Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Jimbo la Karagwe mkoani Kagera linaenda kiulaini mikononi mwa CHADEMA kutokana na NEC ya CCM kurudisha jina la BLANDES GOZIBERT. Viongozi wa CCM hapa Karagwe wanasema BLANDES hawezi kushinda na hata akishinda hawezi kuongoza akiwa gerezani. Wanatoa sababu zifuatazo:
-Amekuwa anakabiliwa na kesi ya rushwa tangu uchaguzi wa ndani ya chama, na tarehe 4/8/2010 hakimu alitamka kuwa ana kesi ya kujibu baada ya kuhitimisha mchakato wa awali.
-Tarehe 30/8/2010 Blandes alikamatwa na TAKUKURU tena na wapambe wake na kulala ndani kwa mahojiano. Hivi sasa wanakamilisha taratibu za kumfungulia kesi nyingine ya rushwa.
-Kamati ya siasa ya wilaya na Mkoa walitoa alama ya chini kwa jina lake kwa kuhofia kuwa likirudi atashindwa kirahisi.
Wakati huo huo, CHADEMA wamemsimamisha kijana DEUSDEDIT JOVIN kwa jimbo la Karagwe. Kijana huyu, miaka 38 anauzika vizuri kwa watu, ana ujasiri na uwezo mkubwa wa kuchambua masuala mbalimbali. Licha ya kubobea katika kufundisha IT lakini ni mwandishi mchambuzi katika magazeti ya Raia Mwema, Mwana Halisi na Tanzania Daima. Zamani aliandika sana katika Rai, lakini lilipouzwa kwa Rostam aliacha.
Habari ndiyo hiyo.
-Amekuwa anakabiliwa na kesi ya rushwa tangu uchaguzi wa ndani ya chama, na tarehe 4/8/2010 hakimu alitamka kuwa ana kesi ya kujibu baada ya kuhitimisha mchakato wa awali.
-Tarehe 30/8/2010 Blandes alikamatwa na TAKUKURU tena na wapambe wake na kulala ndani kwa mahojiano. Hivi sasa wanakamilisha taratibu za kumfungulia kesi nyingine ya rushwa.
-Kamati ya siasa ya wilaya na Mkoa walitoa alama ya chini kwa jina lake kwa kuhofia kuwa likirudi atashindwa kirahisi.
Wakati huo huo, CHADEMA wamemsimamisha kijana DEUSDEDIT JOVIN kwa jimbo la Karagwe. Kijana huyu, miaka 38 anauzika vizuri kwa watu, ana ujasiri na uwezo mkubwa wa kuchambua masuala mbalimbali. Licha ya kubobea katika kufundisha IT lakini ni mwandishi mchambuzi katika magazeti ya Raia Mwema, Mwana Halisi na Tanzania Daima. Zamani aliandika sana katika Rai, lakini lilipouzwa kwa Rostam aliacha.
Habari ndiyo hiyo.