Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,555
- 41,063
Tungekuwa tupo katika nchi zilizostaarabika, wakati huu, uongozi wote wa Jeshi la Polisi ungekuwa umeshaondolewa kwa mambo ya ajabu yanayofanywa na jeshi hili yanayoashiria kukosekana kwa weledi ndani ya chombo hiki.
Jeshi la Polisi linapofanya kazi ya kuwatengenezea watu kesi za kubumba ili kuwatesa na kuwaumiza, linakuwa halina tofauti na kikundi cha kigaidi. Jeshi la Polisi, kinyume na matakwa ya sheria iliyoanzisha jeshi hili, limegeuka na kuwa kikundi cha kuwatisha watu wasikemee uovu au makosa yanayofanywa na dola dhidi ya umma.
Inawezekana vipi ndani ya jeshi zima wakosekana watu ambao wanaelewa hata tafsiri tu au vitendo na mazingira ya mtu kuweza kufanya ugaidi?
Huko siku za nyuma, wakati wa utawala wa Ali Hassan Mwinyi, mchungaji Mtikila, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, akiwa anapinga muundo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwenye mkutano uliohudhuriwa na maelfu ya watu kwenye viwanja vya Jangwani, aliwahi kunena.
"Huyu Rais Mwinyi ambaye ni tx, tunamwambia aende kwao. Hivi hajui nini hutokea watu wanapokataa kutawaliwa? Watanzania ni watu wa amani, tunataka Mwinyi arudi mwenyewe, hatutaki arudi akiwa kwenye jeneza. Watanganyika hawataki kutawaliwa na Tx. Wanasema kuwa sisi ni wa damu moja, wamasai wa Kenya na Tanzania, siyo wa damu moja? Wakurya wa Tarime na wa Kenya, siyo wa damu moja? Kwa ninj hatujawa nchi moja?"
Lakini kauli yake wala haikuwahi kutafsiriwa kuwa ni uhaini. Sababu ni moja, kwa sababu hakukuwa na vitendo wala mazingira yalioshiria kuna nia ya kumwondoa Mwinyi madarakani kwa mapinduzi au kuundoa uhai wake kwa njia yoyote ile ya kupangwa. Na hatukuwahi kusikia mtu yeyote akishtakiwa kwa makosa ya ugaidi au uhaini, nadhani ni kwa sababu wakati huo ndani ya jeshi la Polisi kulikuwa na viongozi waliokuwa na weledi, tofauti na sasa.
Mtu kutamka, "matendo haya ya uuzwaji wa rasilimali za nchi, yakifanyika katika nchi nyingine, Serikali au Rais anaweza kupinduliwa", haiwezi kuwa ni uhaini. Hii ni kauli ya tahadhari. Lazima uwe mjinga sana kuamini kuwa kauli ya tahadhari ni uhaini. Kauli ya tahadhari inawezaje kumwondoa Rais madarakani?
Hivi mtu akikuambia kuwa ukinywa sumu unaweza kufa, maana yake anataka kukuua?
Chini ya katiba mbaya tuliyo nayo, tumeona jinsi utendaji wa Jeshi la Polisi ulivyo mbaya. Tupiganie katiba mpya. Kwa uzoefu wa utendaji mbaya wa Jeshi la Polisi ambao tunaushuhudia, katiba mpya iangalie namna nchi itakavyoweza kuwa na Jeshi la Polisi lenye weledi na litakalofanya kazi kwa kuzingatia sheria zote za ndani ya nchi na za kimataifa. Tukiendelea na jeshi la namna tuliyo nayo, kuna wakati wananchi watashindwa kuvumilia, hivyo watachukua hatua dhidi ya chombo hiki kisichotambua majukumu yake na kinachofanya kazi bila kuzingatia sheria, bali kwa utashi na matakwa ya watawala.
Jeshi la Polisi linapofanya kazi ya kuwatengenezea watu kesi za kubumba ili kuwatesa na kuwaumiza, linakuwa halina tofauti na kikundi cha kigaidi. Jeshi la Polisi, kinyume na matakwa ya sheria iliyoanzisha jeshi hili, limegeuka na kuwa kikundi cha kuwatisha watu wasikemee uovu au makosa yanayofanywa na dola dhidi ya umma.
Inawezekana vipi ndani ya jeshi zima wakosekana watu ambao wanaelewa hata tafsiri tu au vitendo na mazingira ya mtu kuweza kufanya ugaidi?
Huko siku za nyuma, wakati wa utawala wa Ali Hassan Mwinyi, mchungaji Mtikila, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha DP, akiwa anapinga muundo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwenye mkutano uliohudhuriwa na maelfu ya watu kwenye viwanja vya Jangwani, aliwahi kunena.
"Huyu Rais Mwinyi ambaye ni tx, tunamwambia aende kwao. Hivi hajui nini hutokea watu wanapokataa kutawaliwa? Watanzania ni watu wa amani, tunataka Mwinyi arudi mwenyewe, hatutaki arudi akiwa kwenye jeneza. Watanganyika hawataki kutawaliwa na Tx. Wanasema kuwa sisi ni wa damu moja, wamasai wa Kenya na Tanzania, siyo wa damu moja? Wakurya wa Tarime na wa Kenya, siyo wa damu moja? Kwa ninj hatujawa nchi moja?"
Lakini kauli yake wala haikuwahi kutafsiriwa kuwa ni uhaini. Sababu ni moja, kwa sababu hakukuwa na vitendo wala mazingira yalioshiria kuna nia ya kumwondoa Mwinyi madarakani kwa mapinduzi au kuundoa uhai wake kwa njia yoyote ile ya kupangwa. Na hatukuwahi kusikia mtu yeyote akishtakiwa kwa makosa ya ugaidi au uhaini, nadhani ni kwa sababu wakati huo ndani ya jeshi la Polisi kulikuwa na viongozi waliokuwa na weledi, tofauti na sasa.
Mtu kutamka, "matendo haya ya uuzwaji wa rasilimali za nchi, yakifanyika katika nchi nyingine, Serikali au Rais anaweza kupinduliwa", haiwezi kuwa ni uhaini. Hii ni kauli ya tahadhari. Lazima uwe mjinga sana kuamini kuwa kauli ya tahadhari ni uhaini. Kauli ya tahadhari inawezaje kumwondoa Rais madarakani?
Hivi mtu akikuambia kuwa ukinywa sumu unaweza kufa, maana yake anataka kukuua?
Chini ya katiba mbaya tuliyo nayo, tumeona jinsi utendaji wa Jeshi la Polisi ulivyo mbaya. Tupiganie katiba mpya. Kwa uzoefu wa utendaji mbaya wa Jeshi la Polisi ambao tunaushuhudia, katiba mpya iangalie namna nchi itakavyoweza kuwa na Jeshi la Polisi lenye weledi na litakalofanya kazi kwa kuzingatia sheria zote za ndani ya nchi na za kimataifa. Tukiendelea na jeshi la namna tuliyo nayo, kuna wakati wananchi watashindwa kuvumilia, hivyo watachukua hatua dhidi ya chombo hiki kisichotambua majukumu yake na kinachofanya kazi bila kuzingatia sheria, bali kwa utashi na matakwa ya watawala.