Ukiona umedoda ujue hakuna anaye upa kipau mbeleHapa tunatoa elimu sio kudoda. Baada ya hapa nitaleta sheria za Police
Anyway me cku hizi sibishani mabishano hayamake $. So with u am done.Soma vizuri ndugu maandishi yanaonekana usilazimisha maana tofauti na hapo.
shida yangu sio sheria ya maandamano kaka.nataka kujua kuhusu sheria inayosimamia vyama vyenye usajili wa kudumu.Rudia kusoma vizuri kabisa. Halafu baada ya hapo nitakuletea Sheria ya maandamano.
Ungemshauri kwanza pombe ungekua mtu wa maana sanaKatiba ni kwaajiri ya watanzania.
unaongea vitu ambavyo hata havihusiani na maandamano, inainekana upo mtupu sana kichwani.Katiba ni kwaajiri ya watanzania.
Madaraka ya Pekee ya Mamlaka ya Nchi
31.-(1) Mbali na masharti ya ibara ya 30(2), sheria yoyote
iliyotungwa na Bunge haitakuwa haramu kwa sababu tu kwamba
inawezesha hatua kuchukuliwa wakati wa hali ya hatari, au
wakati wa hali ya kawaida kwa watu wanaoaminika kuwa
wanafanya vitendo vinavyohatarisha au kudhuru usalama wa
taifa, ambazo zinakiuka masharti ya ibara ya 14 na ya 15 za
Katiba hii.
(2) Ni marufuku kwa hatua zilizotajwa katika ibara ndogo ya
(1) ya ibara hii kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria yoyote wakati
wa hali ya hatari, au wakati wa hali ya kawaida kwa mtu yeyote,
isipokuwa tu kwa kiasi ambacho ni lazima na halali kwa ajili ya
kushughulikia hali iliyopo wakati wa hali ya hatari au wakati wa
hali ya kawaida kushughulikia hali iliyosababishwa na mwenendo
wa mtu anayehusika.
(3) Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika ibara hii
hayataidhinisha mtu kunyang'anywa haki yake ya kuwa hai
isipokuwa tu kwa kifo kama matokeo ya vitendo vya kivita.
Hiyo hiyo ibara ya 30:
(4) Bila ya kuathiri masharti mengineyo yaliyomo katika
Katiba hii, Mahakama Kuu itakuwa na mamlaka ya kusikiliza kwa
mara ya kwanza na kuamua shauri lolote lililoletwa mbele yake
kwa kufuata ibara hii; na Mamlaka ya Nchi yaweza kuweka
sheria kwa ajili ya-
(a) kusimamia utaratibu wa kufungua mashauri kwa
mujibu wa ibara hii;
(b) kufafanua uwezo wa Mahakama Kuu katika kusikiliza
mashauri yaliyofunguliwa chini ya ibara hii;
(c) kuhakikisha utekelezaji bora wa madaraka ya
Mahakama Kuu, hifadhi na kutilia nguvu haki, uhuru
na wajibu kwa mujibu wa Katiba hii.
(5) Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria
yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au
mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu
muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na
Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria au hatua inayohusika,
kwa kiwango inachopingana na Katiba ni batili au kinyume cha
Katiba basi Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi
ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua
hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili
ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha
hitilafu iliyopo katika sheria inayotuhumiwa au hatua inayohusika
katika muda na kwa jinsi itakavyotajwa na Mahakama Kuu, na
sheria hiyo au hatua inayohusika itaendelea kuhesabiwa kuwa ni
halali hadi ama marekebisho yatakapofanywa au muda
uliowekwa na Mahakama Kuu utakapokwisha, mradi muda mfupi
zaidi ndio uzingatiwe.
Soma ibara 30
Mamlaka ya Rais
Nasikitika kuona jinsi unavyowagaragaza vijana wa UKUTA kwa kutumia vifungu vya KATIBA..!Mamlaka ya Rais
148.-(1) Bila ya kuathiri masharti yatakayowekwa na sheria
yoyote iliyotungwa na Bunge, miongoni mwa madaraka ya Rais
akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu ni kuyaamuru majeshi ya nchi
yatende mambo yanayohusika na vita vya ulinzi wa Jamhuri ya
Muungano, mambo ya kuokoa maisha na mali ya watu katika
hali ya hatari na mambo mengineyo ambayo Amiri Jeshi Mkuu
ataona yahitajika, na kwa ajili hiyo Amiri Jeshi Mkuu aweza
kuyaamuru hayo majeshi yatende mambo hayo ama ndani au
nje ya Tanzania.
Madaraka ya Pekee ya Mamlaka ya Nchi
31.-(1) Mbali na masharti ya ibara ya 30(2), sheria yoyote
iliyotungwa na Bunge haitakuwa haramu kwa sababu tu kwamba
inawezesha hatua kuchukuliwa wakati wa hali ya hatari, au
wakati wa hali ya kawaida kwa watu wanaoaminika kuwa
wanafanya vitendo vinavyohatarisha au kudhuru usalama wa
taifa, ambazo zinakiuka masharti ya ibara ya 14 na ya 15 za
Katiba hii.
(2) Ni marufuku kwa hatua zilizotajwa katika ibara ndogo ya
(1) ya ibara hii kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria yoyote wakati
wa hali ya hatari, au wakati wa hali ya kawaida kwa mtu yeyote,
isipokuwa tu kwa kiasi ambacho ni lazima na halali kwa ajili ya
kushughulikia hali iliyopo wakati wa hali ya hatari au wakati wa
hali ya kawaida kushughulikia hali iliyosababishwa na mwenendo
wa mtu anayehusika.
(3) Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika ibara hii
hayataidhinisha mtu kunyang'anywa haki yake ya kuwa hai
isipokuwa tu kwa kifo kama matokeo ya vitendo vya kivita.
Katiba inasomwa na kutafsiriwa kisheria sio kama unatafsiri vipimo vya kutengeneza madawati.Safi sana
CDM wana tumia umbumbumbu wa wanachama wao
Kuwa danganya.
Nakuambia hawa hawana nafasi tena
Wana tapatapa,
Hoja ya Ufisadi imewapoteza hawana
Muelekeo tena