Jimbo la Buhigwe linaliwa kama mchwa

mwanzo wetu

JF-Expert Member
May 4, 2014
1,581
461
Habari wakuu,. Poleni na majukumu ,

Nianze Kwa kusema kuwa Jimbo la Buhigwe ni Moja ya Jimbo ambalo linapokea Miradi mingi ya maendelo Kuliko wilaya nyingi za hapa Tanzania, na Hii ni kutokana na Jimbo Hilo kuwa eneo analozaliwa makamu wa Rais hivyo Hii imechangia sana kupata maendeleo haraka,

Kwa mda mfupi Wana benki ya NMB, chuo Cha Tehama Kiko mbioni kujengwa , stend kubwa ya mabasi ikiwemo barabara za mji wa Buhigwe kutandikwa lami.

Jimbo la Buhigwe Liko chini ya CCM na linaongozwa na Kavejuru licha kuwa anaupinzani mkubwa kutokana na Jimbo Hilo kuwa na viashiria vya kuwepo kwa watu wanaoonekana kulitaka Jimbo Hilo kwa nguvu Zote.

Zaidi nacho taka kusema juu ya Jimbo la Buhigwe ni tatizo la viongozi wengi kutokuwa waadilifu kwa kutumia pesa vibaya zinazofika ktk wilaya ya Buhigwe

Matumizi mabaya ya fedha Kwa wilaya hiyo kumepelekea baadhi ya mambo kukwama ,
viongoz wengi wa jimbo Hilo siyo wazalendo Bali wanawaza kuwaibia wananchi tu na pesa za Miradi kutumika vibaya .

Jimbo la Buhigwe linakila sababu za kupata mabadilko makubwa ya uongozi hapa na imaana wapate viongozi waadirifu na wenye utu Ili kulinda Rasilimali za wanabuhigwe na pesa Za maendeleo zinazofika ktk Maeneo ya Jimbo.

NB. Mpango awe makini Jimbo linaharibiwa kumchafua Ili ionekane hajali maendeleo ya nyumbani jambo ambalo siyo sahihi.

Wananchi wa Buhigwe wabutuke watetee maendeleo Kwa kuwa na viongozi wazuri wenye uchungu na maendeleo.
 
Back
Top Bottom