Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,555
- 41,065
Wayahudi, idadi yao ni ndogo sana, japo kuna wakati walikuwa wengi kidogo. Mwaka 1939, kabla ya vita kuu ya Dunia, idadi ya Wayahudi ilifikia 15.3 million Hitler aliwaua Wayahudi wapatao milioni 6. Wayahudi waliprudi Mashariki ya kati na kuanzisha Taifa la Israel mwaka 1948 walikuwa 0.806 milioni. Ifahamike kuwa mwaka 1933, idadi ya Watanganyika inakadiriwa kuwa watu milioni 5 tu, yaani Wayahudi walikuwa wengi mara 3 ya Watanganyika.
Kabla ya Wayahudi kuvamia na kutwaa eneo la Caanan ambalo ndiyo ardhi asilia ya Wayahudi, lilikuwa na ukubwa wa 50,000 kilometa za mraba. Israel ya leo ina ukubwa wa mita za kilometa za mraba 22,145.
Lakini hata kabla ya haya yaliyowapata baada ya Kristo, kabla yake walipitia madhira mengi kama vile kutengwa na Mungu (walipotenda kinyume na maagano), kuuawa na kutiwa utumwani mara kadhaa. Hivyo, kwa Wayahudi, kuuawa, kupigana vita na kushinda na hata kushindwa, kuishi kwa kumpendeza Mungu, kumkana, na kutenda kinyume cha mapenzi ya Mungu, imekuwa ndiyo mfumo wao wa maisha wakati wote. Na kiimani, tunaamini kuwa hayo yote ndivyo mpango wa Mungu ulivyo dhidi ya Israel na Ulimwengu mzima.
Israel imewahi kudhulumiwa na Wamisri, Wamaleki, Wafilisti, Wapersia, Wababiloni, Warumi, na nchi na makabila mengine mengi.
Kwa nini yote haya yanawatokea Waisrael?
Kwa kadiri ya biblia, ni kwa sababu, Mungu ana mpango na Taifa la Israel, na shetani yupo kwa sababu ya kuharibu mpango wa Mungu. Hivyo ni shetani anawatumia majirani zake, kuiangamiza Israel.
Kiimani, ni kwamba sijui awe ni Hitler, Iran, Wasyria, Hamas au Hizibollah, Wabogoni (Russia), hakuna aliyeweza au atakayeweza kuwaangamiza na kuwapoteza Waisrael. Maangamizi ya Waisrael yatakuja na kutoweka, na wala maangamizi hayo hayamaanishi kuwa tunaelekea siku za mwisho kama baadhi ya watu wanavyotaka kutuaminisha.
Nyakati hizi za mahangaiko ya Wayahudi inatajwa kuwa tribulation (Yeremia 30:7).
Lakini kuhusu siku za mwisho, kuhusiana na Israel, biblia inasema kuwa, makundi makubwa ya Wayahudi yatarejea kwenye ardhi ya Israel (Kumbukumbu la Torati 30:3; Isaya 43:6; Ezekiel 34:11-13; 36:24; 37:1-14). Ifahamike mpaka sasa hivi, Wayahudi wanaoishi Israel ni milioni 9 tu. Wayahudi wapatao 18 milioni wanaishi nje ya Israel, kwenye mataifa mbalimbali.
Kisha mpinga Kristo atafanya mkataba wa amani wa miaka 7 na Waisrael (Isaya 28:18; Daniel 9:27).
Hekalu lililovunjwa (bila shaka kutokana na vita) litajengwa upya mjini Yerusalem (Daniel 9:27; Matayo 24:15; 2 Watesolonike; 2:3-4; Ufunuo 11:1).
Mpinga Kristo atavunja mkataba wa amani uliosainiwa, na mauaji makubwa ya Wayahudi yatafanyika (Daniel 9:27; 12:1, 11; Zacharia 11:16; Matayo 24:15, 21; Ufunuo 12:13). Israel itavamiwa (Ezekiel 38-39).
Kisha Wayahudi watamtambua na kumkiri Yesu kuwa ndiye Masiha (Zacharia 12:10). Baada ya kumkiri Kristo, Israel mpya itazaliwa, itahuishwa, na itaungamishwa kama ilivyokuwa kale (Yeremia 33:8; Ezekiel 11:17; Warumi 11:26).
Andiko hili ni kwaajili ya wanaotaka kujifunza, wasio na nia hiyo, wasihangaishwe nalo.
Kabla ya Wayahudi kuvamia na kutwaa eneo la Caanan ambalo ndiyo ardhi asilia ya Wayahudi, lilikuwa na ukubwa wa 50,000 kilometa za mraba. Israel ya leo ina ukubwa wa mita za kilometa za mraba 22,145.
Lakini hata kabla ya haya yaliyowapata baada ya Kristo, kabla yake walipitia madhira mengi kama vile kutengwa na Mungu (walipotenda kinyume na maagano), kuuawa na kutiwa utumwani mara kadhaa. Hivyo, kwa Wayahudi, kuuawa, kupigana vita na kushinda na hata kushindwa, kuishi kwa kumpendeza Mungu, kumkana, na kutenda kinyume cha mapenzi ya Mungu, imekuwa ndiyo mfumo wao wa maisha wakati wote. Na kiimani, tunaamini kuwa hayo yote ndivyo mpango wa Mungu ulivyo dhidi ya Israel na Ulimwengu mzima.
Israel imewahi kudhulumiwa na Wamisri, Wamaleki, Wafilisti, Wapersia, Wababiloni, Warumi, na nchi na makabila mengine mengi.
Kwa nini yote haya yanawatokea Waisrael?
Kwa kadiri ya biblia, ni kwa sababu, Mungu ana mpango na Taifa la Israel, na shetani yupo kwa sababu ya kuharibu mpango wa Mungu. Hivyo ni shetani anawatumia majirani zake, kuiangamiza Israel.
Kiimani, ni kwamba sijui awe ni Hitler, Iran, Wasyria, Hamas au Hizibollah, Wabogoni (Russia), hakuna aliyeweza au atakayeweza kuwaangamiza na kuwapoteza Waisrael. Maangamizi ya Waisrael yatakuja na kutoweka, na wala maangamizi hayo hayamaanishi kuwa tunaelekea siku za mwisho kama baadhi ya watu wanavyotaka kutuaminisha.
Nyakati hizi za mahangaiko ya Wayahudi inatajwa kuwa tribulation (Yeremia 30:7).
Lakini kuhusu siku za mwisho, kuhusiana na Israel, biblia inasema kuwa, makundi makubwa ya Wayahudi yatarejea kwenye ardhi ya Israel (Kumbukumbu la Torati 30:3; Isaya 43:6; Ezekiel 34:11-13; 36:24; 37:1-14). Ifahamike mpaka sasa hivi, Wayahudi wanaoishi Israel ni milioni 9 tu. Wayahudi wapatao 18 milioni wanaishi nje ya Israel, kwenye mataifa mbalimbali.
Kisha mpinga Kristo atafanya mkataba wa amani wa miaka 7 na Waisrael (Isaya 28:18; Daniel 9:27).
Hekalu lililovunjwa (bila shaka kutokana na vita) litajengwa upya mjini Yerusalem (Daniel 9:27; Matayo 24:15; 2 Watesolonike; 2:3-4; Ufunuo 11:1).
Mpinga Kristo atavunja mkataba wa amani uliosainiwa, na mauaji makubwa ya Wayahudi yatafanyika (Daniel 9:27; 12:1, 11; Zacharia 11:16; Matayo 24:15, 21; Ufunuo 12:13). Israel itavamiwa (Ezekiel 38-39).
Kisha Wayahudi watamtambua na kumkiri Yesu kuwa ndiye Masiha (Zacharia 12:10). Baada ya kumkiri Kristo, Israel mpya itazaliwa, itahuishwa, na itaungamishwa kama ilivyokuwa kale (Yeremia 33:8; Ezekiel 11:17; Warumi 11:26).
Andiko hili ni kwaajili ya wanaotaka kujifunza, wasio na nia hiyo, wasihangaishwe nalo.