Jimbo la Magu, Mwanza

Jimbo la Magu, Mwanza

kuleha1

Member
Joined
May 8, 2013
Posts
51
Reaction score
8
TAARIFA KWA UMMA WA MAGU;

Tujiulize mbunge wetu mh.Dr. Limbu kaenda bungeni kutuwakirisha kua hata sisi jimbo letu haliko wazi!au ameenda bungeni kutusemea matatizo yetu kwa serikali ili itutatulie, Nimeaza na maswali manake kunamatatizo mengi sana na ahadi zake hakuna hata moja aliyotekeleza mfano alisema atapeleka umeme toka magu mjini hadi mahaha kupitia Ng'haya,Kabila,Shishani mpaka Mahaha lakin hata dlili hakuna,ataleta maji toka Ziwa Victoria na kusambaza kwenye vijiji mpaka sasa hakuna,atachangia jitihada ya ujenzi wa secondary Mahaha,
hajatoa mchango wowote,ujenzi wa barabara ktk kiwango cha ubora,lakini hajuna,ataboresha hospital ya Magu Mjini,Kabila na Mahaha,hiyo ilikua ni danganya toto ya watu wa Magu,ataboresha soko na minada ya Magu Mjini,Ng'haya Kabila na Maha lakini hilo limekua ndoto za mchana.

JE, WANAINCHI WEZANGU WAZALENDO MKO TAYARI KUIPOKEA HIYO TAARIFA??Kwa mawazo yangu huyu hafai hata kidogo kwa mbunge wetu tena.
 
Wananchi ma Magu ni watu wa kupewa chumvi, t-shirt na kofia tu. Hayo mengine uliyoandika hapa sijui ya barabara, ujenzi wa shule, kuboresha hosp, maji n.k usahau. Lakini pia si aliwagawieni fulana, kofia, chumvi, pombe n.k . Hivyo kama mmeshavitumia vimeisha mumsubiri tena 2015 awaletee na mchague tena. Kwa Magu Mjini nilimsikia akiwapasha wananchi live kuwa huwa anashinda ubunge kwa pesa zake sio kwa kura zao again mnategemea kuletewa maendeleo ? Kaeni msubiri 2015 mletewe tena chumvi, t-shirt na kofia .
 
Huyu jamaa ni mkia wa mbuzi,kashindwa hata kutoa maji Nyamhongoro hadi Kisesa,huyu ni gamba,ila kushindwa kwake,cyo kushindwa kwa CCM,huyu jamaa ni moja ya wabunge wa CCM NISIOWAKUBALI kabisa.

Utaratibu wa bunge ni kwamba,waziri na manaibu mawaziri hawaruhusiwi kuuliza maswali,sasa huyu jamaa siyo waziri wala naibu,ila toka avuliwe unaibu waziri wa fedha,huwa hachangii chochote,nata huwa simuoni,ukute hata bungeni huwa haendi
 
Kaka kilicho na mwanzo na mwisho ipo tayari,kanda za vijijini elimu ya maendeleo kwa saä inashika kasi ya ajabu.ni kweli t-shirt hua anatoa,chumvi ndo usiseme,lakini akumbuke kwa sasa yupo kikaangoni.
 
Huyu jamaa ni mkia wa mbuzi,kashindwa hata kutoa maji Nyamhongoro hadi Kisesa,huyu ni gamba,ila kushindwa kwake,cyo kushindwa kwa ccm,huyu jamaa ni moja ya wabunge wa ccm NISIOWAKUBALI kabisa.Utaratibu wa bunge ni kwamba,waziri na manaibu mawaziri hawaruhusiwi kuuliza maswali,sasa huyu jamaa siyo waziri wala naibu,ila toka avuliwe unaibu waziri wa fedha,huwa hachangii chochote,nata huwa simuoni,ukute hata bungeni huwa haendi


Je,kaka kati ya haya majina aitwe nani sasa mbuzi,kondoo,kupe,bata,punda,kuku,mtu,mjinga,mwelevu,au jina tofauti.
 
Huyu jamaa ni mkia wa mbuzi,kashindwa hata kutoa maji Nyamhongoro hadi Kisesa,huyu ni gamba,ila kushindwa kwake,cyo kushindwa kwa ccm,huyu jamaa ni moja ya wabunge wa ccm NISIOWAKUBALI kabisa.Utaratibu wa bunge ni kwamba,waziri na manaibu mawaziri hawaruhusiwi kuuliza maswali,sasa huyu jamaa siyo waziri wala naibu,ila toka avuliwe unaibu waziri wa fedha,huwa hachangii chochote,nata huwa simuoni,ukute hata bungeni huwa haendi
huyu ni mburura,jimbo this term ni kwa makamanda tu.
 
Dr. F.Limbu ni msomi na ni Mchumii kitaaluma. Kwanini nimeanza na hilo, huyu mh alikuwa mwl wangu wa uchumi pale UDSM, nje ya siasa akiongea unajua kabisa hawezi kukaa meza moja na CCM, kwa maana inakuwa ngumu sana kwake kuinuka na kusifia, Mh Speaker, waziri, n.k. Pili mh. huyu siyo mwanasiasa kiuhalisia (naogopa kusema malengo yake yalikuwa uwazir/unaibu) hivyo kukaa na kuandaa taarifa za kusema uongo zinamshinda.
Wana Magu mnambuge Mchumi, mweledi ila kwenye chama ambacho siyo size yake. Ki ukweli ili ongee mara nying na upeleke hoja bungeni lazima uwe na uwezo wa kudanganya, kama huwezi ukapeleka makafu wanakubana mbavu kama Filikunjombe nk.
SP
 
atufai ata kidogo .kapita kwa kutumia pesa anajiamini atapita kwa kutumia pesa tena .tunamsubili itakula kwake.
 
Walai tena Dr.limbu namfaha si kiundani sana ,swala la elim sana nafaham,na mwabulenga nyumbani kwa napafaham,hadi dogo wake godi namfaham fika.sema tu elimu hiyo iko kwenye akili za .....haiwezekani ukawa na elimu na ukafanya mambo ya ajabu kama hayo,ama kweli unaweza kuwa na elimu bila hekima na busara,kama ccm ni kiatu ambacho hakimfai ya nini kung'ang'ania??hata wakati wa kwanza 1995,alikuja akiwa NCCR-MAGEUZI; Mafisadi wakamrubuni akahamia huko,mwache 2015 tunampiga chini.
 
Dr. ni janga la kitaifa, kiukweli sidhani kama anampango wa kugombea tena ubunge kwa jimbo la Magu, niliwahi kuuliza hapa JF kwa wanaMagu ni lipi la maana katufanyia mheshimiwa huyu? Mtoa uzi kaongelea ahadi za maeneo ya kwao na mheshimiwa kumbukeni kuna kata kama Yichobela, maeneo ya Lugeye,Kahangara na kwingineko pako hoi kabisa lakini ukiuliza vizee utashangaa na utaona Tanzania bado tuna safari ndefu! Nilikuwa kijiji cha Nyashimba siku moja nikawa naongea na babu yangu alichosema ni kwamba yeye na wazee wenzake hawana haja na maendeleo kwa sababu hata kama watatengeneza barabara au kuleta umeme havimsaidii bora mtu atakae wapa mche wa sabuni utamsaidia kwa wiki hata mbili ndo maendeleo kwake! Nilichoka na kuona kwa staili hii wabunge mburura wataendelea kushinda kama wana pesa. Ni jukumu letu wana Magu kulikataa hili na bahati nzuri kwa sasa vijana wapiga kura ni wengi zaidi ya wazee, hivyo basi ni jukumu letu kulikomboa jimbo la Magu kwa kujiandikisha kwa wingi na kujitokeza kupiga kura na kuhakikisha tunalinda kura zetu isijetokea kama uchaguzi ulopita!
 
Dr. ni janga la kitaifa, kiukweli sidhani kama anampango wa kugombea tena ubunge kwa jimbo la Magu, niliwahi kuuliza hapa JF kwa wanaMagu ni lipi la maana katufanyia mheshimiwa huyu? Mtoa uzi kaongelea ahadi za maeneo ya kwao na mheshimiwa kumbukeni kuna kata kama Yichobela, maeneo ya Lugeye,Kahangara na kwingineko pako hoi kabisa lakini ukiuliza vizee utashangaa na utaona Tanzania bado tuna safari ndefu! Nilikuwa kijiji cha Nyashimba siku moja nikawa naongea na babu yangu alichosema ni kwamba yeye na wazee wenzake hawana haja na maendeleo kwa sababu hata kama watatengeneza barabara au kuleta umeme havimsaidii bora mtu atakae wapa mche wa sabuni utamsaidia kwa wiki hata mbili ndo maendeleo kwake! Nilichoka na kuona kwa staili hii wabunge mburura wataendelea kushinda kama wana pesa. Ni jukumu letu wana Magu kulikataa hili na bahati nzuri kwa sasa vijana wapiga kura ni wengi zaidi ya wazee, hivyo basi ni jukumu letu kulikomboa jimbo la Magu kwa kujiandikisha kwa wingi na kujitokeza kupiga kura na kuhakikisha tunalinda kura zetu isijetokea kama uchaguzi ulopita!



Ichobela baba umenena ama kweli kuna mburura duniani,nimeshafanya survey maeneo mengi sana na ndo mana nikainisha machache,mfano;ng'wamabanza,Nyanguge,Nyasato,Nhobola,Jinjimili,Isolo,Kitongo,ng'wanhing'wa,na maeneo mengi lakini HOVYO, Kabolonga huyu jamaa,atakuja kuniona la sivyo atokomee.
 
Last edited by a moderator:
Poleni sana wananchi wa Jimbo la Uchaguzi la Magu kwa kufanywa kichwa cha mwenda wazimu ambacho kila mtu hujifunzia kunyoa!!! Kalagabaho, mmeshaliwa hivyo, na ukiona manyoya ujue ameliwa. Hata hivyo kwa kuwa mmegundua kuwa mbunge wenu hana upendo na nyie basi mjipange vizuri mwaka 2015 mchague mbunge mzuri. Kwa ufupi mbunge mzuri ni yule ambaye kwanza kabisa ana upendo wa dhati na nchi yake, na pili awe na upenndo wa dhati na jimbo lake la uchaguzi, wapiga kura wake awatumikie na kuwaheshimu kwa kuwa ndio waajiri wake. Kwa wakati huu huyo mtu wenu, kulingana na hii discussion interest zake siyo nyie wapiga kura, yeye aliutaka uwaziri apate neema. Jipangeni mtafute mmbunge mwenye upendo nanyi kama alivyo Mhe Luhaga Mpina, mbunge wa Kisesa, mkoani Simiyu, Mhe Lugola wa Jimbo la Mwibara, wilaya ya Bunda; na Deo Filikunjombe, Mbunge wa Ludewa. Angalieni mchoro huu hapa chini mjifunze, Mbunge anatakiwa awe na ukakamavu ule ule wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi, lakini ukiisha uchaguzi akapoa mjue mmeliwa!!!
View attachment 93264
 
Poleni sana wananchi wa Jimbo la Uchaguzi la Magu kwa kufanywa kichwa cha mwenda wazimu ambacho kila mtu hujifunzia kunyoa!!! Kalagabaho, mmeshaliwa hivyo, na ukiona manyoya ujue ameliwa. Hata hivyo kwa kuwa mmegundua kuwa mbunge wenu hana upendo na nyie basi mjipange vizuri mwaka 2015 mchague mbunge mzuri. Kwa ufupi mbunge mzuri ni yule ambaye kwanza kabisa ana upendo wa dhati na nchi yake, na pili awe na upenndo wa dhati na jimbo lake la uchaguzi, wapiga kura wake awatumikie na kuwaheshimu kwa kuwa ndio waajiri wake. Kwa wakati huu huyo mtu wenu, kulingana na hii discussion interest zake siyo nyie wapiga kura, yeye aliutaka uwaziri apate neema. Jipangeni mtafute mmbunge mwenye upendo nanyi kama alivyo Mhe Luhaga Mpina, mbunge wa Kisesa, mkoani Simiyu, Mhe Lugola wa Jimbo la Mwibara, wilaya ya Bunda; na Deo Filikunjombe, Mbunge wa Ludewa. Angalieni mchoro huu hapa chini mjifunze, Mbunge anatakiwa awe na ukakamavu ule ule wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi, lakini ukiisha uchaguzi akapoa mjue mmeliwa!!!
View attachment 93234

mama mdogo attachment haipo.
 
Mimi pia natokea Magu, nimeishi na kukulia magu nayajua mateso na mahangaiko ya watu wa magu. Matatizo ambayo yapo ndani ya uwezo wa mwakilishi wetu. kitu kikubwa watu wa magu tujitahidi kuwaelimisha wenye mawazo mgando, watu waliozoea kula nyama siku limbu akishinda, kupewa khanga, chumvi na samaki na kununuliwa kahawa.
 
Mimi pia natokea Magu, nimeishi na kukulia magu nayajua mateso na mahangaiko ya watu wa magu. Matatizo ambayo yapo ndani ya uwezo wa mwakilishi wetu. kitu kikubwa watu wa magu tujitahidi kuwaelimisha wenye mawazo mgando, watu waliozoea kula nyama siku limbu akishinda, kupewa khanga, chumvi na samaki na kununuliwa kahawa.
 
mama mdogo attachment haipo.

Pole sana, lakini attachment ipo. Naiweka tena hiyo attachment ili ujionee mwenyewe!!! Angalia picha ya huyu paka, kabla na wakati wa uchaguzi anakuwa mkali anashambulia kwa njia zote, halali na haramu; na mara akikipata kiti anachokipigania anakuwa mpoleeee wala hawahangaikii wapiga kura wake. Amkeni, wakati ni huu!!!

View attachment 93265
 
Back
Top Bottom