Jifunze uvumilivu na subira

Jifunze uvumilivu na subira

Mjusi Sharobalo

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2025
Posts
7,442
Reaction score
12,715
Mwenye subira hula mbivu, mara nyingi hula zilizoiva vizuri zaidi. Mtu hukata jiwe sio kwa nguvu, bali kwa kudumu. Endelea tu, usichoke. Wakati sahihi wa Mungu ni bora kuliko haraka ya mwanadamu. Tulia na amini mchakato. Mbegu haichanui si ileile inayopandwa. Vitu vizuri huchukua muda. Subira ni chungu, lakini matunda yake ni matamu zaidi... Mjusi na tafakari.
 
Mwenye subira hula mbivu, mara nyingi hula zilizoiva vizuri zaidi. Mtu hukata jiwe sio kwa nguvu, bali kwa kudumu. Endelea tu, usichoke. Wakati sahihi wa Mungu ni bora kuliko haraka ya mwanadamu. Tulia na amini mchakato. Mbegu haichanui si ileile inayopandwa. Vitu vizuri huchukua muda. Subira ni chungu, lakini matunda yake ni matamu zaidi... Mjusi na tafakari.
Exactly....wenye kuwa na subra wa pamoja na M/mungu
 
Exactly....wenye kuwa na subra wa pamoja na M/mungu
Kwanza nikupongeze bwana makoti kwa kukalia siti ya mbele leo. Hongera sana. Naamu watu wengi hushindwa kufikia malengo sababu ya kutokowa na subira katika mambo yao. Kumbuka hata mbuyu ulianza kama mchicha, jifunze kuheshimu kila hatua ya maendeleo yako unayopiga maishani mwako.
 
Mwenye subira hula mbivu, mara nyingi hula zilizoiva vizuri zaidi. Mtu hukata jiwe sio kwa nguvu, bali kwa kudumu. Endelea tu, usichoke. Wakati sahihi wa Mungu ni bora kuliko haraka ya mwanadamu. Tulia na amini mchakato. Mbegu haichanui si ileile inayopandwa. Vitu vizuri huchukua muda. Subira ni chungu, lakini matunda yake ni matamu zaidi... Mjusi na tafakari.
Maamae mjusi sharobalo mwajuma's ndala ndefu boy friend. Unashusha nondo za uhakika na kutema madini yaliyojitosholeza.

Nyau wewee!
 
Haiwezi kufanya kazi mara zote , kuna mda inakupasa usiwe mvumilivu , ili kuokoa muda .
 
Haiwezi kufanya kazi mara zote , kuna mda inakupasa usiwe mvumilivu , ili kuokoa muda .
Katika makosa makubwa unayopaswa kuyaepuka kufanya bwashee, ni kuharakisha mambo kabla ya wakati sahihi, wahenga wanakwambia haraka haraka haina baraka, jifunze kufuata utaratabu katika kila jambo.
 
Katika makosa makubwa unayopaswa kuyaepuka kufanya bwashee, ni kuharakisha mambo kabla ya wakati sahihi, wahenga wanakwambia haraka haraka haina baraka, jifunze kufuata utaratabu katika kila jambo.
Dogo , endelea kuwa na subira hapo kwa shemeji yako.
 
Bado wewe ni mdogo kujadili hili .vitu vingine ni muhimu sana kujifunza kwa uzoefu.
Bwashee unajivua vyeo wewe mwenyewe kwa kuongea vitu visivyo na mantiki namna hiyo, maisha hayachagui umri wa mtu, pia hoja hujibiwa kwa hoja na si kuangalia udogo au ukubwa wa mtu.
 
Kwanza nikupongeze bwana makoti kwa kukalia siti ya mbele leo. Hongera sana. Naamu watu wengi hushindwa kufikia malengo sababu ya kutokowa na subira katika mambo yao. Kumbuka hata mbuyu ulianza kama mchicha, jifunze kuheshimu kila hatua ya maendeleo yako unayopiga maishani mwako.
Swadakta kabisa.....
 
1-Mvumilivu hula mbivu.

2-Subira yavuta heri.

3-Chelewa chelewa utakuta mwana si wako.

Sasa utachagua mwenyewe. Moja, mbili au tatu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom