Jihadhari na matapeli hawa wa Kupatana.com

mwanaMtata

JF-Expert Member
Oct 18, 2014
2,393
1,432
Habari ya wakati na muda kama huu ndugu zangu watanzania na East Afrika kwa ujumla. Nianze kwa kutoa pole kwa ndugu jamaa na rafiki wote walioko kwenye mfungo. Mwenyezi awajalie wepesi.

Dhumuni la kuanzisha thread hii ni kuwafungua tu macho watu hasa wale wanaopenda biashara ya mtandao. Kuna mitandao mingi sana ila leo naomba tuongee hii site ambayo ni kama "advertising center" www.kupatana.com

Kwa mimi kupatana ndio kama kariakoo yangu na nina uzoefu sana na pia ninmara chache sana inatokea nafanyiwa dhuluma na hii ni pale mtu anaamua kukuuzia kitu kwa ujanja ujanja ila pia mwisho wa siku ukitumia mbinu mbadala anapatikana.

Kuna siku niliingia kupatana nikakutana na tangazo hili

8a8a036801f473973d4e0221d631c4fc.jpg


dcf6558116283d017ca2e8de9d3bdf80.jpg


Nilipoona tangazo ninla bei rahisi na namba iko ya nchini kwetu kwanza nikapiga, haikuwa hewani ndipo nikamchatisha whats app
Mazungumzo yalikua hivi

705a3cf2b27554ff3fc82681e1efc220.jpg


Akaniambia yuko kenya na kujitetea kwingi. Sasa uzuri mimi kenya ni kama nyumbani. Nina marafiki kibao na ndugu pia nikaona sio kesi nikaunda Group kati yangu mimi, yeye na Derick rafiki yangu aloko kenya

2c00af1eb7ad5c642f84e222122faa17.jpg


Jamaa akawa analefu tuu kila saa ikabidi nimfate inbox nimtulize wenge kwa kumuelewesha

3d1e8ca505291b4b6a5e98061ffdddcf.jpg


Hatimaye akakubali kua kwenye group nikamrudisha tena na mazungumzo yakaendelea kama ifuatavyo

2a1e0ce7e356a238c6cd5be3ec4fe825.jpg


14f276813569ae9852d79abf34ea9e19.jpg


Nilivoona anataka biashara za yule jamaa mwingine anaesemaga yuko mtwara nikamuuliza jina la kampuni labda ingenipa muongozo

52b3b0e61e309a07985403a5721becd2.jpg


Baada ya kutaja jina la kampuni niliingia Google na kuangalia cha kwanza nikakuta kampuni iko india. Sikutilia maanani kwani majina tu yanaweza kufanana ila nikafanya more digging sijakuta kampuni yenye jina hilo kenya

f89888fb985298859fe795a2629efd25.jpg


Baada ya kukosa kampuni hio ilinipasa kuomba blog au website pengine hapo ningepata mwanga. Aliposema pia hata hivo hana nikajua hawa ndo walewale wanasubiri watu watafute pesa kwa jasho wao waje wale kirahisi.

b738806ce6707e96aa20535fed5ebb02.jpg


Ombi na pendekezo langu si kwa wamiliki wa kupatana tuu, bali humu jamii forum (matangazo madogo madogo) na hata kina OLX muwe na acccess ya kumwezesha mtumiaji wa hii service yenu kulalamika pale anapofanyiwa fraud, mkiridhika na utafiti kwamba kweli mlengwa au mtajwa ametapeli basi muwezeshe kutiwa nguvuni kwa jangiri hilo.
Najua mnaogopa kupoteza viewers kwa ajili ya CPM na mambo kama hayo, ila ukiangalia kwa undani watu wengi watakua wanatumia mtandao wako kwani wana uhakika walau asilimia 60% kwamba hata wakipigwa (kutapeliwa) kuna msaada.
NI HAYO TUU WAKUU KARIBUNI KWA KUCHANGIA
 
Dunia imeharibika. Uaminifu BASHITE!

Ahsante mkuu wengi tungepigwa.

Ahsante mkuu kwa ujumbe

Asante mkuu kwa kutufumbua macho

Yaani wako wengi sana chamsingi ni kua waangalifu.
Sitaki kuwa na dhana ya kuwaogopesha kua mali za bei rahisi hakuna zipo na watu wanaziuza kutokana na misala wanayopitia maishani. Kuna rafiki yangu alikua katoka kutoa hela ATM akalipie pango maana baba mwenye nyumba alikua kashamkalia kooni, bajaji aliopanda wakafanya yao wakachukua shilingi zile zote. Akarudi nyumba an LG curved smart ya 40" akaiuza 700,000/= kwa io vitu vya bei rahisi vipo ila cheza na muuzaji mpeleleze.

1)Ukiskia anaanza story za huu mzigo una wateja kama tano broo tuma ela fasta nikutumie basi muogope

2) akiwa anakimbilia kukuliza uko wapi muulize kwanza wewe uko wapi? Wengi wanategea ukishamwambia niko dar anakuambia niko mtwara. Sasa mtegee akisema nipo lindi na wewe mwambia nipo Ruvuma hapa ila nina safari ya kuja lindi kesho utaona anabadili maelezo..

3) mtu anaetaka uweke deposite ndo akuletee mzigo. Yaani mtu yuko hapa dar kama wewe ila anakuambia simu ya laki saba ili itoke ofisini lazima aache deposit ya laki tatu ndo akuletee.. hao nao wapigaji
 
Kupatana asilimia kubwa ni matapeli, labda ninabahati mbaya.

First time nilipost gari, jamaa toka Dar akata aje mkoani kununua hiyo gari lakini story ikawa ndefu sana. Mara nauli vitu vingi nikajua hapa napigwa nikashituka.

Second time nyumba, same story.

Kuna jamaa mmoja wa Iring huyu ndio tapeli aliyebobea. Sijui kupatana hawalijui hilo, au wanaziba pamba masikio
 
Laiv Mzeee watu wamekua Co watuuuuu saiv lengo n kupiga fwezaaa na ishu za mtandaon without knowing kinachoendeleaaa watakuumizaa sanaa
 
Kupatana asilimia kubwa ni matapeli, labda ninabahati mbaya.

First time nilipost gari, jamaa toka Dar akata aje mkoani kununua hiyo gari lakini story ikawa ndefu sana. Mara nauli vitu vingi nikajua hapa napigwa nikashituka.

Second time nyumba, same story.

Kuna jamaa mmoja wa Iring huyu ndio tapeli aliyebobea. Sijui kupatana hawalijui hilo, au wanaziba pamba masikio
Yaani mkuu mtu yeyote akikosa umakini hata ukiingia kwenye mall kama Mlimani City bado inaweza ukatoka umeshika kichwa.
1)jua unachonunua
2)jua thaman
3)jua ubora {kujua fake na original}
4) omba Mungu biashara iende smooth maana skuizi kuna wanaotumia visu kutisha watu
 
Watu sio waaminifu hata kidogo sikuhz usipokua makini unatapeliwa
Jana nimetumiwa SMS hii:


Habari ya leo sasa kuhusu nafasi uliyoniomba imepatikana tayari JWTZ(TPDF)tunateua kwenda TANAPA mwandae kijana wako aje 2kamilishe utaratib na 2napokea vijana wa mafunzo ya awali kwa mujibu wa sheria niongezee vjana wa2au3 wenye sifa za JKT.


Wife naye katumiwa nimebaki kucheka tu.
 
Uzur alikukuta nawe ni kajanja flan wa mjini,,ulimzungusha unavyotaka wewe mwsho akaingia mzima mzima kutaka kukimbia,,big up bro,umetufumbua macho sana wengi humu
 
Jana nimetumiwa SMS hii:


Habari ya leo sasa kuhusu nafasi uliyoniomba imepatikana tayari JWTZ(TPDF)tunateua kwenda TANAPA mwandae kijana wako aje 2kamilishe utaratib na 2napokea vijana wa mafunzo ya awali kwa mujibu wa sheria niongezee vjana wa2au3 wenye sifa za JKT.


Wife naye katumiwa nimebaki kucheka tu.
Hawa hawana tofauti na wale wanaojidai wamekosea meseji inakuja yenye ujumbe huu "KAZI ULIONITUMA KONGO NIMEMALIZA MKUU, YULE MFANYAKAZI ALOKUIBIA SASA ANAPATA MATATIZO YEYE NA FAMILIA YAKE, YULE MWANAMKE UNAEMTAKA WIKI HII ATAKUJA KWAKO NA ILE YA MAFANIKIO SASA NDO KUNA MASHARI KIDOGO YAMEBAKI. UKITIMIZA HAYO MILIONI ZITAKUA ZINAINGIZWA KWAKO KILA SIKU NA WATU USOWAJUA"
Hapo ukimwambia wrong number anakuambia anhaa sasa anaanza kutiririka sifa zake
 
Uzur alikukuta nawe ni kajanja flan wa mjini,,ulimzungusha unavyotaka wewe mwsho akaingia mzima mzima kutaka kukimbia,,big up bro,umetufumbua macho sana wengi humu
Sasa huyu ni mwizi maskini. Kuna wape wako vizuri yaani wamejipanga "kukupakua" una kuta wana website kila kitu wamekamilika wanakupa a good customer service mpaka unaingia kingi. Ukituma hela sasa ndo mtihani unaanza hapo.
 
Mkuu kuna kua mshamba na kutokujua kitu. Alafu kama kupigwa watu wanapigwa hadi live live kkoo. Hapa tunajaribu kupunguza makali tu ya wapigaji
Sijui why JF kuna too much negativity! Sijui ni kujua kwingi or what, no matter how the gud the topic is lkn lazma atoke Mr Negative jst from nowhere atibue! Watakuwa ndo wapigaji wenyewe hawa!
Thnks for the awareness
 
Back
Top Bottom