Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
[h=2]Sunday, July 8, 2012[/h][h=3]SAKATA LA WATUMISHI WASIO NA SIFA JIJI LA MBEYA KUPANDISHWA VYEO LASABABISHA MAKUBWA[/h]
SAKATA la baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kupandishwa vyeo pasipokuwa na sifa, limechukua sura mpya ambapo aliyekuwa afisa utumishi wa Jiji hilo aliyejulikana kwa jina la Koming'o ameondolewa katika nafasi hiyo.
Taarifa za uhakika zilizoufikia mtandao wa kalulunga zimesema kuwa kuondolewa afisa huyo kwenye nafasi yake ni pamoja na kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili zikiwemo za kupokea rushwa kwa watumishi aliowapandisha vyeo.
Kabla ya Afisa huyo kuondolewa kwenye nafasi hiyo, aliitwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Juma Idd pamoja na jopo lake ambapo alipopewa kusoma barua ya tuhuma zake aliishika barua hiyo kisha akaishiwa nguvu na kuanguka mbele ya Mkurugenzi huyo na kukimbizwa Hospitalini.
Kwa mujibu wa habari za uchunguzi ambazo kikosi kazi cha mtandao wa kalulunga kimezinasa, mtumishi huyo akithibitika kuhusika na tuhuma hizo atafukuzwa kazi na kwa taarifa za jalada lake la kazi amebakiza mwaka mmoja kustaafu katika utumishi wake.
Habari za kuanguka alipokuwa ameitwa ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji hilo zimethibitishwa na Mkurugenzi Juma Idd alipohojiwa na mtandao huu ambapo alisema kuwa hakuwa tayari kuzungumzia tuhuma hizo kwa ujumla wake.
Posted by PASTOR GORDON KALULUNGA at 10:11 PM 0 comments
SAKATA la baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kupandishwa vyeo pasipokuwa na sifa, limechukua sura mpya ambapo aliyekuwa afisa utumishi wa Jiji hilo aliyejulikana kwa jina la Koming'o ameondolewa katika nafasi hiyo.
Taarifa za uhakika zilizoufikia mtandao wa kalulunga zimesema kuwa kuondolewa afisa huyo kwenye nafasi yake ni pamoja na kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili zikiwemo za kupokea rushwa kwa watumishi aliowapandisha vyeo.
Kabla ya Afisa huyo kuondolewa kwenye nafasi hiyo, aliitwa na Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Juma Idd pamoja na jopo lake ambapo alipopewa kusoma barua ya tuhuma zake aliishika barua hiyo kisha akaishiwa nguvu na kuanguka mbele ya Mkurugenzi huyo na kukimbizwa Hospitalini.
Kwa mujibu wa habari za uchunguzi ambazo kikosi kazi cha mtandao wa kalulunga kimezinasa, mtumishi huyo akithibitika kuhusika na tuhuma hizo atafukuzwa kazi na kwa taarifa za jalada lake la kazi amebakiza mwaka mmoja kustaafu katika utumishi wake.
Habari za kuanguka alipokuwa ameitwa ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji hilo zimethibitishwa na Mkurugenzi Juma Idd alipohojiwa na mtandao huu ambapo alisema kuwa hakuwa tayari kuzungumzia tuhuma hizo kwa ujumla wake.
Posted by PASTOR GORDON KALULUNGA at 10:11 PM 0 comments
Reactions: |