Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
VIJANA WENGI tumepotea hapo,tuonapo basi tunataka kutimiza ile macho imeona,na hii ni hatari sana!Hebu tuwaulize na madada wanaovaa hivyo wana malengo gani?au ndo biashara yenyewe iko sokoni?Hata kama ni sokoni,je wale madada wanaovaa hivyo hali wanajua kuwa ni wake za watu wanakuwa wamenuia kufanya nini?au wanakuwa kwenye mazingira ya kusaliti ndoa zao?Anyway sijui bwana lakini nachoomba Kijana simama imara usije ukalaumu jicho kuwa limekuponza!Wengine wakianguka katika zinaa, utawasikia wakijitetea na kusema; "Nilibanwa mno hata nikashindwa kujizuia – nikaanguka katika zinaa."
Unaweza ukajitetea hivyo, lakini ungeamua kushinda, Bwana angeuwezesha kushinda. Kwa kuwa imeandikwa; " Ninyi watoto wadogo mwatokana na Mung; nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye NDANI YENU NI MKUU KULIKO aliye katika dunia." (1 Yohana 4:4) " Lakini katika mambo hayo yote TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDANA kwa yeye (Yesu Kristo) aliyetupenda (Warumi 8:73)