GE2025 Jeshi la Polisi: Tumewadhibiti wafuasi wa CHADEMA walioleta fujo Mahakama Kuu Dar es salaam

GE2025 Jeshi la Polisi: Tumewadhibiti wafuasi wa CHADEMA walioleta fujo Mahakama Kuu Dar es salaam

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Polisi naona wanajidai wenyewe kwamba wamewadhibiti. Ila hawa jamaa

Tarehe 15 Septemba, 2025 majira ya asubuhi eneo Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakati mashauri mbalimbali yakiendelea, lilijitokeza kundi la Wanachama wa CHADEMA baada ya ukumbi uliokuwa unatumiwa kwenye kesi ya Tundu Lissu kujaa na hivyo baadhi ya wafuasi hao waliokuwa nje ya Mahakama walianzisha fujo na kujaribu kuwashambulia askari ambao walijilazimisha na kutuliza fujo hizo haraka.

Jeshi la Polisi linatoa wito kuwa kitendo chochote cha kuwachokoza askari kitashughulikiwa haraka na kuyarejesha mazingira ya usalama kwenye eneo husika haraka kwa kadiri inavyowezekana.

Screenshot 2025-09-15 195849.png
 
Nawapongeza polisi huyo mtu alierusha ngumi ilitakiwa wamvunje mkono ili iwe fundisho kwa wavunjaji wengine wa sheria
 
Polisi naona wanajidai wenyewe kwamba wamewadhibiti. Ila hawa jamaa

Tarehe 15 Septemba, 2025 majira ya asubuhi eneo Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakati mashauri mbalimbali yakiendelea, lilijitokeza kundi la Wanachama wa CHADEMA baada ya ukumbi uliokuwa unatumiwa kwenye kesi ya Tundu Lissu kujaa na hivyo baadhi ya wafuasi hao waliokuwa nje ya Mahakama walianzisha fujo na kujaribu kuwashambulia askari ambao walijilazimisha na kutuliza fujo hizo haraka.

Jeshi la Polisi linatoa wito kuwa kitendo chochote cha kuwachokoza askari kitashughulikiwa haraka na kuyarejesha mazingira ya usalama kwenye eneo husika haraka kwa kadiri inavyowezekana.

Mkalukungone Mwamba inaelekea wewe uliambiwa. Kama uliambiwa ulipotoshwa. Polisi ndio waliwashambulia raia ambao hawakua hata na tooth pick.
Video zipo mitandaoni kama utahitaji kujiridhisha.
 
Polisi hivi ndio mnazidi kuharibu mnahisi siku wakiandamana maelf mkitumia virungu na wao wakatumia mawe nani ataloose?
 
Polisi naona wanajidai wenyewe kwamba wamewadhibiti. Ila hawa jamaa

Tarehe 15 Septemba, 2025 majira ya asubuhi eneo Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakati mashauri mbalimbali yakiendelea, lilijitokeza kundi la Wanachama wa CHADEMA baada ya ukumbi uliokuwa unatumiwa kwenye kesi ya Tundu Lissu kujaa na hivyo baadhi ya wafuasi hao waliokuwa nje ya Mahakama walianzisha fujo na kujaribu kuwashambulia askari ambao walijilazimisha na kutuliza fujo hizo haraka.

Jeshi la Polisi linatoa wito kuwa kitendo chochote cha kuwachokoza askari kitashughulikiwa haraka na kuyarejesha mazingira ya usalama kwenye eneo husika haraka kwa kadiri inavyowezekana.

Ila hili jeshi nalo jau sana
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kutokea kwa vurugu katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo wakati shauri la kiongozi wa CHADEMA, Tundu Lissu likiendelea kusikilizwa, ambapo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro amesema vurugu hizo zilihusisha baadhi ya wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao walikuwa wamekusanyika nje ya ukumbi wa Mahakama uliokuwa ukisikiliza kesi ya Tundu Lissu na baadhi ya wafuasi waliokuwa nje kuanza kufanya fujo na kuwashambulia Askari.

"Baadhi ya wafuasi waliokuwa nje ya Mahakama walianzisha fujo na kujaribu kuwashabulia askari ambao walikuwa eneo hilo, askari polisi walijihami na kufanikiwa fujo hizo haraka"

 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kutokea kwa vurugu katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo wakati shauri la kiongozi wa CHADEMA, Tundu Lissu likiendelea kusikilizwa, ambapo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro amesema vurugu hizo zilihusisha baadhi ya wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao walikuwa wamekusanyika nje ya ukumbi wa Mahakama uliokuwa ukisikiliza kesi ya Tundu Lissu na baadhi ya wafuasi waliokuwa nje kuanza kufanya fujo na kuwashambulia Askari.

"Baadhi ya wafuasi waliokuwa nje ya Mahakama walianzisha fujo na kujaribu kuwashabulia askari ambao walikuwa eneo hilo, askari polisi walijihami na kufanikiwa fujo hizo haraka"
Tumekuwa wajinga sasa hata video hatuzielewi
 
Moja ya makamanda wa polisi wa hovyo kuwahi kutokea nchini, nadhani huyo munani sijui yuko kwenye 3 bora! Kwa hiyo vijana wake ndiyo wana haki ya kushambulia raia wasio na hatia, kuwajeruhi, kuwaua, nk! Ila wakishambuliwa wao ni kesi ya jinai!

Kumbe ndiyo maana kuna watu huwa wanafurahia sana hao askari wanapopata ajali na kufa.
 
Back
Top Bottom