Jeshi la zimamoto Manyara

Jeshi la zimamoto Manyara

nawenge

Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
18
Reaction score
9
Hivi sheria gani mnayotumia kukusanya michango kwa wafanyabiashara mjini babati. Ninavyofaham mm kama ilivyo kwa majeshi mengine, Jeshi la zimamoto ni kikosi halali kilicho chini ya wizara ya mambo ya ndani kama police nk. Kitendo cha wananchi/wafanyabiasha kuchangia jeshi hili ni cha nchi nzima? Je serikari imeshindwa kuhudumia kikosi hiki? Tunachangishwa pesa hizi kwa lazima na wakati mwingine wanasema watawapeleka mahakamani wale wote wasiochanga pesa hizo. Wanatumia kigezo cha watanzania wengi kutokujua sheria na woga wa mahakama na vurugu/vita. Wanachangisha pesa hizi na kisha wanatoa certificate tena zenye expire date na yaonesha hili zoeli ni endelevu. LEO TUNACHANGIA ZIMAMOTO, KESHO WAKIJA JWTZ NA SHERIA YAO TUTAGOMA? MSAADA KWENU MJUAO SHERIA. Hii cert mimi ninayo tena kwa jina langu.
 
Mkuu Kwanza pole kwa kuchangishwa.
Pili naamini wewe ni msomi. Hebu soma hicho cheti vizuri mpaka mwisho then utapata jibu la maswali yako.
Kumbuka kutokubadili maneno yako pindi moto utakapotokea na ukashindwa kulipwa bima kwa sababu ya kutokuwa na hicho cheti.
Kosa Lao kubwa ni kwamba hawawaelimishi watu kwanza.
 
sawa ndugu, lakini kauli mbiu yao ni kwamba wanataka kununua magari sababu wana upungufu wa magari hayo, lakini hatuoni hayo magari na muda wa ile cert (validity period of awarded cert) unaishia feb 2015.
Tuambiwe je hii ndo bima ya majanga ya moto? Na swali kuu Je mchangisho huu ni kwa nchi nzima? na Je ni kwa zima moto peke yao?
 
Back
Top Bottom