Jina la Benki hii lipi?

Kamaanisha ktk neno CRDB BANK neno bank limetajwa Mara 2 hapo kama ukirefusha hill CRDB na kuweka neno la mwisho BA.NK
Ni kutojua matumizi ya initials kwenye logo ndo maana unafananisha CRDB Bank na Barabara ya Nyerere road. CRDB hapa B haijitoshelezi ikisimama pekee kuitwa Bank. Hapa CRDB inesimama kama logo na logo hiyo haijakamilika bila hiyo mistari na neno Bank. Angeandika 'Cooperative and Rural Development Bank Bank' kwa maneno ndo lingekuwa kosa. Kuna initials ambazo huwa neno kamili na hapa CRDB Bank imechukua muundo wa neno hilo
 
Inaitwa CRDB Bank PLC baada ya kustrasform kutoka kwenye mikono ya serikari na kuwa Private company sasa CRDB imebaki Kama jina la company na usilefushe wewe sema CRDB Bank PLC
 
Kwa vyovyote hujaelewa ninachotaka kukifahamu. Cooperative Rural Development Bank ni CRDB lakini pana maandishi mengine ya "Bank" ndio maana nikasema Tazama Logo!
Yaan ndo yaleyale ya kusema nimepita "barabara ya Kilwa Road"

Tumeelewana.!
 
Jina crdb bank plc ,kirefu cha crdb kilishaachwa kutumika.
 
Haina kirefu ni CRDB Bank
 
Ukirefusha CRDB Bank neno Bank la pili litakosa maana.
CRDB haina kirefu, ni neno moja kama ilivyo mama, mtu, azam, n,k. Baada ya kubinafsishwa mwaka 1996, bank ilibadili jina kutoka Cooperative Rural Development Bank na kuwa CRDB Ltd na baadaye 1999 ikawa CRDB Bank Ltd. Mwaka 2009 ilipojiunga na soko la hisa DSE ikawa CRDB Bank PLC.
 
CRDB ni sawa na wewe ukiamua jina lako kuwa initials za majina yako na kwenda kuapa mahakamani au kwa mwanasheria - deed poll.
 
Cooperative Rural Development Bank. Bank!!
 

Wakurupukaji hawatakuelewa
 
Zamani hilo jina ndio lilikuwa na kirefu chake, but baada ya kuuzwa kwa wawekezaji wao waliamua kuuiita CRDB Bank lakini hawakutoa kirefu chake. Hivyo basi CRDB ndio jina la benki.
 
Asee aliyeleta uzi huu nadhani amelala.... NMB Bank.. NBC Bank.., BOA Bank... DTB Bank... Ni hivi pale tunapotumia UFUPISHO WAKE LZMA TUWEKE KITU BANK ILI KUELEZEA KUWA HICHO KILICHOFUPISHA NI BANK FULANI.... Kwa mfano BOA.. yaweza itwa BARRIERS OF AUDITING (BOA)... So wanaweka hiyo ili kufafanua zaidi juu jina tajwa hapo..
 
Inaitwa CRDB Bank PLC baada ya kustrasform kutoka kwenye mikono ya serikari na kuwa Private company sasa CRDB imebaki Kama jina la company na usilefushe wewe sema CRDB Bank PLC
PLC means Public Limited Company... not private... ikiwa prvte huitwa Only limited (LTD)
 
Chama Cha CCM. Kuwa serious basi ndugu.
 
Kwa sasa hakuna kirefu chake inaitwa CRDB BANK ndio brand name kwa sasa
 
Ndiyo majanga ya CCM usinikumbushe Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini.

Sasa ni benki ya wana hisa sisi Vijijini hatuna uwezo wa kununua hizo hisa wala benki yenyewe haituamini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…