Jiji la Arusha leo limeamka na mgomo wa daladala

Jiji la Arusha leo limeamka na mgomo wa daladala

Trafick wa Ar ni aibu tupu. Ni omba omba hadi basi. Ajabu unampa halafu anaenda kituo kingine ukipita anakupiga mkono anaomba tena. Hivi ni lazima wawepo baarabarani kila siku ? Si wameshakagua yote ?
 
Kwakwel inaumiza sana nimepita pale maeneo ya Soko mjinga kuna mwanafunzi amegongwa na bodaboda maskin cjui atapona!yaan kuna vurugu za bodaboda sana
 
Yaweza kuwa shughuli ya ziada kwani ninavyoijua A-town wanafunzi kwa pamoja hawachelewi kutia tim kwa wakuu au kufunga ile barabara ya IACC.
 
mgomo huu sababu kuu ni trafiki wamefanya daladala ni mahali pa kupatia pesa .wanachukua rushwa peupe mchana .
 
pamoja na malipo duni kutoka kwa bosi wao ligavament siyo sababu ya kugeuza dalala vitega uchumi
 
Kituo cha Usa river ni kama mali ya polisi na wakiamua kukuminya wanakuminya wapendavyo hata mbele ya bosi wao.
Hakuna haki wala hawakuambii kosa fulani sheria inasemaje wala hakuna cha onyo.....eti afande adhabu yake mwandikie elfu sitini na asikupotezee muda akitaka aende anakojua atapata haki.....

Hapa Usa River yupo polisi aitwaye ALLAN/ALLEN mwizi mla rushwa shetani mgandamizaji, yanii ni vurugu tupu wapo na wenziwe ila majina yananitoka, natamani na sisi tungekuwa na magereza ya kuwaweka maana wao ni miungu watu phuuuu takataka usa river.


Tumekata tamaa tunajuta kuzaliwa Tanzania pasipo na haki serikali inashindwa kuwasimamia watendaji wake ambao ni polisi, ccm inashindwa kuondoa dhuluma, hakuna elimu ya uraia kwamba polisi unapaswa umhoji kitu gani........
 
Trafiki Arusha wanatia aibu sana nchini. Kuna wakati huwa natamani kuwagonga wanaponipiga mkono.
 
uuuuwi jamani hayamateso yamezidi serekali sikivu tunatabika sisi walalahoi
 
mimi arusha kwa trafic sisimami na nikisimama nimechukia muda wote.------- nyaji hawa.
 
Wanalalamika kukamatwa na polisi wa barabarani kwa makosa yanayosababishwa na mamlaka ya mji haswa ni vituo, mamlaka haijaweka vituo maalum au madereva hawajui vituo halaf wakisimama sehemu wanayoamini ni vituo wanakamatwa kwa kutosimama kituoni.

Asante kwa ufafanuzi unanitoa hofu yangu. Askari ndo zao hasa tunapokaribia na sikukuu yoyote, na sasa Pasaka inakaribia!
 
Back
Top Bottom