Jeshi litachukua nchi Misri?

Naambiwa Muslim Brotherhood are the likes of HAMAS na AL-QAEDA ni chama chenye msimamo mkali sana na Serikali ya Marekani wanafanya kila liwezekanalo ili chama hicho kisishike hatamu ya uongozi Misri
 

Israel je????
 
MwanaFalsafa1 i really like your comment it reflects something
 
Ukishaanza kuua wananchi wako kwa ajili ya kubakia mabadarakani katika mazingira ya kisiasa unachochea wananchi wako kuzidi kukupinga. Hii ni kanuni ambayo bado haijaoneshwa kuwa ya uongo.
Sio kweli, kanuni yako imepinda.

Kina Sadaam, Kim Jong Il, Iddi Amin, Hitler, Bokassa, Mobuttu, Bongo wametawala kwa kuua raia, na wamebaki madarakani mpaka wakafia Ikulu baadhi, hakuna mwananchi aliyewapinga na kuwaondoa bila ya kuwa na intervening forces kama vita vya dunia au na nchi jirani (Tanzania na Amin). Dictators wanatawala kwa mkono wa chuma, hakuna cha ridhaa ya wananchi, ndio maana wanaua!

Hivyo umebakia uamuzi mmoja tu nao ni jeshi kuchukua madaraka na kuandaa muda wa kurejesha utawala wa kiraia.
Sio kila jeshi linapochukua nchi "linaandaa muda wa kurejesha utawala wa kiraia." Linaweza likaja jeshi na likakaa forever.
 
hivi kwa nini siyo tanzania? mbona na sisi tumekichoka chama kilichopo madarakani ila hatuchukui hatua? dowans epa IPTL MFUMUKO WA BEI, MIKATABA MIBOVU NA HUDUMA MBOVU ZA KIJAMII HIVI HATUJAPANDISHA HASILATU?
Tanzania people reflect the leaders themselves too much talking
 
Kwa hali ya kisiasa inavyoendelea kama Mubarak angekuwa na akili angeamuaa tu kutangaza kujiuzulu, kwani kadri inavyoelekea yaweza kutokea mengi zaidi especially vifo. Kadri vifo vinavyoongezeka na hasira za wana Egypt inazidi kukuwa,
Matokeo:: Kama jeshi litachukuwa nchi kwa lazima, na kama vifo vitaendelea basi atakapotelewa kwa lazima Mubarak baadae anaweza kushitakiwa kwa kusababisha mauaji nchi misri na uharibifu wa mali... Mimi ningeona ni busara kama angeamua tu kujiondoa kama wamisri wanavyotaka.

Misri hawataki changes za viongozi (prime minister), wanataka Husni atoke, hiyo ndo anatakiwa afanye .
 
ni kweli jeshi halitaki kabaisa kuua raia na limekuwa very friendly to people kwani wana diriki hata kuvuta sigara na kugongesheana,wanawapa hadi simu protesters, ndio maana leo police wote wameamuliwa kurudi barabarani tena baada ya juzi kutolewa.
Hii inaonyesha kuwa Jeshi pia limeshachoka na Mbaraka.
 
ni kweli kabisa , hao jamaa wanasemekana wanataka kuanzisha SHARIA, hapo hapo insemekana tatizo sio wananchi tu bali ni hao Brotherhood kutopendezwa na ushirika uriopo kati ya USA na Egypt hivyo wakiingia madaraka tegemea mabadiliko mengi sana.
Kuna swala jingine la Peace treaty with Israel swala ambalo hao jamaa wanaweza kulikataa na kusabbabisha tension kubwa mashariki ya kati.
Na hayo ndio mambo makubwa ya USA kufumbia u-dictator wa Hosni Mbaraka huku wakihubiri democrasia, huyu jamaa ni mshirika wao mkubwa sana kwa middle east yote na mpaka sasa wanashindwa kujua nininni na kipi kitakachofuata baadaya ya Hosni.
yetu macho
Naambiwa Muslim Brotherhood are the likes of HAMAS na AL-QAEDA ni chama chenye msimamo mkali sana na Serikali ya Marekani wanafanya kila liwezekanalo ili chama hicho kisishike hatamu ya uongozi Misri
 
Nadhani JWTZ wanatamani sana hali hii itokee ili watimize ya kwao. Uporaji + everything.
 
sio kwamba jeshi lipo lipo tu, hawa jamaa wanajua jinsi ya kufanya kazi, hwataki kuuua raisi bila sababu yeyote.
Pia kumbuka kuwa huyo Makamu wa raisi aliyechaguliwa alikuwa ndiye kongozi wa Intelijensia jeshini maana yake ni kuwa wako kazi moja.
Hawa Army wako karibu sana na raia ndio maana utawaona wanavuta sigara na protesters na kufanya mambo mengi tu ya kawaida, kwa kifupi ni kuwa nao wameshamchoka Hosni Mbaraka
.
 
Ushirikiano wa kiusalama wa Misri na Israeli usiku huu utaamua kama Mubarak anasurvive the final assault ya wananchi hii Ijumaa. Kama hadi Jumamosi inapambazuka Mubaraka hajaangushwa sioni kama kuna uwezekano wa kumuangusha kwani vyanzo vyote vya usalama vinadokeza kuwa siku hizi chache zilizopita Misri imepata msaada mkubwa wa kiulinzi toka Israeli katika jitihada za kuvunja maandamano ikiwemo matumizi ya gasi. Hivyo kinachoweza kutokea kesho Ijumaa ni mauaji (watu kuuana kwa sababu kunyagana) kwani watakapopush kuelekea presidential compound zitatimuka mbinu na nguvu za kutawatawanya.

Swali kubwa kiasi gani cha watu Mubarak yuko tayari kuua kuzuia kuondolewa madarakani? Tunakumbuka yaliyotokea China na utawala wa Kichina bado uko madarakani. Kama Mubarak yuko tayari kuua kiasi chochote cha watu kuzuia kuondolewa kwa nguvu na jeshi likawa tayari kufanya kazi hiyo in the name of the "state" basi Mubarak ataendelea kuwepo.
 

Mkulu
Heshima mbele, siyo sahihi kusema jeshi litachukua nchi na baada ya muda watarejesha utawala wa kiraia.

Sitaki kuamini kwamba hujui kuwa Mubarak si kiongozi wa kiraia, Mubarak ni Mwanajeshi si raia.Egypt hawajawahi kuwa chini ya Utawala wa Kiraia(democratically elected regime)

Egypt haitaongozwa na jeshi tena,wananchi wa Egypt wametoa maagizo kwamba siku ya mwisho ya kiongozi huyu ni friday, they choose this day wakijua kuwa, leo ni siku ya ibada,watu watakwenda kwenye swala ya ijumaa na watamwomba ALLAH AWANUSURU na huyu mtu,then wakitoka misikitini utasikia SHUGHULI ITAKAYOFUATA HAPO NI KUBWA..nguvu hiyo hata jeshi wataweza kuizuia

Mubarak aondoke ofisini kabla ya hawa watu wahajamaliza swala.........najaribu ku-imagine kitakachotokea, NAOGOPA.

MM watu wananguvu kuliko jeshi.
 

Mkulu
Heshima mbele,natofautiana kwa kiwango kikubwa sana kuhusu mtazamo wako juu ya jeshi la Egypt.

Hilo ndilo what we describe as A PROFESSIONAL ARMY, ni jeshi la wananchi, siyo jukumu lao kutumia nguvu kwa wananchi wao, wanalielewa hilo na wanaliweka kwenye vitendo.Picha zile wanazopigwa na watu wa habari zikionesha wanajeshi wamebeba watoto na kukaa nao kwenye vifaru na nyingine kizee kimoja kinambusu mwanajeshi aliyejuu ya kifaru...zimenifanya macho yangu yajae machozi...its......ahhh

I WISH HIZI PICHA VIONGOZI WA JESHI LETU(TPDF/JWTZ) WAZIONE, NAAMINI WAMEZIONA AND MANY MORE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…