa sasa!! Haukuwa ukame wa kawaida!! Mida ya jioni ilipofika ktk pishana pishana nikaanza kurusha ndogondogo, . Siunajua mie nilikuwa nimemaliza form six yeye form four tuu basi ikawa ndiyo silaha!
English nyiingi you know, eeh if I could do do do, I could be that, then you know, here I am ..yaani akazimia mwenyewe na kulainika maana nilimpigisha shule kali mno!
Ilipofika saa moja hivi usiku nikapata nafasi ya kusimama nae hivi kwenye kagiza ka michongoma, we bwanaawee ujana hatari kwelikweli! Bunduki ilikuwa imekasirika vibaya sana, kidogo ijifyatue! nikambembeleza sana tumalize hata palepale fasta lakini akagoma kabisa, badala yake akanipa mpango huu; Yaani usiku nisiondoke kwenda Tegeta nyumbani nilale pale kwa mjomba, kisha akanielekeza kona anayolala sebuleni pamoja na akina mama wageni waliokuwa wanalala sebuleni. Ilikuwa ni kona ya kulia ukitoka kwenye korido chini ya swtchi za taa na feni, niende nikamuamshe pale watu watapokuwa wamelala, nikaona ni mpango safi kabisa! Moyo ukatulia kidogo lakini ile nguzo ya moto ikwa inaendelea kuwaka huku nikihisi inatoa machozi mepesi kwa hasira!!
Ilipofika muda wa wageni wa hapahapa Dar kuondoka nikapiga chenga hadi ikakubaliwa nilale pale hadi kesho yake asubuhi ndiyo niende nyumbani. Nikaona safi, nikawa hatua moja mbele ya mafanikio.
Ilipofika muda wa kulala mie nililala chumbani na ndugu wengine wa kiume wageni kwa wenyeji, tulijazana mle. Kutokana na ulevi watu hawakuchukua raundi wakapitiwa na usingizi wa pono! Mie kamanda, waapi nilikuwa mkavu safari hii bunduki ikitweta kwa hasira, baada ya kama saa nzima na nusu hivi nikainuka taratibu na kuanza kunyata kuelekea sebuleni ambako kulikuwa kimya kabisa mudahuo .nyatu, nyaat! Nyaaatu!...
Nikafika ile sehemu aliyolala Suzy salama, alikuwa amejifunika shuka nyeupe hivi. Pale mahali palikuwa na kagiza kidogo watu woote mle walikuwa wamelala, nadhani ilkuwa ni fofofo. Nikainama, pale kwenye kona tu kutoka kwenye korido nikampigapiga tarrriibu Suzy kwenye bega,..alishtuka kidogo lakini akaendelea kulala. Nikabadilisha mwelekeo nikampapasa kwenye makalio tarratiibuuu huku niki sema Ssssssuuuzzzyhhh.. (yaani kwa sauti ya chini iliyoelekea kwenye sikio lake moja kwa moja) huku upigaji wa kiwowo chake ukiendelea ila safari hii nikijitaja jina .ni mimi Masanilo, Masnilooo, Massssannn! Sssuuu twende basi! Nikapiga kwa nguvu zaidi baada ya kuona hastuki.
Hapa ndipo ulipo nikuta mkasa, kwasababu aliinuka ghafla na kuwasha taa.. Dah! Hakuwa Suzy bwana alikuwa shangazi yangu mke wa mjomba! Akasema pumbavvv kumbe ndiyo michezo yenu hii! Yaani wewe una . Hakumalizia, wala sikumsubiri amalizie . Nikachomoka kwa spidi ya ajabu! badala ya kutokea mlango wa jikoni, nikatokea palepale kwenye mlango wa sebule na kwa mwendo wa kutembelea vidole gumba vya miguu, amini usiamini walikuwa watu lundo lakini sikumkanyaga wala kugusa mtu! Nahapo ndipo nilipogundua kuwa kumbe ile nguzo kuu haina lolote mbele ya hofu, maana ilanguka ghafla na kwa kishindo tuu!! (Nikaisikia ikipiga kwenye paja langu la kulia inakopenda kulalia!) Kwisha! Ikawa nguzo ya Uji!
Basi bwana kwa mjomba hakukulalika tena, nikaanza kuhangaika kutafuta mahala pa kulala maana ilikuwa usiku sana, nisingeweza kufika Tegeta usafiri haukuwepo!
Nisiwachoshe wapendwa, nilikuja gundua baadae kuwa kumbe mke wa mjomba usiku ule akaona ni vema akalala na kina mama wageni pale sebuleni na akachagua ile sehemu ya Suzy kwasababu ilkuwa rahisi kutoka kwenda chumbani sasa akawa amemhamisha Suzy pale, agh! Nae Suzy kumbe alikuwa amepanga kutolala ili nikitokea tu kwenye kona aamke anifuate, lakini du! Akapitiwa eti na usingizi!!
Nasikia kina mama waliamshwa wakapewa kisa kizima, ! Mjomba alipoambiwa alicheka ssanaa! Na mengine meengi yakasemwa. Yaani niacheni tu jamani niliona soni kweli!
Jina la Masanilo siyo halisi nimelitumia tu ili story ieleweke sawasawa.