Jifunze namna ya kutengeneza dawa ya kusafishia marumaru

Najaribu kukupm nashindwa nina jambo muhimu sana na wewe mkuu yna2 hata sijui nifanyeje
Habari za jumapili wapendwa,

Yna2 Leo nimewaletea somo la kujifunza namna ya kutengeneza dawa ya kusafishia marumaru.

MAHITAJI

-hydrochloric acid Lita 10- kazi yake kuondoa uchafu sugu ulio kwenye marumaru
-maji lita30
-sless au sabuni ya maji lita1-kuleta povu kwenye dawa yetu
-perfume vijiko 6 vya chakula- kuleta manukato kwenye dawa yetu
-pipa au ndoo
-rangi ukipenda vijiko 2 vya chakula
-usisahau gloves..mask ya pua..buti

JINSI YA KUTENGENEZA

Andaa mazingira yako yawe masafi. Tayarisha pipa au ndoo/beseni yako. Anza kuweka maji lita30, ikifuatiwa na hydrochloric acid Lita 10, ikifuatiwa na sless au sabuni ya maji lita1, perfume na rangi kisha koroga kwa dakika 15.

Dawa yetu itakua tayari

Nimemaliza.
 
Toa ufafanuzi hapa kwenye hivi vipengele:

1. HCl iwe na conc asilimia ngapi?

2. Ni perfume gani hapa unayotaja, fragrant oil extracts zile za perfume au ni katika form ipi?

3. Rangi zipi hapa, zile za vyakula, nyumba, magari ama?
Na “ BUTI “ , pia hajasema ni aina gani la mgambo,gum au kama lile wanalovaa wapiga deki mahospitalini
 
Habarii,kwanza nakushukuru ww ulieleta uzi huu,kwa waliokuwa dar mahitaji ya vitu vivyo waende machinga pale utapata vyooooooooooooooote, jamani rangi ya nyumba haipakwi kwenye nguo, kila bidhaa ya kama sabani ,iwe ya maji au kipande ,mafuta ya mdando ,na hizi dawa za kuuwa wadudu lazima ziwekwe pafyum kwa ajili ya kuleta harufu nzuuuli lkn kila bidhaaa ina rangi yake na pafyum yake
 
Naam haya ndio maneno yna2...

Maana hii michanganyiko ya kemikali hukawii kutengeneza compound isiyo na jina
Kweli muhimu sana mtu anaweza akachukua acid yenye 98% concentration akatengeneza moto nyumbani watu wakamshangaa,kumbe ni kwa vile maelekezo aliyopewa hayakuwa complete.
 
Back
Top Bottom