Jeshi La Wananchi waendelea na Operation ya kupiga Raia Mtwara

Safi sana, hamtokuwa madketa wa kwanza kaitka dunia hii. kicheko chenu ni cha kasi kama mabomba yatakavo kuja na kitakatika kwa kasi mpaka mtashangaa, jipe muda tu na utakumbuka kama ni duwa la kuku au nini. na naomba usije kubadilishe jina kujifanya ulikuwa mmoja wetu. Leo sisi ni wanyonge sana lakini tunapajua tunapokwenda
Haha ha nyie ni wanyonge, kwa iyo unyonge wenu ndo unawanya mlazimishe gesi isije mjini,tena mnatumia neno GESI YETU basi na ss wa kilimanjaro tuseme madini yetu,mbuga yetu,mlima wetu,hivi hizo rasilimali tulizo nazo apa kilimanjaro tungesema na sisi tuzizuie kwa aji ya manufaa ya mkoa wetu si kilimanjaro na arusha ilishakuwa new york,namalizia hivii,,gechi lachima ije darechalamul
 
Wacha wafanye kazi kudhiwadhibiti makundi ambayo yalikuTatizo siyo wanajeshi, wao wapo hapa kuufanya mji wa Mtwara na vitongoji vyake utawalike uwe na amani na utulivu watu waendelee na shughuli zao za kujitafutia ridhiki na maendeleo bila vitisho vya wenyewe kwa wenyewe eti tu kwa kuwa humuungi mkono Murji na Chama Cha CUF.

Jeshi lipo hapa kukomesha tabia iliyotaka kuota mizizi ya kuathiri maisha ya watu kwa kila siku kuanzisha fujo wenyewe waratibu wanaita KIMENUKA AU LIMENUKA kupora na kuchoma nyumba za watu mali za serikali Mahakama ili kusipowepo utawala wa sheria na kesi za wezi zifutwe kufunga huduma za jamii na kuleta kero kubwa na athari kubwa kwa maisha ya kawaida ya kila siku.

Jeshi lilikuja baada ya kundi hilo la watu kulitishia jeshi la polisi na kutekeleza vitisho vyao na kulifanya lisifanye kazi zake ikiwa pamoja na kupora mali zao na kuwachomea nyumba zao moto kulazimisha watu waliyowapangisha kuwafukuza vinginevyo watawachomea moto nyumba zao kuwalazimisha kutumia bunduki na wakitumia wanashitakiwa na kuwafanya wawe waoga katika kukabiliana na makundi hayo ya vijana waporaji kitendo kinachowapa nafasi za kuendeleza fujo hizi wakishangilia kuwa polisi wamewashinda

Mpaka kufikia hapa wananchi wa Mtwara wanaishukuru serikali kwa kuamka na kuwadhibiti watu hao wakorofi wanaokuwa wanalazimisha watu kufunga maduka kusimisha huduma za usafiri kufunga soko kuu na kufanya maisha kuwa magumu sana sana mjini hapa kila kukicha na watu kukaa kwa hofu kubwa.

Hata hivyo serikali imechelewa sana kuchukuwa hatua hii hadi watu kupoteza maisha yao, serikali kupoteza mali zake na uharibufu mkubwa kufanywa na makundi hayo hatari mkoani kwetu ambayo yanajulikana na yalianza kupandisha bendera ya utawala wao ndani ya utawala hili ni hatari mwishoni mwa mwaka jana kwa kisingizio cha gesi.

Serikali inalaumiwa kwa kumwacha DC Wake Wilman Ndile akilea kuviimarisha vikundi hivi tangu Desemba mwaka jana mpaka vikapata mimba na kuzaa mauti na bado yupo anawafariji na kuwapa moyo.

Chanzo au kiini kinachowaathiri wananchi wa Mtwara kilicho nyuma ya pazia ni Siasa na kugombea madaraka gesi inatumika kama pazia au fimbo ya kuwashikisha wananchi wapingane wenyewe kwa wenyewe.

CUF wameibuwa mgogoro huu na kwa kutumia vitisho na uelewa mdogo wa wananchi kujenga chuki kati ya wananchi na serikali na CCM jambo ambalo linaonekana kupata nguvu.
Kama wananchi wangekuwa na uelewa na kama siyo kutishiwa kuchomewa majumba moto kuuwawa kwa wale wanaobaika kutokukubaliana na upande wao ingetowa fursa ya kupinga hoja za CUF za kupinga ujenzi wa Bomba la Gesi la kupeleka Rasimali hii sokoni kuuzwa kwa ajili ya manufaa ya Mtwara na Taifa kijumla kuliko kukaa nayo majumbani kama wanavyotaka wao CUF tuamini kuwa ndiyo italeta maendeleo kwa vipi.

Tunawauliza CUF chini ya Lipumba kama wakichukuwa nchi gesi hii hamtauza mtauzia wapi? na mwekezaji wenu kutoka Dubai aendelee kuchimba bila kuuza hatapata Hasara? Maana mimi ninajua Lipumba ni ni msomi anajua kuwa rasimali hi anaeiendeleza kwa kuivuna siyo serikali na mfanyabiashara ambaye anataka auze na apate faida na serikali ipate faida.

CUF ninyi mkichukuwa nchi hii gesi mtaipeleka sokoni kwa njia gani ambayo huyo mwekezaji wenu kutoka Oman atapata faidia au ninyi mtauza wapi soko leni liliko Newala Masasi na Tandahimba tu maana hamtaki kuuza nje haitoki?

CUF Kwa nini tu gesi hamtaki kuuza nje korosho hamjui ikibanguliwa Mtwara yote hao wananchi mnaowalazimisha waunge mkono watanufaika zaidi kuliko gesi?

CUF Tueleze nchi gani iliyo na gesi ambayo haiuzwi nje hapo na haisafirishwi kwa bomba?

CUF kazi ya serikali siyo kujenga viwanda hiyo ni kazi ya wafanyabiashara kazi ya serikali ni kujenga miundo mbinu ya kuwavutia wawekezaji sasa unaposema ahadi ya ccm ni ya uwongo ulitaka hivyo viwanda vilivyoahidiwa vijengwe kwa miaka miwli ni vya aina gani hiyo ya viwanda?Hapo Dar Mwanza hadi kuwa miji ya viwanda viljengwa kwa miaka mitano?

Kingine katika sakata hili ni ugomvi wa Murji wa kutaka kutawala mkoa mzima kwa kuwaweka viongozi wa kuchaguliwa wanaomtii yeye ili waweze kutawaliwa kwa remote control kwa maslahi ya kulinda biashara zake.

Ugomvi unakuja anapota wanaompinga na kushindwa Hapo Muhindi huyu kwa kutumia pesa alizochuma mikononi mwetu kutuangamiza wenyewe bila huruma kwa kuwachochea mtandao wa vijana wake wa tukale wapi na kuwatishia watu wakubaliane na anavyotaka bwanamkubwa wao vinginevyo watachomewa nyumba moto.

Murji kupitia mtandao wake wa mafia ameweka viongozi wa serikali katika ngazi ya kata zote mjini Mtwara yaani madiwani wanajulikana kama madiwani wa Murji katika katika uchaguzi wa Chama mwaka jana alijitahidi kusimika viongozi kunazia ngazi ya kata wilaya na mkoa lakini akakwama ngazi ya mkoa katika nafasi ya mwenyekiti na baadhi ya wajumbe.

Aliyokuwa anapambana nao ni wazalendo wabunge wote wa Mkoa huu wakiongozwa na Mkuchika na Hawa Ghasia ambapo.
Kitendo hicho ndicho alichoaapa Murji mbele ya watu na katika vikao kuwa Mwenyekiti huyo wa CCM na baadhi ya wajumbe hawaongoza chama hiki kwa amani na utulivu yeye akiwa hai na kwamba atakiadhibu kwa kuhakikisha hakiongozeki na kushindwa katika chaguzi pamoja na kuwahamisha wananchama kuwapeleka upinzani Mpaka CCM wampigie magoti na kumwondoa Sinani

Pia anatamba kuwa jimbo la Ghasia linachukuliwa na wapinzani wakitaka kwa kumwadabisha Ghasi asigombee tena ubunge hivyo hivyo kwa Mkuchika kisa kumpinga bwana mkubwa huyu wa India.

Kutokana na mgogoro huu ndipo Murji alipowasaliti wananchi wa Mtwara na serikali kwa kuungana na wapinzani na CCM yake yote ya wilaya kupinga bomba la gesi bila hoja za msingi bali kuiokomoa CCM.

Haya ndiyo maeneo mawili ya msingi ya vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyopo Mtwara ambayo nje ya Mtwara imepewa jina la Rasimali kuwanufaisha wananchi wa maeneo inakotoka, ahadi hewa na mengine mengi ambayo yamebeba mwamvuli wa Wananchi wa Mtwara au kusini kumbe ni mgogoro wa CUF NA CCM NA MURJI NA HAWA GHASIAMKUCHIKA NA CCM.

KATIKA HALI HII KAMA SERIKALI ISINGELETA JESHI KATIKA MKOA HUU HALI INGEKUWA MBAYA SANA MAANA UTAWALA WA SHERIA ULISHAANZA KUTOWEKA KWA KUCHOMA MAHAKAMA MOTO KUWACHOMEA MAHAKIMU NYUMBA ZAO MOTO
wa na malengo tofuti na yanayodaiwa kama haya hapa chini.
 
Hata wafanyeje gesi haitoki katika utawala huu wa jk.t. Nipo mtwara kweli wanajeshi wanapiga raia. juzi walienda kupiga wananchi wa Newala sababu hawakufungua maduka yao kuwaunga mkono waliofikishwa mahakamani siku hiyo. Hata wapige raia vp,haitabadilisha msimamowa wanamtwara. jifunzeni kupitia maeneo mengine yenye raslimali. ipo siku mtatupigia makofi nya..u nyie!
 
Kama mnafanya fujo serikali iwachekee? Kilochotokea Mtwara ni uasi. Lazima uzimwe kwa nguvu zote.
 
gesi haitoki,then????hiyo ni product kama unataka kupata faida zake lazima uuze kwa wateja wanaoihitaji,sasa kama wateja wengi wapo dar kwa nini wasiuziwe?tatizo wamekaririshwa kuwa gesi inakuja dar kwa ajili ya umeme tu na wao bila kutaka kujua zaidi wameridhika na hiyo story.huko ulaya watu wanajenga mabomba marefu kusafirisha gesi kufuata wateja sasa hapa kwetu siasa uchwara ndio zinatuangamiza.
Kama wanaohitaji ni watu wa Dar tu basi ni rahisi kusafirisha kwa mitungi
kuliko Bomba, kama inahitajika maeneo mengine ya nchi kama Mwanza, Mbeya
Arusha n.k ina maana mabomba yatasambazwa nchi nzima?
 
Tz bana, wajeshi hawaoni twiga wakipanda ndege, wala hawaoni tembo wakiteketea, sijui ni miwani ya mbao??

Sasa hili geshi kwanini lisikamate na majangili? Linalinda mipaka gani wakati majangili wanapita mumo humo. Mambo kama haya ndiyo yanawafanya watu wafikirie kuwa kuna double standard katika maamuzi mengi
 
Wacha wafanye kazi kudhiwadhibiti makundi ambayo yalikuTatizo siyo wanajeshi, wao wapo hapa kuufanya mji wa Mtwara na vitongoji vyake utawalike uwe na amani na utulivu watu waendelee na shughuli zao za kujitafutia ridhiki na maendeleo bila vitisho vya wenyewe kwa wenyewe eti tu kwa kuwa humuungi mkono Murji na Chama Cha CUF.

Jeshi lipo hapa kukomesha tabia iliyotaka kuota mizizi ya kuathiri maisha ya watu kwa kila siku kuanzisha fujo wenyewe waratibu wanaita KIMENUKA AU LIMENUKA kupora na kuchoma nyumba za watu mali za serikali Mahakama ili kusipowepo utawala wa sheria na kesi za wezi zifutwe kufunga huduma za jamii na kuleta kero kubwa na athari kubwa kwa maisha ya kawaida ya kila siku.

Jeshi lilikuja baada ya kundi hilo la watu kulitishia jeshi la polisi na kutekeleza vitisho vyao na kulifanya lisifanye kazi zake ikiwa pamoja na kupora mali zao na kuwachomea nyumba zao moto kulazimisha watu waliyowapangisha kuwafukuza vinginevyo watawachomea moto nyumba zao kuwalazimisha kutumia bunduki na wakitumia wanashitakiwa na kuwafanya wawe waoga katika kukabiliana na makundi hayo ya vijana waporaji kitendo kinachowapa nafasi za kuendeleza fujo hizi wakishangilia kuwa polisi wamewashinda

Mpaka kufikia hapa wananchi wa Mtwara wanaishukuru serikali kwa kuamka na kuwadhibiti watu hao wakorofi wanaokuwa wanalazimisha watu kufunga maduka kusimisha huduma za usafiri kufunga soko kuu na kufanya maisha kuwa magumu sana sana mjini hapa kila kukicha na watu kukaa kwa hofu kubwa.

Hata hivyo serikali imechelewa sana kuchukuwa hatua hii hadi watu kupoteza maisha yao, serikali kupoteza mali zake na uharibufu mkubwa kufanywa na makundi hayo hatari mkoani kwetu ambayo yanajulikana na yalianza kupandisha bendera ya utawala wao ndani ya utawala hili ni hatari mwishoni mwa mwaka jana kwa kisingizio cha gesi.

Serikali inalaumiwa kwa kumwacha DC Wake Wilman Ndile akilea kuviimarisha vikundi hivi tangu Desemba mwaka jana mpaka vikapata mimba na kuzaa mauti na bado yupo anawafariji na kuwapa moyo.

Chanzo au kiini kinachowaathiri wananchi wa Mtwara kilicho nyuma ya pazia ni Siasa na kugombea madaraka gesi inatumika kama pazia au fimbo ya kuwashikisha wananchi wapingane wenyewe kwa wenyewe.

CUF wameibuwa mgogoro huu na kwa kutumia vitisho na uelewa mdogo wa wananchi kujenga chuki kati ya wananchi na serikali na CCM jambo ambalo linaonekana kupata nguvu.
Kama wananchi wangekuwa na uelewa na kama siyo kutishiwa kuchomewa majumba moto kuuwawa kwa wale wanaobaika kutokukubaliana na upande wao ingetowa fursa ya kupinga hoja za CUF za kupinga ujenzi wa Bomba la Gesi la kupeleka Rasimali hii sokoni kuuzwa kwa ajili ya manufaa ya Mtwara na Taifa kijumla kuliko kukaa nayo majumbani kama wanavyotaka wao CUF tuamini kuwa ndiyo italeta maendeleo kwa vipi.

Tunawauliza CUF chini ya Lipumba kama wakichukuwa nchi gesi hii hamtauza mtauzia wapi? na mwekezaji wenu kutoka Dubai aendelee kuchimba bila kuuza hatapata Hasara? Maana mimi ninajua Lipumba ni ni msomi anajua kuwa rasimali hi anaeiendeleza kwa kuivuna siyo serikali na mfanyabiashara ambaye anataka auze na apate faida na serikali ipate faida.

CUF ninyi mkichukuwa nchi hii gesi mtaipeleka sokoni kwa njia gani ambayo huyo mwekezaji wenu kutoka Oman atapata faidia au ninyi mtauza wapi soko leni liliko Newala Masasi na Tandahimba tu maana hamtaki kuuza nje haitoki?

CUF Kwa nini tu gesi hamtaki kuuza nje korosho hamjui ikibanguliwa Mtwara yote hao wananchi mnaowalazimisha waunge mkono watanufaika zaidi kuliko gesi?

CUF Tueleze nchi gani iliyo na gesi ambayo haiuzwi nje hapo na haisafirishwi kwa bomba?

CUF kazi ya serikali siyo kujenga viwanda hiyo ni kazi ya wafanyabiashara kazi ya serikali ni kujenga miundo mbinu ya kuwavutia wawekezaji sasa unaposema ahadi ya ccm ni ya uwongo ulitaka hivyo viwanda vilivyoahidiwa vijengwe kwa miaka miwli ni vya aina gani hiyo ya viwanda?Hapo Dar Mwanza hadi kuwa miji ya viwanda viljengwa kwa miaka mitano?

Kingine katika sakata hili ni ugomvi wa Murji wa kutaka kutawala mkoa mzima kwa kuwaweka viongozi wa kuchaguliwa wanaomtii yeye ili waweze kutawaliwa kwa remote control kwa maslahi ya kulinda biashara zake.

Ugomvi unakuja anapota wanaompinga na kushindwa Hapo Muhindi huyu kwa kutumia pesa alizochuma mikononi mwetu kutuangamiza wenyewe bila huruma kwa kuwachochea mtandao wa vijana wake wa tukale wapi na kuwatishia watu wakubaliane na anavyotaka bwanamkubwa wao vinginevyo watachomewa nyumba moto.

Murji kupitia mtandao wake wa mafia ameweka viongozi wa serikali katika ngazi ya kata zote mjini Mtwara yaani madiwani wanajulikana kama madiwani wa Murji katika katika uchaguzi wa Chama mwaka jana alijitahidi kusimika viongozi kunazia ngazi ya kata wilaya na mkoa lakini akakwama ngazi ya mkoa katika nafasi ya mwenyekiti na baadhi ya wajumbe.

Aliyokuwa anapambana nao ni wazalendo wabunge wote wa Mkoa huu wakiongozwa na Mkuchika na Hawa Ghasia ambapo.
Kitendo hicho ndicho alichoaapa Murji mbele ya watu na katika vikao kuwa Mwenyekiti huyo wa CCM na baadhi ya wajumbe hawaongoza chama hiki kwa amani na utulivu yeye akiwa hai na kwamba atakiadhibu kwa kuhakikisha hakiongozeki na kushindwa katika chaguzi pamoja na kuwahamisha wananchama kuwapeleka upinzani Mpaka CCM wampigie magoti na kumwondoa Sinani

Pia anatamba kuwa jimbo la Ghasia linachukuliwa na wapinzani wakitaka kwa kumwadabisha Ghasi asigombee tena ubunge hivyo hivyo kwa Mkuchika kisa kumpinga bwana mkubwa huyu wa India.

Kutokana na mgogoro huu ndipo Murji alipowasaliti wananchi wa Mtwara na serikali kwa kuungana na wapinzani na CCM yake yote ya wilaya kupinga bomba la gesi bila hoja za msingi bali kuiokomoa CCM.

Haya ndiyo maeneo mawili ya msingi ya vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyopo Mtwara ambayo nje ya Mtwara imepewa jina la Rasimali kuwanufaisha wananchi wa maeneo inakotoka, ahadi hewa na mengine mengi ambayo yamebeba mwamvuli wa Wananchi wa Mtwara au kusini kumbe ni mgogoro wa CUF NA CCM NA MURJI NA HAWA GHASIAMKUCHIKA NA CCM.

KATIKA HALI HII KAMA SERIKALI ISINGELETA JESHI KATIKA MKOA HUU HALI INGEKUWA MBAYA SANA MAANA UTAWALA WA SHERIA ULISHAANZA KUTOWEKA KWA KUCHOMA MAHAKAMA MOTO KUWACHOMEA MAHAKIMU NYUMBA ZAO MOTO
wa na malengo tofuti na yanayodaiwa kama haya hapa chini.

N.B Tulisahau kuwaeleza kuwa Taarifa hii imeandaliwa na KATIBU WA PROPAGANDA ZA CCM
kanda ya kusini.
 
Kama wanaohitaji ni watu wa Dar tu basi ni rahisi kusafirisha kwa mitungi
kuliko Bomba, kama inahitajika maeneo mengine ya nchi kama Mwanza, Mbeya
Arusha n.k ina maana mabomba yatasambazwa nchi nzima?

gesi isafirishwe kwa mitungi wakati kuna njia cheap ya kuipeleka kwa bomba?
 
wanachodai wanantwara hakina budi kuungwa mkono na watanzania wote,kwani kuna maeneo mengi kuna rasilimali lakini wenyeji hawanufaiki mwaka huu mgodi wa Tulawaka uliopo Runzewe unafungwa nenda kaangalie maisha ya wanajamii yalivyo mabovu,Mgodi wa Golden Pride Nzega unafungwa mwaka huu pia nenda kaangalie alichofanya mwekezaji kwa wanajamii hamna kitu.Ipo haja kuangalia jamii jirani na watanzania kiujumla tunanufaika vipi na resource tuache ushabiki usio na maana.
watuwezi kuunga mkono wakati hamtaki na wa2 walionje ya mtwara tufaidike,,cha msingi mmeshaelimishwa hamtaki kuelewa so endeleeni kuleta vurugu alafu 2one ka ndo mtapata hayo maendeleo,..mtawapa watu wengine ulaji kutokana na izo vurugu kama jwtz na kamati kibao....
Jaribuni kuelewa kinachozungumzwa
 
Nina wasiwasi Mtwara kutakua na Raia wa Nchi jirani wengi sana na ndio maana Serekale imepeleka full vifaa vya kijeshi kumaanisha kwamba hilo ni onyo tu.
 
Si majuzi mliweka post mkasema kuwa askari wa jeshi la wananchi wamepokelewa kwa shangwe na wana mtwara na wamekuwa kama marafiki na walinzi wao kuliko polisi?? sasa imekuwaje tena?Naanza kuacha kuwaamini wa huko kwenye gesi ya mgogoro!!
Hahahaaaaa!umenichekesha sana.ila mwanadamu ndivyo alivyo!waliwapokea jwtz kwa shangwe Leo wanawalalamikia.hata Yesu alipokelewa kwa shangwe na wanadamu na baadae wanadamu wakamsulubisha.kazi kweli kweli
 
Kile kinachoonekana kama kutumia nguvu kubwa na kukiuka haki za binaadamu,jeshi la wananchi linaendelea na utekelezaji wa order waliyopewa na mkuu wa nchi kupiga watu,leo asubuhi JWTZ wamevamia eneo la Magomeni Manispaa ya Mtwara Mikindani na kuendelea na Operation ya kupiga Raia.

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lilianzishwa tarehe 01 Septemba 1964 Kwa lengo la kulinda mipaka ya nchi .

Tunajipanga na Rwanda wala hatuna muda na hao watoto wa ndani ambao polisi inawatosha kuwanyamazisha
 
Si majuzi mliweka post mkasema kuwa askari wa jeshi la wananchi wamepokelewa kwa shangwe na wana mtwara na wamekuwa kama marafiki na walinzi wao kuliko polisi?? sasa imekuwaje tena?Naanza kuacha kuwaamini wa huko kwenye gesi ya mgogoro!!

Yaani ile nataka kuuliza swali hilihili,naona xomment yako mkuu! Sasa tutaanza kutowaamini hawa wanaojiita wana mtwara kwani wanatuletea hadithi ya kijana mchungaji na mbwa mwitu-maarufu kama Crying Wolf!
 
Huwa najiuliza kwanini M/Mungu AMETUPA AKILI karibu watu wote japo si wote lakini HAKUTUPA BUSARA.Hili suala la Mtwara linahitaji BUSARA TU.Hii inamaana kweli ndani ya baraza la mawaziri ambalo kwa wiki wanakaa si chini ya mara moja hakuna mwenye busara ya kuona hatari ya kuingiza jeshi mtaani kujibu hoja ya wana Mtwara.Kweli naamini sasa KUFIKIRI ni kazi ngumu ndo maana wengi wetu hatuifanyi hiyo kazi.Ipo siku jeshi litaasi.

Acha kuwajaza nduguzo ujinga. Busara ilishatumika mkabembelezwa mtoto wa mkulima akahamia huko lkn kichwa ngumu hamuelewi sasa kilichobaki ni kichapo kwa kwenda mbele. JWTZ kaza buti hakuna kucheka na kima tutavuna mabua. Hakuna mjinga anayeweza kuendelea kuwaendekeza. Huu sasa ni upuuzi na laiti ningekuwa Amiri Jeshi ningetoa kichapo ambacho hakijawahi kutoikea kusini mwa sahara. Acheni upuuzi la nendeni MOSAMBIQUE.

 
Haha ha nyie ni wanyonge, kwa iyo unyonge wenu ndo unawanya mlazimishe gesi isije mjini,tena mnatumia neno GESI YETU basi na ss wa kilimanjaro tuseme madini yetu,mbuga yetu,mlima wetu,hivi hizo rasilimali tulizo nazo apa kilimanjaro tungesema na sisi tuzizuie kwa aji ya manufaa ya mkoa wetu si kilimanjaro na arusha ilishakuwa new york,namalizia hivii,,gechi lachima ije darechalamul
Nilidhani najadili na mtu mweye uelewa kumbe ni wale wale wapika majungu, ni wapuuzi tu wanaozungumza gesi yetu, madini yetu, swala ni manufaa gani yanayo patikana, ni wazi hili swala la gesi lima mambo mengi tu ya kifisaadi ndani yake,...hivyo kapitie vizuri ndiyo uje tena...mfano mdogo ni jinsi tanzanite isivyo tufaidisha
 
Back
Top Bottom