Jimbo la Spika lawaka moto!

Nawaza kwa jinsi Bunge lilivyoendeshwa atleast kidemokrasia msimu huu hata kama ni ni kwa 0.5% democracy, ni hatua kwa Tanzania.Kwa miaka yangu michache niliyoishi na kulitazama Bunge,nimefurahia sana Sitta alivyothubutu kuruhusu baadhi ya mambo kujadiliwa live bungeni, Sikatai baadhi ya madhaifu yake ila nawaza kama Sitta atangolewa basi nani atamrithi. Generally alijaribu hata kama alikua ana agenda ya siri.

Anna Makinda au Sofia Simba
 
Kama watamchagua huyu basi wa urambo wamekwisha. Yaani kwake kipaumbele ni vyombo vya usafiri. Watanzania ( sio wa Urambo mashariki tu ) tuwe serious na matatizo yanayotukabili watu wanaokaa mjini na kututembelea kila baada ya miaka mitano hawajui shida zetu.

Anadhani tutakula chombo cha usafiri, tukiumwa chombo cha usafiri kitasaidia.


NN,
Nilitegemea Bw. Maswanya awaeleze mikakati yake ya kuwapigania wana jimbo kuwatoa ktk lindi la matatizo!! Binafsi nimefika Urambo; hali bado ni tata. Mimi sidhani kama kweli huyu ni mtu atakaye wasidia...

Aje na mipango ya kweli ya kuwkomboa wana Urambo. Hata hivyo, nakutakia kila la kheli bwana Mswanya.:cool:
 
Unataka ushahidi gani Mkuu wakati kila kitu kipo wazi? kaka kuwa targeted si lazima bastola iwe sikioni - ni matendo tu anayofanyiwa huyu kamanda kweli yanaashiria mwisho wa Sitta CCM. na hata akin'gan'gania kubakia humo bado atakuwa na misukosuko mingi sana kuelekea uchaguzi mkuu.

Kitendo cha UVCCM kukabidhiwa majimbo yote ya hawa wapiganaji kuhakikisha yanachukuliwa na wao ni kitendo tosha kwamba wameshawachoka.

Mtera - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Urambo - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Nzega - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Simanjiro - Jimbo limekabidhiwa kwa UVCCM nk

UVCCM watapata kila support kutoka makao makuu kuhakikisha list hii hapa chini hairudi bungeni kwa tiketi ya CCM

Kwa hiyo, Sintashangaa kutowaona Malecela, Selelii, Sitta, Sendeka, Mwakyembe, Sherukindo, Shibuda kwenye bunge lijalo - ni vizuri tu waanze kujipanga mapema kukabiliana na vita hii ndani ya CCM.
ELNINO unaripoti unayoyasikia ndani ya CCM au ni mawazo yako kwamba watu hao wamechoka kuna tofauti kati ya kusikia na mawazo yako kama ni mawazo yako what is wrong with these guys
 
Tunahitaji vijana zaidi. One of these days Sitta atafukuzwa na kunyang'anywa kadi ya CCM. Lets wait and see...Kwa tabia yake ya kuzungumzia mambo yao ya ndani yaliyotokea kwenye vikao vyao kwenye hadharani, na kwa CCM ninaifahamu nadhani watachukua jukumu la kumwadabisha huyo mzee. Hivyo inabidi aangalie mambo katika kona zote!!!!!!
Unaweza toa sababu kwa nini t/unahitaji vijana na si wazee au ndiyo chorus ya kileo kwamba t/unadhani kijana yeyote lazima atakuwa na uwezo wa uongozi
 
Binafsi namfahamu Bwana Maswanya na ni kijana mzuri. Lakini linalonijia kichwani ni kwamba hivi alisubiri mpaka awe kamanda ndiyo awakumbuke wana Urambo? Amekuwa mtumishi wa Zain na kabla ya hapo Celtel na TTCL kwa muda mrefu na shida za wana Urambo, hazikuanza leo. Hii timing haitoi hitimisho lolote zaidi ya kuwa amesukumwa na hoja ya kisiasa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu. Mimi naamini wana Urambo wanaijua hii style ya watu kusimikwa ukamanda ili wajijengee uhalali wa kupita jimboni na kumimina ahadi na hata kuhujumu incumbents. Lakini je, kama Maswanya ni mwenyeji wa Urambo na mwenye mapenzi, alisubiri nini miaka yote hii asizione kero za urambo (usafiri siyo kero ya kipaumbele) hadi miezi michache kabla ya mchakato? Hii ni dhihaka na ana kazi ngumu kujiondoa kwenye tuhuma za kutumiwa na wale wanaodaiwa ni maadui wa Mzee Sitta. Hata Rungwe imeotkea hivyo hivyo kwamba aliyepewa ukamanda wa UVCCM Mkoa wa Mbeya ndiye hivi sasa amepewa rungu la kujaribu kumng'oa Prof. Mwandosya. Hakika bunge lijalo si la wananchi, ni la watu wanaowawakilisha vigogo wenye nazo.

Kila la heri swahiba yangu Maswanya lakini unajaribu kukata mbuyu na wewe una wembe, utaweza?
 
Akufukuzae hakwambii toka, Sitta muda wako wa kukaa CCM umeshakwisha...your targeted...
Siyo CCM tuu
Huu ni wakati wa kuwaachia vijana ambao wanaweza kuchemka na changa moto zinatukabili mikoani vinginevyo watanyakua na kuwaach wazee kama hawa kuaibika.
Huu siyo wakati wa kuoneana haya 'You can't train old dog new trick'
 
Unataka ushahidi gani Mkuu wakati kila kitu kipo wazi? kaka kuwa targeted si lazima bastola iwe sikioni - ni matendo tu anayofanyiwa huyu kamanda kweli yanaashiria mwisho wa Sitta CCM. na hata akin'gan'gania kubakia humo bado atakuwa na misukosuko mingi sana kuelekea uchaguzi mkuu.

Kitendo cha UVCCM kukabidhiwa majimbo yote ya hawa wapiganaji kuhakikisha yanachukuliwa na wao ni kitendo tosha kwamba wameshawachoka.

Mtera - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Urambo - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Nzega - Jimbo limekabidhiwa wa UVCCM
Simanjiro - Jimbo limekabidhiwa kwa UVCCM nk

UVCCM watapata kila support kutoka makao makuu kuhakikisha list hii hapa chini hairudi bungeni kwa tiketi ya CCM

Kwa hiyo, Sintashangaa kutowaona Malecela, Selelii, Sitta, Sendeka, Mwakyembe, Sherukindo, Shibuda kwenye bunge lijalo - ni vizuri tu waanze kujipanga mapema kukabiliana na vita hii ndani ya CCM.

I am still not convinced na hiyo uliyoweka hapo, naona ni hisia zako tu zinakutuma hivyo kutokana na vuguvugu lililopo, la sivyo ungesema ilala, kinondoni, kyela, Ukerewe, kondoa kusini, dodoma mjini, nk.

CCM has alot of democracy to share this year within the party na si kwasababu watu wamechokwa au majimbo wamepewa UVCCM

Unataka kuniambia CCM wamekaa na kukubaliana UVCCM wapewe less than 10 majimbos?? hell No!!!

Just get your facts right and acknowledge pale ambapo unaspeculate ili tuwe vyema
 
ELNINO unaripoti unayoyasikia ndani ya CCM au ni mawazo yako kwamba watu hao wamechoka kuna tofauti kati ya kusikia na mawazo yako kama ni mawazo yako what is wrong with these guys

bana eh!!!
 
Uongozi ni kupokezana kila mmoja anajaribu. Kwakuwa kila mtu anahaki ya kugombea mie sioni shida kuwa na Wagombea wengi. Tumwache naye ajaribu japo hatujui kipya alichonacho. Hizo ahadi tu zimeshanipa wasiwasi juu yake.

Gofu Zulu
 
Nchi hii ushabiki umezidi, mara nyingine watu hata hawajui wanashabikia nini? Sijui ni kwa sababu hatuna mafanikio ya kushangilia? Sasa huyu kuwaahidi vijana usafiri ana maana gani? Halafu haya mawazo ya mtu kutaka uongozi kwa kusema atanunua hiki kwa fedha zake, ni lazima aulizwe anazipata wapi?
...ushabiki mwingi wa namna hii una element za uislamu!!!
 
Jimbo la Urambo leo lilizima kwa maandamano makubwa ya kumpokea kamanda mteule Bwana Ally Maswanya ambaye ni kurugenzi wa kampuni ya Zain kanda ya Ziwa, maandamano hayo yalikuwa na lengo la kumsimika u-kamanda bwana maswanya ambaye pia anatajwa kulinyemelea jimbo hilo.
Maandamano hayo yaliyotanguliwa na msafara wa pikipiki karibu 70 na tax 50 zilizofuatiwa na magari ya kifahari karibu 30. hata hivyo katika hali ya kushangaza Bwana Spika aligoma kuhudhuria sherehe hizo zilifanyika mbele ya jengo la ccm wilaya ya Urambo, habari zaidi zinasema mgeni rasmi katika sherehe hizo alikuwa bwana Edwin sanda (MNEC Uvccm) ambaye alimwakilisha katibu mkuu Uvccm Martin Shigela aliyetakiwa kuwa mgeni rasmi.
akihutubia wananchi wa Urambo Bwana Maswanya ambaye kwa umri bado anaonekana kijana aliwaahidi vijana wa Urambo kuwapatia vyombo vya usafiri baada ya kuona kuwa vijana hao wamekosa mtu wa kuwajali kwa kipindi kirefu

Hivi huu moto umeshaunguza nyumba au vipi?
 
Jimbo la Urambo leo lilizima kwa maandamano makubwa ya kumpokea kamanda mteule Bwana Ally Maswanya ambaye ni kurugenzi wa kampuni ya Zain kanda ya Ziwa, maandamano hayo yalikuwa na lengo la kumsimika u-kamanda bwana maswanya ambaye pia anatajwa kulinyemelea jimbo hilo.
Maandamano hayo yaliyotanguliwa na msafara wa pikipiki karibu 70 na tax 50 zilizofuatiwa na magari ya kifahari karibu 30. hata hivyo katika hali ya kushangaza Bwana Spika aligoma kuhudhuria sherehe hizo zilifanyika mbele ya jengo la ccm wilaya ya Urambo, habari zaidi zinasema mgeni rasmi katika sherehe hizo alikuwa bwana Edwin sanda (MNEC Uvccm) ambaye alimwakilisha katibu mkuu Uvccm Martin Shigela aliyetakiwa kuwa mgeni rasmi.
akihutubia wananchi wa Urambo Bwana Maswanya ambaye kwa umri bado anaonekana kijana aliwaahidi vijana wa Urambo kuwapatia vyombo vya usafiri baada ya kuona kuwa vijana hao wamekosa mtu wa kuwajali kwa kipindi kirefu

vyombo gani vya usafiri? piki piki? hapo anawaua vifua tu. tax 50 urambo zilitoka wapi? au Urambo huijui wewe!!!!!!!! utakuwa mmoja wao au wamekutuma
 
Jamani someni alama za nyakati.
Huko nyuma niliwahi kuwaambia kuwa kulia lia ya mzee ni uoga wa kukubali ukweli kuwa amepauka huko kwao wengi mlinibeza na kunibandika majina.
Nyinyi watu ambao mko dar kuna wengine wanajifanya wanaelewa sana na kwamba unapowaambia ukweli halisi basi waanza "this country bwana......"
Mimi nimekuwa nikipita jimbo hili mara kwa mara na tabia niliojijengea ni kuwa nikifika ugenini hufunga mdomo na kuyaweka masikio yangu mkao wa kusikiliza tu na unapoona kuwa wengi huzungumzia kitu kimoja basi ni dhahir kuwa hiyo ni hali halisi.
Tutawaita wajinga na majina mengi lakini ukweli ni kuwa wao ndiyo wenye uwezo wa kuamua [siyo wajinga kama mnavyofikiri].
Mzee kupita urambo safari hii itakuwa moja ya miujiza ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom